Msekwa Atoboa siri ya Butiama

Mr EWA

JF-Expert Member
Mar 15, 2007
331
64
Katika hali isiyokuwa ya kawaida Mzee Msekwa akiwa kwenye mjadala uliendeshwa na TBC1 kuhusu swala la Mwafaka wa Zanziba.

Mzee Msekwa alijikuta ukweli juu ya yaliotokea Butiama ukitoka wenyewe na kama kawaida ya ukweli huwa unatabia ya kutoka wenyewe ukizuiwa kwa mda mrefu.

''Baada ya kubanwa sana na wajuzi wakuuliza maswali alikiri inabidi awe wazi na aseme ukweli na kusema wajumbe wa kutoka Zanziba walio wengi hawakukubali ile rasimu ya mwafaka na kupelekea kuirudisha hoja hiyo kwa wananchi wa zanziba ili waweze kufanya maamuzi juu ya Mwafaka.

''Katika mjadala huo pia msekwa alibainisha mambo mengi sana ya ndani ambayo yalifichwa sana na pengine kwa mtizamo wangu ufafanuzi ulitakiwa kutolewa kwa uwazi kuhusu kilichotokea ili wananchi wajue tatizo hasa ni nini kuliko kuendelea kuficha na alivyoeleza msekwa baada ya kubanwa sana ndio akaamua kusema ukweli.

''Pia kuna mafunzo ambayo niliyapata kutokana na mjadala huo kuwa viongozi wetu wanapaswa kujua pia wananchi wanauelewa mkubwa sana juu ya mambo yanayotokea kwahiyo viongozi wajiepushe kuficha mambo na mfano mzuri ni maswali mazuri aliyoulizwa msekwa na kumpelekea kusema ukweli.

''Funzo la pili ni kuwa viongozi wanapaswa kujua kuwa hakuna siri ya watu wengi kama waliokutana butiama ni wazi pia kilichotokea ni lazima kingesemwa na baadhi ya wajumbe kwahiyo viongozi wanapaswa kutoa maelezo kwa kina kuepusha kutokueleweka vizuri na umma.

''Mwisho nauliza swali kutokana na hayo yaliyotokea je CUF wangetoa kauli ipi? ama wafanyeje kutokana na haya yaliyotokea?
 
Mimi hata siku moja sikutegemea kama CCM wangeliwaachia nafasi wapinzani Zanzibar kilichotoke baadhi ya wana CCM hata wa bara walikijua mapema kuwa kitakuwepo.

Self nafikiri kama kweli anajua Siasa alitakiwa ajue hili pia.
 
Mimi hata siku moja sikutegemea kama CCM wangeliwaachia nafasi wapinzani Zanzibar kilichotoke baadhi ya wana CCM hata wa bara walikijua mapema kuwa kitakuwepo.

Self nafikiri kama kweli anajua Siasa alitakiwa ajue hili pia.
Mh. Seif anajua siasa. Ni mwanasiasa mahiri tu.Lakini tatizo lake kuwa ni hakutulia. Hulka yake ni mtu wa pupa, mtu wa kutumia "excessive forces" pahala panapohitaji busara, mtu wa kusema madhali nataka hili basi na liwe hili-tena sasa hivi, ni mtu mwenye tamaa (yule ambaye hana cha kile mnachoita Plan B), ni mtu ambaye ingawa ni mtetezi na mpambanaji mzuri, inapokuja rehma ana tabia ya kuipapatikia na kusahu hata ile dhamira yake ya kutetea wengine. Hali hii inafanya iwe rahisi kupikuliwa na kufungwa bao na "opponents wake" amabo hutulia na kum-time" vizuri. Huyo Ndiye Maalim Seif.
 
Msikilizaji yeyote makini aliyesikiliza kipindi hicho cha kituo cha serikali cha runginga kwenye channel yake ya TBC1 "This week in perspective" atagundua CCM wako makini zaidi ya CUF kwenye kutafuta huo muafaka.

Mtoa hoja mmoja aliniboa naye ni Dr. Lwaitama ati kwa kuwa Zanzibar imegawanyika kati ya CCM na CUF then kura za maoni zitaleta matokeo yale yale...

Makamu Mwenyekiti wa CCM alijibu vizuri na mimi nikamuelewa. Kwamba... wakati wa kuenda kwenye kura ya Maoni vyama vyote viwili CUF na CCM vimeridhia kwamba iundwe serikali ya Mseto!!! Kwa hivyo watatoka CCM wengi tu watakao kubali huo mfumo...

CCM walichosema ni kwamba lazima kuwe na mfumo utakaoeleweka kwa maana ijulikane kwamba je chama kimoja kitapopata 85% je kutakuwa na lazima ya Serikali ya Mseto... S

Suala lingine ni kwamba already term moja iko zaidi ya nusu, hakuna haja kutaka serikali ya Mseto sasa, tuandae mazingira, tubadilishe katiba... ili baada ya uchaguzi 2010 basi matokeo yakitoka serikali ya mseto itaundwa, kama ameshinda CUF, CCM itashirikishwa pia.

Ieleweka wazi kwamba hata kwenye katiba inasema Rais akishindwa kuongoza nchi kwa namna yoyote ile ilikuwa ni pamoja na kufa, kuugua etc. nadhani baada ya muda fulani makamu wa Rais ataapishwa kuwa Rais moja kwa moja kwa kipindi kinachobakia... lakini ikitokea ni mapema sana ya muhula wake... basi pamoja na makamu wa rais kukaimu lakini pia lazima uchaguzi uitishwe... ndani ya 90days.

CCM wanahoja ambazo CUF wanatakiwa watulie wajadili...

By the way CUF walivunya MOU kwamba makubaliano yoyote yatatangazwa na makatibu wakuu wawili...

Sasa wakalibuka... Juzi tena kabla hata CCM haijawaandikia wakalipuka tena... sijui kwa kikao kipi cha Chama it is reall a shame...

Sasa anaenda kuuza ati CCM haina nia kwa mabalozi... wakati yeye akitembea kwenye Boing 777-200R; Membe anawaita mabalozi kwa muda mfupi anaongea na dunia nzima...

In short CUF wamefanya utoto sana.

CCM wamesema kubadilisha mfumo wa Utawala maana yake ni kubadilisha katiba ya Zanzibar tena big time; sasa swali Katiba ya Zanzibar ibadilishwe na Maalimu Seif na Luteni Makamba, au na Baraza la kuu la CUF na NEC ya CCM tu? Je Jahazi Asilia katiba haiwahusu, Je CHADEMA katiba haiwahusu etc... je wasiokuwa wanachama wa vyama vya CUF na CCM mabadiliko ya Katiba hayawahusu?

Mzee Msekwa amesema; Historia inaonyesha huu ni Muafaka wa nne Tangu 1957; na kumetokea matatizo ya namna hii kwa ukubwa tofauti lakini yametokea kila baada ya uchaguzi... wao CCM wanachofikiri waende slow but sure lakini "Agreement/Muafaka" utakaotokea sasa uwe ndio unaleta maridhiano Zanzibar...

Kwa hiyo basi hakuna haja ya kuangalia tu sasa kwamba Lazima Maalimu Seif Alambe uwaziri kiongozi kwa Mara nyingine... People should THINK BIG; tuachane na hili tatizo moja kwa moja.
 
Wasitishe mazungumzo na CCM na wajipange vizuri kwa ajili ya 2010 naamini watashinda.

..watashinda wapi? bara au visiwani?. nshasahau,nilitakiwa kuuliza,"je,wataachwa washinde?"

..huko tusubiri mapinduzi mengine! lini sijui!ila tusubiri!yanakuja!kwani haki usipoipata mezani utaipata vitani!
 
Kasheshe inawezekana unatetea hoja hii ukiangalia ibara ya 15 ya chama cha CCM na ndo maana ya majiby yako haya
Kwa hili sio mkuu; wala hata sina hiyo katiba.

Kwa sababu, kama Viongozi wa CCM wa ngazi za juu wanakili kuwa viongozi wa CCM wa zanzibar waliweka ngumu katika hili na wao kukubali, kama waliweza kuwasikiliza na kuwakubalia iwekwe wazi kwamba mambo ya siasa ya Zanzibay waachiwe waamue wenyewe kwa sababu wanaweza kuamua kama walivyofanya kule Butiama
Hii ni hekima tu ndugu yangu!!! Kwa kuwa pilipili ya shamba yakuwashia nini? Lazima usikilize wale wanaoishi huko, wanaopatwa na Msukosuku... Lakini Ukumbuke hili "CCM na CUF Wameridhia Serikali ya Mseto" Kuara ya maoni au sijui nini ni namna gani ya ku-implement.

Na nakukumbusha kwamba Both CCM na CUF, wanaridhia Serikali ya Mseto... kinachotakiwa ni kuwashirikisha ambao hawako CCM wala CUF... kama unaona si muhimu... utakuwa una-makengeza ya akili.

Pili, je ni kwa katiba gani inasema kuwa kura ya maoni itakuwa ikitumika katika kufanya maamuzi, kwa sababu mambo mengi sana hapa Tanzania yamekuwa yaamuliwa tu bila kuangalia maslahi ya nchi, na wala kura ya maoni haifuatwi, sasa ni wapi ambapo kura ya maoni inastaili?
Ni uzembe wa kufikiri kwamba hakuna evolution kwenye maisha tunayoishi... kwenye technolojia, utamaduni na Siasa pia kuna evolution hatutafanya mambo yote kama juzi, mengine yatakuwa na mabadiliko kulingana na wakati na mazingira... Hivyo si jambo la kujadili kwamba lazima with time tusirudie makosa ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambapo watu wengine wanasema ni wa Nyerere na Karume. we don't want to go back to as far as that period.

By the way alternative ya Kura ya maoni ni kupitia Baraza la Wawakilishi, Mambo mengi ya mabadiliko makubwa yamepitishiwa huko...

Tatu, ikumbukwe kuwa CCM na CUF walishakubaliana kuwa daftari la wapiga kura la zanzibar na sheria za tume ya uchaguzi ya zanzibar zina upungufu mkubwa sana na matatizo mengi, na wakakubaliana kufanya malekebisho kabla ya 2010, sasa hapa utaratibu gani utatumika katika kupiga kura hizo wakati daftari na sheria zote ni mbovu??
Hizi ndio hoja zile zingine kati ya Tano... zilishakubalika... hakuna shida huko ndugu yangu... hakuna haja ya kujadili kitu ambacho both parties have agreed.

Na je, unaweza kueleza kuwa kwa hali ya siasa ya Zanzibar ilivyo, CCM hawataiba kura za maoni kama kawaida yao, je kitakachowafanya wasiwe wezi wa kura ya maoni ni nini, wkati ndo kawaida yao??
CCM hawana haja ya kuiba kura kwa kuwa CCM wameunga mkono serikali ya Mseto, kinachohitajika ni huo uamuzi uwe wa wananchi na wala sio CCM au CUF ... jumla watu 12

Na mwisho kabisa, sasa tunaelekea katikati ya mwaka 2008, ambapo uchaguzi mkuu utakuwa umebakiza 2.5, lakini maandalizi ya kupiga kura ya maoni sio laisi kama tunavyofikilia, wananchi wanahitaji elimu ili kujua haki katika kupiga kura ya kuamua mustakabali wao, sasa haya yote yatafanywa lini ikiwemo, kuwaelimisha wananchi, kurekebisha sheria pamoja na daftari la wapiga kura, ili muafaka ufikiwe kabla ya 2010 kutokana na ahadi za Mh.Predident?

Ni kweli lakini Zanzibar ina wananch 1M... it is possible; eneo lake ni dogo, wananchi wako wako active kwenye siasa, uhamasishaji utakuwa rahisi tofauti na Mkoa wa Manyara...


Mwisho: Nashukuru kwa ku-raise concern ambazo ni za watu wengi... lakini kwa hakika they have all been taken care.
 
Wana JF, asilimia kubwa ya Wana - CCM Zanzibar wanatokana na Wana ASP ambao ndio waliongoza mapinduzi ya mwaka 1964.
Hawa ni Wahafidhina halisi hawatakubali Mjukuu wa Sultani atawale tena au watawale naye Zanzibar.
 
Wana JF, asilimia kubwa ya Wana - CCM Zanzibar wanatokana na Wana ASP ambao ndio waliongoza mapinduzi ya mwaka 1964.
Hawa ni Wahafidhina halisi hawatakubali Mjukuu wa Sultani atawale tena au watawale naye Zanzibar.
Afana-aleik na wewe umekwishakumbwa na propaganda za CUF. Hiyo ndiyo gea inayotumiwa na CUF kujihalalaishia umaarufu. Wengi wa wana CCM -Zanzibar wanaijua ASP katika Historia tu kama vile wana CCM Bara wanavyoijua TANU katika historia. Tena basi ukiangalia Zanzibar ndiko kwenye wanachama (damu mpya) katika CCM kwani wanapewa nafasi ya kuwa wanachama na kuchukua uongozi ukilinganisha na CCM-Bara. Huo uhafidhina unatoka wapi kwa kina watu kama Mh. Dogo na wa aina yake ambao wamo mpaka katika (CCM- CC)?
 
Mimi Ningekuwa Kikwete Ningenyamaza Na Kungoja Wakati Wa Uchaguzi Ninafanya Mambo Matatu
1. Sipeleki Jeshi, Ninawacha Hawa Wazanzibar Kuamua
2. Sipeleki Mamluki Wa Kupiga Kula
3. Ninhakikisha Tume Ya Zenji Inakuwa Huru Na Haki Ili Wananchi Waosisitizwa Na Kalume Waamue.
 
Wasitishe mazungumzo na CCM na wajipange vizuri kwa ajili ya 2010 naamini watashinda.

Naweza kukubaliana na wewe kuwa kiasi fulani, lakini issue hii ni pana kuliko tunavyofikiri, kama uki-trace back utaona kuwa injustice iliyofanywa Zanzibar wakati wa mapinduzi, pamoja na juhudi zote za Nyerere kuzifunika, siasa za ushindani zilizorudi Zanzibar zimefunua tena, na chuki bado ipo, busara ya muafaka Zanzibar haikwepeki.

Ya kusema kuwa wajipange vizuri 2010 watashinda is non sense, kwa sababu mara zote tatu kwenye uchaguzi walishinda na (kwa busara nzuri tu) waliporwa ushindi, this is open secret, the story will be the same in 2010, CUF watashinda, watapigwa, watauawa wengine watakuwa wakimbizi CCM wataingia madarakani, wataanzisha mazungumzo mengine ya muafaka yatachukua muda kama huu wa sasa, halafu janja ya kisiasa itatokea then, itarudi kwenye square one, kama ilivyokuwa kwenye chaguzi tatu zilizopita.

Kama unakumbuka ni kuwa Uhuru ulitolewa kwa chama kilichoshinda kwenye uchaguzi wa vyama vingi (ZPPP) kabla ya mwingereza kubwaga Manyanga, lakini mapinduzi yaliyoongozwa na walioshindwa ASP yalichukua madaraka kimabavu na kufanya uhalifu mwingi tu, na Nyerere alijitahidi sana kuleta reconciliation na kuunda kitu kinachoitwa serikali ya umoja wa kitaifa chini ya kivuli cha chama Kimoja, lakini baadaye baada ya Nyerere kuondoka na hasa baada ya Seif kufukuzwa kwenye chama na Salmini kutawala kidikteta, ujinga ujinga na ubinafsi ulianza kuletwa na baadhi ya watu zanzibar, na upemba na uunguja ukaanza kuwa wazi zaidi na sasa ndio uko wazi kabisa. Matokeo yake watu wanamaitain hiyo status quo at any cost bila hata kujali maendeleo ya watu.

Ukiangalia katika kipindi chote hicho utaona kuwa Zanzibar na udogo wake ule hakuna maendeleo hata kidogo, kisa ni watu kuikalia politiki, kuweka maendeleo nyuma, na Pemba imekuwa kama gereza kubwa ambalo watu ndani yake wana uhuru kidogo hata wa kusafiri.

Siasa za vyama vingi zimerudisha hali ileile iliyokuwepo wakati mwingereza anaondoka, ni ajabu kuwa mpaka leo bado iko vilevile. Kwa hiyo issue ya muafaka Zanzibar haikwepeki hata kidogo, kwa demography ya sasa kila uchaguzi CUF (ZPPP) itashinda, unless watu wa CCM Zanzibar (ASP) wazaane kwa wingi sana ili wawaout number watu wa CUF.

At the same time CUF nao wanajua kuwa sio rahisi kwa wao kutawala kisiwa alone.

Hali inayotokea sasa lawama zinatakiwa ziende moja kwa moja kwenye wenyekiti wa CCM kwa pande zote mbili, kwa kuwa waoga, kuonesha udhaifu na kuweka mbele maslahi ya chama (na huenda siyo ya chama ni ya watu wachache) kuliko ya taifa, muafaka usiangaliwe kwa Seif au Duni kupewa uwaziri kiongozi tu, it is more than that, hata Kama Seif na Duni wakifa leo CUF itaendelea kuwepo na ule mpasuko utazidi kuendelea kuwepo.
 
Mimi Ningekuwa Kikwete Ningenyamaza Na Kungoja Wakati Wa Uchaguzi Ninafanya Mambo Matatu
1. Sipeleki Jeshi, Ninawacha Hawa Wazanzibar Kuamua
2. Sipeleki Mamluki Wa Kupiga Kula
3. Ninhakikisha Tume Ya Zenji Inakuwa Huru Na Haki Ili Wananchi Waosisitizwa Na Kalume Waamue.

Hasyo matatu unayosema hayatafanyika ndio hasa yatakayofanyika, just wait and see! Watu walishasema kuwa mpemba hatatawala kisiwa!
 
Hii ya Msekwa ni matatizo ya kuwaweka vizee katika CCM na kuifanya kama miungu yao midogo ,mtu huyu inaonyesha ameshapoteza akili na analolisema na kulitenda halijui ,hata ?

Unafahamu kama unakunya uharo au vitu ni vigumu lakini Msekwa hafahamu kabisa ,hivi ni kitu gani kilichomsahaulisha mtu aliependekezwa kuwa raisi wa Zanzibar kule Unguja ,maana Mh. KARUME alitokea wa mwisho na alitoka sijui na kura tatu tu,kufika DODOMA alitokea wa mwanzo na wale walioonekana wanafaa wote wakapigwa na chini ,na mpaka leo wenyewe bado wana usongo na jambo lililofanywa na DODOMA.

Halafu mnasema CCM Zanzibar ndio wamewekea mguu ,huo umekwishatambulika kuwa ni uongo hivyo Msuya ni mwongo hana tofauti na mafisadi wanaojitetea,kinachofanywa ni kuendeleza kuwawekea Wazanzibari kibaraka ili wazidi kugandamizwa na watu wa Tanganyika na karume ameshasikika akisema waliomchagua si Wazanzibari bali ni ndugu zake kutoka Tanganyika fahamu tu kuwa Karume ana asili ya Malawi kutokana na baba yake ambae ni mtu wa Malawi.

Na anavyosema kauli hiyo kuwa Wazanzibari hawakumchagua anamaanisha ule uteuzi wa kumpata mgombea waUraisi kwa tiketi ya CCM ambapo Wajumbe wa Zanzibar walimpiga na chini ,hapo fahamuni kuwa CUF haimo katika mkumbo wa wa Karume ,kama ni wafuatiliaji wa siasa basi Karume na ukoo wao wote walikuwa ni moja katika mashina ya CUF wenye kuaminika na hilo hakuna Mzanzibari anae likataa bali tatizo lipo ndani ya CCM wenyewe ili kutaka kukomoana si mnafahamu kuwa MH.Salmini Amour alipata matatizo ya kutokuona vizuri tatizo ambalo bado anaendelea nalo ,Mh.Karume na serikali yake walimuekea ngumu na kukataa kumsafirisha kwa ajili ya kupata matibabu hata gari pia ilifika hatua ya kumnyang'anya.

Mheshimiwa Kikwete anaifahamu fika kadhia hii ya tatizo la Salmini Amol komando ,kwani yeye ndie aliempigia simu daktari wake na kumwaambia aende akamjulie hali Salmini Amour ,kufika tu kwa hali aliyokuwa nanyo akamjulisha Muungwana kuwa jamaa asipowahiwa atapoteza macho ,ndipo hapo alipochukua juhudi za kumsafirisha hadi Uchina ,sasa Mh. Kikwete akilipima hilo anaweza kuona kuwa Karume hana utu wa kushughulikia wananchi zaidi ya maslahi binafsi ikiwa mmoja kati ya viongozi wa CCM ambae pia aliwahi kuwa Raisi na kigogo wa CCM aliwachwa solemba itakuwa hali ya wengine ,joto la mh. Kikwete la kuona wananchi wanaondokana na umasikini litafikiwa ikiwa ndani yake mna watu wa dizaini hizi ??

Mnapoambiwa kuwa CCM Zanzibar ni kikundi au genge la wachache basi msiwapime kwa kipimo cha upinzani na CUF bali tizameni ndani ya CCM yenyewe huko Zanzibar.
 
1. Sitapenda kujadili historia ya Zanzibar, asili ya mtanziko wa kisiasa huko; lakini mimi naomba nichangia suala la principle tu hapa- kwamba pande mbili zimekaa zimajadiliana na kukubaliana mambo Fulani Fulani; baadaye upande mmoja umeanza kwenda tofauti. It's a political problem, that needs a political solution.

2. Nimesoma neno kwa neno rasimu ya makubaliano ya CUF na CCM ambayo ilishakubaliwa na kamati zote mbili. Suala la serikali ya pamoja linapaswa kutekelezwa kabla ya mwaka 2010.

3. Nimesoma ripoti ya Kamati ya CCM iliyopeleka Butiama kwa ajili ya Kamati Kuu na baadaye halmashauri Kuu; ukweli ni kuwa hoja ya kura ya maoni haikuzuka kikaoni- iliandaliwa kabla kwa pendekezo la Karume na kukubaliwa na wanakamati. Pamoja na uzuri wa dhana ya kura za maoni, lakini nia(motive) yake hapa si nzuri! Kwa serikali ambayo haifanyagi referendum katika masuala muhimu kihistoria kama Muungano, Katiba, Mfumo wa Vyama vingi, kumuundoa Rais wa Zanzibar kama makamu wa Rais(ambalo lilikuwa ni suala katika makubaliano mama ya muungano); inatia shaka serikali kama hiyo itakapo suala la kura za maoni Zanzibar. Ni Kikwete huyu huyu ambaye alipokwenda Kenya hakutaka wakina Raila na Kibaki wafanye kura za maoni, akata wasaini makubaliano na kuyatekeleza. Wakati wa kuibwa kwa kura hakuitishwa kura za maoni, kosa moja haliwezi kuhalalisha kosa, lakini kosa moja linaweza kutoa ishara ya kosa lingine! Kwa ujumla ukiisoma ripoti hii ya Kamati ya CCM; ukisoma na Barua ya Mwisho ya Makamba; utagundua kuwa Makamu Mwenyekiti Msekwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete- hawakusema kweli wakati wakieleza mchakato wa Maazimio ya NEC ya CCM na Matokeo yake!


4. Nilikuwepo Diamond Jubilee jana na nimemsikiliza Lipumba toka mwanzo mpaka mwisho. Nilichokielewa ni kwamba CCM imekuwa ikiwatapeli CUF toka baada ya uchaguzi, ikiwafanyia unafiki wa hali ya juu- CUF nayo kwa upande wake ilikuwabali ku-give in too much; ikakubali ghilba za aina zote ikiwa na matumaini makubwa kwamba Kikwete yuko genuine! Na kwa kiasi kikubwa mambo yote haya yalifanyika kwa siri ya pande mbili; kwa mategemeo makubwa ya CUF kwamba pengine serikali ya mseto ingetokea. Kumbe CCM wakati wote ilikuwa ikiweka kadi chache mezani na nyingine nyingi zaidi kuzificha chini ya meza.Ukiangalia mtiririko wa matukio katika hii miaka mitatu kuhusu Zanzibar utagundua ama Rais Kikwete anafanya unafiki wa hali ya juu wa kisiasa, au ni kiongozi dhaifu katika CCM kama mwenyekiti anayezidiwa nguvu na makundi mengine ndani ya chama chake. Kwa vyovyote vile, hali hii ikiachwa bila panga kuitwa panga na si kisu kikubwa ni ishara mbaya kwa utangamano wetu kama taifa haswa kwa kuwa kwa sasa CCM ndicho chama tawala!

5. Tunaungana mkono na CUF katika hili, kwani kitisho cha demokrasia mahali Fulani ni kitisho cha demokrasia mahali pote. Maandamano ya jumamosi, hayapaswi kuwa maandamano ya CUF, yanapaswa kuwa maandamano ya umma! Ama hakika, uwongo una mwisho- lakini ukweli unapaswa husimama milele, na ukweli hauna itikadi. CUF wanaweza kuwa walijikwaa mahali Fulani katika mchakato huu; lakini sasa ni wakati wa kutazama mbali zaidi, kutazama picha kubwa zaidi- CCM ikiwachwa ikapita katika hili, itandelea kuacha na ufisadi mwingine ukatawala kwenye RICHMOND, BOT nk na hatimaye kuweka misingi ya ufisadi wa kudumu zaidi katika uchaguzi mkuu 2010. Hatupaswi kuacha utadamuni wa ufisadi, usanii wa kisiasa, uchezeaji wa haki, na wananchi kukaaa pembeni kama watazamaji na wanyooshaji vidole kuendelea katika taifa letu. Ni wakati mwingine wa kuandelea kuchukua hatua!

JJ

PS:
• Mwenye Hotuba ya Jana ya Lipumba atuwekee hapa tafadhali
• Mwenye rasimu ya makubaliano ya CUF na CCM iliyokubaliwa na kamati za pande mbili aiweke hapa pia tafadhali
 
Wasitishe mazungumzo na CCM na wajipange vizuri kwa ajili ya 2010 naamini watashinda.
Hivi mimi nipo ulimwengu gani jamani? Au pengine sina phD pengine ndio maana nina mgando wa ubongo! Nashindwa kuelewa!!! Eti wajipange watashinda 2010 hivi hamjui kama CUF imesha shinda mara zote tangu uchaguzi ulioshirikisha vyama vingi kule zanzibar uanze?mnataka washinde vipi ndio wapewe?

Au mmesahau kuwa CCM wao walipindua "MAPINDUZI DAIMA" CUF wanashinda CCM wanaendeleza "MAPINDUZI" na "haiwezekani eti CCM waipate nchi kwa kumwaga damu wao waje waitoe kwa karatasi" na itakuwa ngumu zaidi maana CCM kule zanzibar wanasema wao huwa hawapigi kura ila "WANACHUKUA WANAWEKA WAAAAA".

Na kuhusu Seif mimi natofautiana sana na wanaosema kuwa Seif ni mtu wa kukurupuka na mpenda maslahi yake binafsi Maalim Seif Shariff Hamad he is a man of vision and mission. Mtu alietulia na asiependa ulwa ndio maana hata mke wake anaitwa mama awena haitwa mama seif! na kama maslahi alishayapata angekuwa msaliti asinge ingia tena kweny mazungumzo na CCM si anapewa ulinzi na masurufu yake kama Waziri Kiongozi Mstaafu?

Sasa anataka aongeze nini tena? Angekuwa huu muafaka utamfanya awe rais pengine ndio tunaweza kusema kuwa anatamaa uchu wa madaraka kama waliokuwa nao viongozi wa CCM.

Humu JF kumejaa wapotoshaji wa mada wengi ni mashushu wametumwa kuja kupunguza makali ya darasa zinazotolewa humu. Nasema na Mshindwe na Mlegee! Tanzania ya sasa sio ile mnaoijua nyie. Nyie mashushu mliotumwa kwa hisani zenu, chondechinde Msiwadanganye viongozi wenu kuwa CCM na serikali yake inapendwa sana wapeni ukweli ili wajirekebishe laa sivyo wao wakimwaga unga na nyie hamtakula!!!! "NI MTAZAMO TU"
 
Na mwisho kabisa, sasa tunaelekea katikati ya mwaka 2008, ambapo uchaguzi mkuu utakuwa umebakiza 2.5, lakini maandalizi ya kupiga kura ya maoni sio laisi kama tunavyofikilia, wananchi wanahitaji elimu ili kujua haki katika kupiga kura ya kuamua mustakabali wao, sasa haya yote yatafanywa lini ikiwemo, kuwaelimisha wananchi, kurekebisha sheria pamoja na daftari la wapiga kura, ili muafaka ufikiwe kabla ya 2010 kutokana na ahadi za Mh.Predident?
BabaH, naamini wananchi wa Zanzibar kwa hili hawahitaji kuelimishwa wanajua nani wa kumchagua. Wanaohitaji kuelimishwa ni viongozi kukubali matokeo ya kura ya maoni. Hili ndilo gumu zaidi. Sasa hivi tunaona wenzetu wa Zimbabwe viongozi wa chama tawala wanavyopata ugumu wa kukubali matokeo. Ugumu huu unaongezwa pia kutokana na washiriki kamati ya muafaka kutoka CCM, wengi hawatoki Zanzibar na hawamo kwenye mtandao wa uongozi uliopo Zanzibar. Maamuzi ya CCM bara hayawezi kutekelezeka Zanzibar bila CCM Zanzibar kushirikishwa!!!
 
..... it is more than that, hata Kama Seif na Duni wakifa leo CUF itaendelea kuwepo na ule mpasuko utazidi kuendelea kuwepo.

Mheshimiwa Bongolander inaonekana kidogo unayaelewa mambo ya Zanzibar. Lakini ah. umeangukia kule kule katika propaganda za CUF (Seif na watu wake). Mimi nafikiri unajua nini chanzo cha mgogoro-kuanzia pale Seif alipofukuzwa CCM na Uwaziri Kiongozi kwa kumu-undermine boss wake "Rais Idriss Abdulwakil", Seif alipohamaki na kuapa kulipiza kisasi dhidi ya walio madarakani CCM, alipopandikiza chuki na fitina kwa kutumia dhana ya Upemba na Unguja, ujio wa vyama vingi na kuundwa kwa CUF, ugomvi wake na kina Mapalala. Kuibuka kwa kina Lipumba, kushamiri kwa CUF (chini ya bango la kibaguzi la kuwa ni Chama cha Wapemba), mkakati wa Seif kuiuza CUF kwa Wazanzibari (wahafidhina wenye asili ya Kiarabu waliokimbilia nje baada ya Mapinduzi) Uchaguzi wa l995 na vitimbi vyake, kutotekelezwa kwa muafaka No. 1 na 2 na yote yanayojiri hivi sasa. Ulivyoeleza ni utashi na ushabiki wako ni sawa unahaki yakubakia nao mwenyewe. Lakini nakubaliana na wewe kwa hayo niliyo quote hapo juu. na hivyo ndiyo maana CCM inachukua juhudi hivi sasa tuhakikishe kuwa muafaka huu sio wa kina Seif na Duni na utashi wao au Kina Karume na Shamhuna na utashi wao, bali ni wa kweli utakaohusisha Wapemba na Waunguja wote na kujali maslahi yao na mustakbala wao. Sio watu (binafsi) wawe wowote wale, kutoka popote pale CUF au CCM.
 
Hivi mimi nipo ulimwengu gani jamani? Au pengine sina phD pengine ndio maana nina mgando wa ubongo! Nashindwa kuelewa!!! Eti wajipange watashinda 2010 hivi hamjui kama CUF imesha shinda mara zote tangu uchaguzi ulioshirikisha vyama vingi kule zanzibar uanze?mnataka washinde vipi ndio wapewe?

Au mmesahau kuwa CCM wao walipindua "MAPINDUZI DAIMA" CUF wanashinda CCM wanaendeleza "MAPINDUZI" na "haiwezekani eti CCM waipate nchi kwa kumwaga damu wao waje waitoe kwa karatasi" na itakuwa ngumu zaidi maana CCM kule zanzibar wanasema wao huwa hawapigi kura ila "WANACHUKUA WANAWEKA WAAAAA".

Na kuhusu Seif mimi natofautiana sana na wanaosema kuwa Seif ni mtu wa kukurupuka na mpenda maslahi yake binafsi Maalim Seif Shariff Hamad he is a man of vision and mission. Mtu alietulia na asiependa ulwa ndio maana hata mke wake anaitwa mama awena haitwa mama seif! na kama maslahi alishayapata angekuwa msaliti asinge ingia tena kweny mazungumzo na CCM si anapewa ulinzi na masurufu yake kama Waziri Kiongozi Mstaafu?

Sasa anataka aongeze nini tena? Angekuwa huu muafaka utamfanya awe rais pengine ndio tunaweza kusema kuwa anatamaa uchu wa madaraka kama waliokuwa nao viongozi wa CCM.

Humu JF kumejaa wapotoshaji wa mada wengi ni mashushu wametumwa kuja kupunguza makali ya darasa zinazotolewa humu. Nasema na Mshindwe na Mlegee! Tanzania ya sasa sio ile mnaoijua nyie. Nyie mashushu mliotumwa kwa hisani zenu, chondechinde Msiwadanganye viongozi wenu kuwa CCM na serikali yake inapendwa sana wapeni ukweli ili wajirekebishe laa sivyo wao wakimwaga unga na nyie hamtakula!!!! "NI MTAZAMO TU"


Seif anapewa hayo masurufu kwa kutekeleza hayo matakwa ya kisiasa na kutafuta muafaka. Kisheria si haki yake kwani amefukuzwa Uwaziri Kiongozi, hakustaafu au kumaliza kipindi chake. Katika hili la marupurupu na mafao Seif ni kama Lowassa, Jee naye unaweza kumpa hayo?
 
Back
Top Bottom