Msanii wa filamu, Steve Nyerere atia nia ya kugombea ubunge Kinondoni

kirerenya

JF-Expert Member
Aug 27, 2013
1,696
2,252
Msanii wa filamu, Steve Nyerere ameweka wazi mpango wake wa kugombea nafasi ya Ubunge katika jimbo la Kinondani baada ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Mhe. Maulid Mtulia kupitia tiketi ya CUF na kukihama chama hicho na kuamua kuhamia CCM hivyo na kupoteza sifa ya kuwa mbunge.

Anadai nafasi hiyo sasa ipo kwajili yake na kwamba aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo Maulid Mtulia alimuogopa yeye Steve Nyerere ndo maana akajiuzulu na kuhamia CCM.

Nyerere anaahidi kuwatendea haki wananchi wa Kinondoni na kwamba Kinondoni ni kama Texas kwani marais wote wanatokea jimbo hili na Kinondoni pia inahitaji kijana kutokana na sehemu nyingi na taasisi nyingine muhimu kuwa Kinondoni.

 
Atachuana na Mtulia? Aelewe kuwa Mtulia aliachia hilo jimbo kupitia CUF kwa makubaliano maalum na CCM hivyo ni bora akatafuta kitu kingine cha kufanya.
ni vyema kuhisi kama ulivyohisi kuwa Membe ni mmoja wa wajumbe wa kamati kuu ya CC ya CCM...ni haki yako kuhisi.
 
Steve mvunaji. Anajua hawezi kupita. Anaongeza tu vurugu ili mwenye pesa zake amnunue kumwachia.
Ndiyo biashara yake kubwa
 
Mweupe sana uyo...tungekua na mgombea binafsi ningemgaragaza hadi basi...
 
Msanii wa filamu, Steve Nyerere ameweka wazi mpango wake wa kugombea nafasi ya Ubunge katika jimbo la Kinondani baada ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Mhe. Maulid Mtulia kupitia tiketi ya CUF na kukihama chama hicho na kuamua kuhamia CCM hivyo na kupoteza sifa ya kuwa mbunge.

Anadai nafasi hiyo sasa ipo kwajili yake na kwamba aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo Maulid Mtulia alimuogopa yeye Steve Nyerere ndo maana akajiuzulu na kuhamia CCM.

Nyerere anaahidi kuwatendea haki wananchi wa Kinondoni na kwamba Kinondoni ni kama Texas kwani marais wote wanatokea jimbo hili na Kinondoni pia inahitaji kijana kutokana na sehemu nyingi na taasisi nyingine muhimu kuwa Kinondoni.


Namuunga mkono Steve, kwa sababu kwa sasa ubunge siyo hadhi tena.

Ni bora wampe huyu muhangaikaji mwenzetu apate mtaji.

Akichukuwa fomu ccm nitapambana kuhakikisha anashindana kutowa rushwa ndani ya ccm na anashinda kura za maoni.

Akishashinda upande wa ccm huku nje kwepesi Polisi ndio wanaamuwa mshindi.
 
kwa siasa zilizonyeshwa wakati wa uchaguz mdogo ccm mtatifuana sana mkijua mnaweza kutangazwa hata mkishindwa
 
Atachuana na Mtulia? Aelewe kuwa Mtulia aliachia hilo jimbo kupitia CUF kwa makubaliano maalum na CCM hivyo ni bora akatafuta kitu kingine cha kufanya.
Walishampoteza huyu, time ni muamuzi mzuri!!!
 
Tanzania nakuonea huruma. Tunafika tunaanza kutawaliwa na watu wa ajabu ajabu. I pray for the end of this non sense. Akili ndogo kutawala akili kubwa.
 
Back
Top Bottom