Msanii Mbalamwezi kutoka kundi la 'The Mafik' afariki dunia ikidaiwa ni kutokana na majeraha ya kupigwa

instanbul

JF-Expert Member
Jun 26, 2016
11,381
14,186
Mmoja wa wasanii wanaounda Kundi la The Mafik, ajulikanaye kama Mbalamwezi amefariki dunia usiku wa kuamkia leo. Msanii mwenzake wanaounda kundi hilo Hamadai amethibitisha.

2.jpg

Caption: Msanii Marehemu Mbalamwezi

Chanzo cha kifo chake bado hakijajulikana ingawa inasemekeana kutokana na majeraha ambayo yanahisiwa kuwa amepigwa. Hata hivyo, uchunguzi zaidi unaendelea kuhusu kifo chake

Aidha, Mjomba wa Marehemu aliyejulikana kwa jina moja tu la Mzee Chifu amesema kifo cha Mbalamwezi kina utata. Amesema marafiki zake waliopeleka taarifa ya kifo walieleza kuwa walikuta mwili wa Mbalamwezi umetelekezwa ukiwa hauna nguo

Mwili wa Mbalamwezi umehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

1.jpg

Caption: Kundi la Muziki la The Mafik. Marehemu katikati
 
Saturday , 15th Dec , 2018

Msanii wa kundi la The Mafik anayejulikana kwa jina la Mbalamwezi, amekamatwa na jeshi la Polisi mkoa wa Kinondoni kwa tuhuma za wizi.


Tukio hilo limetokea hapo jana baada ya msanii huyo kumuibia dereva wa gari ya moja ya kampuni zinazotoa huduma za usafiri binafsi jijini Dar es salaam (Taxify), aliyejulikana kwa jina la Calvin.

Akisimulia tukio hilo Calvin amesema Mbalamwezi aliitisha usafiri akitumia simu ya mwenzake, lakini alipokuwa njiani alionekana kuwapigia simu watu kuomba hela kwani hakuwa na pesa ya kumlipa dereva, na ndipo alipochukua uamuzi wa kumuibia dereva baada ya kumfanya apoteze fahamu.

Meneja wa kundi la The Mafik aliyejitambulisha kwa jina la Kapasta amesema ni kweli kuna hilo tukio, lakini ndio yuko njiani akielekea kituo cha Polisi Oysterbay ambako msanii huyo amewekwa rumande ili ajue kinachoendelea.

East Africa Television ilifanya jitihada za kumtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni Jumanne Muliro, lakini alijibu hawezi kuzungumza kwa wakati huo kwani alikuwa kwenye ziara ya Waziri Mkuu.




 
Saturday , 15th Dec , 2018

Msanii wa kundi la The Mafik anayejulikana kwa jina la Mbalamwezi, amekamatwa na jeshi la Polisi mkoa wa Kinondoni kwa tuhuma za wizi.


Tukio hilo limetokea hapo jana baada ya msanii huyo kumuibia dereva wa gari ya moja ya kampuni zinazotoa huduma za usafiri binafsi jijini Dar es salaam (Taxify), aliyejulikana kwa jina la Calvin.

Akisimulia tukio hilo Calvin amesema Mbalamwezi aliitisha usafiri akitumia simu ya mwenzake, lakini alipokuwa njiani alionekana kuwapigia simu watu kuomba hela kwani hakuwa na pesa ya kumlipa dereva, na ndipo alipochukua uamuzi wa kumuibia dereva baada ya kumfanya apoteze fahamu.

Meneja wa kundi la The Mafik aliyejitambulisha kwa jina la Kapasta amesema ni kweli kuna hilo tukio, lakini ndio yuko njiani akielekea kituo cha Polisi Oysterbay ambako msanii huyo amewekwa rumande ili ajue kinachoendelea.

East Africa Television ilifanya jitihada za kumtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni Jumanne Muliro, lakini alijibu hawezi kuzungumza kwa wakati huo kwani alikuwa kwenye ziara ya Waziri Mkuu.




This means polisi ndo wamemuua
 
wanasema katika dunia ya sasa ya teknolojia ya digitali, information is power.

ila jf siku hizi tunapitwa sana na habari. inawezekana member wengi umri wetu umeenda, hatuwezi tena kukimbizana na kasi ya vijana wa instagram na twitter ktk kutafuta habari.

kule instagram na twitter habari za kifo cha huyu msanii zimeanza kusambaa masaa sita yaliyopita. hapa jf habari hii imeanza kuwa reported masaa mawili yaliyopita.
RIP mbalamwezi.
 
wanasema katika dunia ya sasa ya teknolojia ya digitalal, information is power.

ila jf siku hizi tunapitwa sana na habari. inawezekana member wengi umri wetu umeenda, hatuwezi tena kukimbizana na kasi ya vijana wa instagram na twitter ktk kutafuta habari.

kule instagram na twitter habari za kifo cha huyu msanii zimeanza kusambaa masaa sita yaliyopita. hapa jf habari hii imeanza kuwa reported masaa mawili yaliyopita.
RIP mbalamwezi.
Skuizi jf inalala sana, hata Facebook kule Kweny page yao,habari wanapost masaa 6 hadi 8 mbele wakati wenzao ITV,Azam wanapost habar mapema sana tu zikitokea
 
Back
Top Bottom