Msanii gani maarufu umewahi kuonana naye live mkaongea mawili matatu

Mboso ..tangu hajawa star Hadi sasa tukikutana maeneo ya kwao akija kutembea na Mimi nikiwa maeneo hayo salamu za hapa na pale..yupo poa Sana

Godzila (r.i.p)..enzi hizo naishi mbezibeach tulikuwa tunakutana mida ya jioni pale belinda kwa story za hapa na pale na marafiki zangu

Dullyskyes..kwa mara ya Kwanza tulikutana yahya boutique kino..mazoea yakaanzia hapo jamaa yupo straight hapindishi ukizingua

Nitarudi
 
Dully sykes zamani sana alikuwa mshikaji nadhani ilikuwa around 2002 au 2003 wakati huo anatembea na "ATU" ,cha kusikitisha ATU alifariki kwa "NGOMA".

Father Nelly alikuwa msela wangu sana enzi hizo wakati nakaa "NGALIMI".
lile jina lake mzee wa mikasi alijipa tu kama brand au ndio maisha yake alikula sana ujana
 
Nakumbuka kwangu enzi nipo Arusha miaka ya 2016 , Nlikuwa na kawaida ya kwenda club D maeneo ya Moshono.

Siku ya siku wakaja kina Mr Blue na Rommy Jons ambae alipewa u DJ.

Cha ajabu hatukuwa wengi sana, hatukufika hata 30,

Basi ikawa Mr Blue ananipa mic sana tu niwe nafuatiliza nyimbo zake maana nlikuwa nmezikariri nyingi.

Ilikuwa poa sana ile siku kwangu, Jamaa yupo peace hana makuu
Juzi juzi kagonga mtu kea gari kule Alimaua karibu na shule ya mama Salma Kikwete, akakimbia
 
King Dodoo la bouche tulikaa nyumba moja kinondoni msufini...nikaudhuria na harusi yake na bi Salma........lina sanga tulikaa naye meza moja double H Dodoma karibu na maisha club...... Angela chibalonza r.i.p kwenye shoo yake kilimani club....Saida karori kipindi anavuma na chambua kama karanga jamhuri stadium.....WANASOKA NDIO USISEME.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom