Msamiati mpya wa SUKUMA GANG haufai, unaweza kuleta matatizo kwenye jamii hapo baadaye. Mamlaka ziliangalie hili

The lost

JF-Expert Member
Jul 3, 2017
2,695
8,209
Nipo natafakari namna nchi hii imekuwa, hakuna jambo baya kama kumtambua mtu na kumponda kwa kutumia kiashiria cha kabila lake.

Hivi karibuni kumezuka tabia ya watumiaji wa mitandao hasa katika maswala ya kisiasa kutumia neno SUKUMA GANG kama utambulisho wa watu fulani waliokuwa wanafanya kazi kwa karibu na aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania hayati John Pombe Magufuli.

Binafsi neno hili naona linaweza leta matatizo ya kijamii kama ambavyo maneno Intarahamwe, facism, na mengine ya namna hiyo yalivyopelekea matatizo kwenye jamii

Hivyo kutokana na neno hili kuwa na mlengo wa kibaguzi na chuki ni heri mamlaka kupiga marufuku matumizi ya neno hili pia niwaombe wahusika wanaotumia neno hili kuacha mara moja.
 
Kuna kipindi ilikua kawaida kukuta utani wa wasukuma mitandaoni mpaka Rais akatishia watu kufungwa.

Kuna mwaka ikawa ukimsema mtu kisa kavaa yeboyebo unapelekwa polisi.

Hii nchi ina historia nyingi za komedi.

Kuna kipindi ilisemwa ikatokea umemsema mtu aliyevaa nguo ya ccm jiandae kushughulikiwa.
 
TUWAOMBE MSAMAHA watanzania maana ukabila tumeulea sisi wasukuma sasa kuitwa SUKUMA GANG imekuwa nongwa.

Hebu anzia pale mkuu wa nchi mpaka naibu waziri ni akina nani?

Mlipaji mkuu hazina mpaka AG ni nani?

TISS security ni akina nani?

Tume na mashirika wakurugenzi ni akina nani?
 
Kwahio na serikali iingilie kati huu upuuzi kati ya wapuuzi wa kubaguana ?, Tumeshatoka huko ambapo serikali / kiongozi iliona / waliona sifa kupeleka maendeleo kwao sababu watazikwa huko na pia kuwashangaa watu iweje wachague mtu ambae sio wa kwao...

Kazi aliyofanya Mwalimu kwa karne za kutosha imeharibiwa kwa miaka michache
 
Nipo natafakari namna nchi hii imekuwa, hakuna jambo baya kama kumtambua mtu na kumponda kwa kutumia kiashiria cha kabila lake. Hivi karibuni kumezuka tabia ya watumiaji wa mitandao hasa katika maswala ya kisiasa kutumia neno SUKUMA GANG kama utambulisho wa watu fulani waliokuwa wanafanya kazi kwa karibu na aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania hayati John Pombe Magufuli...
Mifano uliyotoa haiendani na sukuma gang. Intarahamwe ni neno lenye maana sawa na watu wa kuja (wasio wenyeji). Neno hili linatumika kuwataja wanyarwanda waliopo Congo DRC, fascism ni mfumo wa kutawala kimabavu. Sukuma gang linatumika katika kueleza kundi wa wasukuma lililokuwa limemzunguka mwendazake na likiwa na mamlaka ya kujipangia chochote.

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
 
TUWAOMBE MSAMAHA watanzania maana ukabila tumeulea sisi wasukuma sasa kuitwa SUKUMA GANG imekuwa nongwa.
Hebu anzia pale mkuu wa nxhi mpaka naibu waziri ni akina nani?
Weka orodha ya mawziri, na viongozi wengine wa jiwe na kanda wanazotoka tuone wasukuma ni wangapi
 
Mifano uliyotoa haiendani na sukuma gang. Intarahamwe ni neno lenye maana sawa na watu wa kuja (wasio wenyeji). Neno hili linatumika kuwataja wanyarwanda waliopo Congo DRC, fascism ni mfumo wa kutawala kimabavu. Sukuma gang linatumika katika kueleza kundi wa wasukuma lililokuwa limemzunguka mwendazake na likiwa na mamlaka ya kujipangia chochote.

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
Umemalizia vizuri lakini umeanza vibaya. "Interahamwe" kilikuwa kikundi cha kijeshi cha Wahutu nchini Rwanda kilichokuwa na lengo la kuua na kumaliza Watusi na wenye mlengo kama wao. Neno lenyewe linamaanisha "Piga pamoja". Umechanganya na " Banyamulenge" ambao ndo Wanyarwanda walioko milima ya Mulenge nchini Kongo.
 
Mifano uliyotoa haiendani na sukuma gang. Intarahamwe ni neno lenye maana sawa na watu wa kuja (wasio wenyeji). Neno hili linatumika kuwataja wanyarwanda waliopo Congo DRC, fascism ni mfumo wa kutawala kimabavu. Sukuma gang linatumika katika kueleza kundi wa wasukuma lililokuwa limemzunguka mwendazake na likiwa na mamlaka ya kujipangia chochote.

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
Nipe majina ya watu waliomo humu na influence yao katika maamuzi ya nchi
 
Back
Top Bottom