Msameheni bure Job Ndugai, amechanganyikiwa baada ya kuomba msamaha batilifu uliokataliwa! Barua yake ya Kujiuzulu nayo pia ni batilifu!

Wanabodi,

Naomba kuanza kwa declaration of Interest
Kwa vile mimi ni mmoja wa waandishi wachache waliowahi kuitwa kuhojiwa na Kamati ya Bunge kwa maandiko yangu, ya kulituhumu Bunge kujipendekeza kwa serikali, hivyo inaweza kuonekana nafurahia kinachompata Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai!. No!. Huyu ni Mkuu wa Mhimili wa Bunge wenye jukumu la kuisimamia serikali, haitakiwa Spika kujipendekeza kwa Executive, inambidi Mkuu wa Executive amuogope na kumheshimu Mkuu wa Bunge na Mahakama, siungi mkono jinsi Job Ndugai alivyodhalilishwa vile pale juzi.

Hili ni bandiko la kupinga ubatili unaendelea katika hili sakata la Spika. Baada ya Spika wetu Job Ndugai kutoa yale matamshi ya ukweli ya kizalendo kwa taifa letu kuhusu mikopo na deni la taifa, halafu akaja kuikana kauli yake na kuomba msamaha batilifu, kwanza niliuliza, Viongozi wetu wanapofanya makosa ya wazi waishie tu kuomba msamaha kisha 'life as usual', au tujenge utamaduni wa kuwajibika kama enzi za Nyerere? kisha nikauzungumzia msamaha batilifu, Ndoa halali, ndoa batili na ndoa batilifu. Je, wajua pia kuna msamaha halali wa kweli, msamaha batili na msamaha batilifu? Msamaha ule ni batilifu! ambao ulikataliwa, na mara baada ya msamaha huo kukataliwa nikauliza tena Baada ya maneno haya ya Rais Samia, kama ni timamu, je, tumshauri to do "The needful?" au akomae nao, till they do him away?

Jana barua hii ya taarifa kwa umma toka kwa Spika kuwa ameandika barua ya kujiuzulu uspika
View attachment 2071447
imesambaa kote. Kama ni kweli hii ndio barua ya Spika Job Ndugai kuuarifu umma kuwa ameandika barua ya kujiuzulu uspika, na kuipeleka kwa Katibu Mkuu wa CCM, kiukweli this looks fake!, ila kama sio fake, then tumsamehe bure Mhe. Job Ndugai, huku kutakuwa ni kutokana na kuchanganyikiwa tuu, barua hii nayo ni barua batilifu!, kwasababu kujiuzulu kwake kumekuwa addressed to a wrong person and to a wrong Institution. Bunge ni mhimili, Mkuu wa mhimili wa Bunge hawezi kujiuzulu kwa barua batilifu na tukaacha tuu hivi hivi, what precedence tunaweka for records?.

Nashauri barua hii ikataliwe, Spika aandike a proper letter ya kujiuzulu kwenye a proper Bunge letterhead kama hii View attachment 2071452

Nakiri nimekuwa inspired kupandisha bandiko hili baada ya kumsoma mwana je huyu

Mkuu Yohane Mbatizaji, johnthebaptist
it's true Job kachemsha!, barua ya kujiuzulu uspika ilipaswa kupelekwa kwa katibu wa Bunge, CCM ndio wanapewa copy. Spika wa Bunge ni Spika wa Bunge la JMT na sio Spika wa Bunge la CCM. Usika wake ni kwa mujibu wa katiba, na kujiuzulu pia kumeelekezwa na katiba anaandika barua kwa nani, na sio kwa CCM!.

CCM ilimpendekeza tuu, baada ya kuchaguliwa, anakuwa ni Spika wa Bunge la JMT na sio Spika wa CCM!, hivyo hata kujiuzulu, anajiuzulu kwa kumuandikia Katibu wa Bunge na sio Katibu wa CCM!. Kama Spika wa Bunge anayepaswa kuijua katiba na kuifuata, anaweza kujiuzulu kwa barua ya kienyeji namna hii, then this is a disgrace kwa nafasi ya Spika!.

Huu sio utaratibu wa kufuata wakati wa kujiuzulu kwa Spika wa Bunge. Ingekuwa anajiuzulu kwa kujivua uanachama wa CCM hivyo kupoteza uSpika hapo ndipo anapeleka barua ya kujiuzulu kwenye chama chake, hata angekuwa amejiuzulu ubunge, barua ya kujiuzulu inakuwa addressed kwa Spika wa Bunge. Japo chama ndicho kimemdhamini kugombea ubunge, na uspika lakini baada ya kuchaguliwa mbunge au Spika, umechaguliwa na Watanzania/Bunge la JMT, unawajibika kwa Bunge na sio kwa chama chako.

Kikatiba, Spika wa Bunge akijiuzulu anatakiwa kufanya kutumia Ibara ya 149(1)(c) ya Katiba ya JMT inayosema iwapo Spika wa Bunge atajiuzulu, basi taarifa ya kujiuzulu aliyoiandika na kuitia sahihi yake ataiwasilisha kwenye Bunge.

Inakuwaje anaipeleka kwenye chama na Bunge lipokee nakala kutoka kwenye chama? . Msameheni bure tuu, Spika atakuwa amechanganyikiwa, maada kwa jinsi alivyokuwa anauringia na kuutambia, "mimi ni mhimili" halafu ghafla unatakiwa kuutema uspika, hata ningekuwa mimi, lazima mtu uchanganyikiwe!

Naendelea kusisitiza Shurti la kudhaminiwa na chama kugombea uchaguzi, ni shurti batili kwa mujibu wa Katiba, linatutia hasara, tulifute!.

Bunge ni mhimili, Spika anapatikana kwa mujibu wa katiba, na akijiuzulu pia anajiuzulu kwa mujibu wa katiba, hawezi kujiuzulu tuu hivi kienyeji enyeji kwa ubatili na kukubaliwa, hata kama ni kujiuzulu, then ajiuzulu kwa mujibu wa katiba, kama kifungu hiki kilivyoeleza

Mkuu Ukwaju thanks kwa kifungu hicho.

Hii tabia ya kuacha na kupuuzia mambo madogo madogo haya ya ubatili, it is now unbecoming, kuna siku tutajikuta tunatengeneza taifa la ubatili. Kama Katiba ndio sheria mama, na imeelekeza jinsi ya kufanyika kwa jambo fulani, there is no options and no negotiations katiba ifuatwe ajiuzulu properly kwa mujibu wa katiba na kujulia mafao yake manene ya 80% ya mshahara na marupurupu ya Spika.

Nakutakia Kustaafu Kwema, ndugu yangu na rafiki yangu, Job Ndugai.
Paskali
[https://res]

Baada ya kuibuka kwa mitazamo tofauti baada ya aliyekuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai kujiuzulu, tumemtafuta aliyekuwa Spika wa Bunge kuanzia 1994 hadi 2005 Pius Msekwa kwaajili ya ufafanuzi.

Msekwa ameeleza kuwa taratibu zote zimefuatwa na hakuna kilichoharibika kwa mujibu wa katiba ya Tanzania.

''Spika amechaguliwa na bunge, kwahiyo utaratibu sahihi barua ya Spika kujiuzulu ni lazima ipelekwe kwenye bunge na isomwe ndani ya bunge'' Spika Mstaafu Pius Msekwa ametoa ufafanuzi.

Zaidi msikilize hapa
 
Umeongea vyema mkuu, nchi inachezewa chezewa sana hii
Tuzidishe juhudi na kupaza sauti sisi sote kwa pamoja,adui yetu anaogopa UMOJA na ndiyo sababu anafanya figisu ili tusiwe na kauli moja.
Tudai Katiba itakayoshirikisha mahitaji ya Jamii pana ya wananchi wa Tanzania ya Tanganyika na Zanzibar.
 
CCM ndio Baba hapa kwetu, hivyo Ndugai inabidi aandike kwa Katibu Mkuu CCM tu, hana jinsi..

CCM ndio kila kitu, utake usitake, CCM yangu is a very powerful machine, ukileta maneno ya kijinga jinga, sijui nchi itapigwa mnada, CCM inakupiga mnada ww mwenyewe, ukome.. Ndugai kapigwa mnada si uona sasa!! 😂😂😂😂😂😂😂😂😂

CCM safii kabisa.
 
Mwenyekiti wa Taifa wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia ametinga Mahakama Kuu ya Tanzania na ameshafungua kesi ya kikatiba kuhusu kujiuzulu kwa Spika Job Yustino Ndugai. Kwa taarifa nilizonazo binafsi, tayari kesi husika imeshasajiliwa na imepangiwa jopo la Majaji watatu la kuisikiliza kesi hiyo. Wakati kesi hiyo ikiwepo mahakamani, tayari CCM na ADC wameshawapitisha wagombea wao wa nafasi ya Spika wa Bunge.

Nimekuwa nikifuatilia maoni ya watanzania na wasio watanzania kwenye mitandao ya kijamii, mitaani, runingani na redioni kuhusu kesi iliyofunguliwa na Mbatia. Wengine wanamuona Mbatia akitaka Ndugai abaki kuwa Spika wa Bunge kwa njia ya Mahakama. Wapo wanaomuona Mbatia kama anayepoteza muda na 'fedha' zake kwa jambo lisilo na maana na kuwa jambo hilo limeshapitwa na wakati. Wapo wanaompongeza. Lakini, wengi wanambeza.

Suala la utetezi wa Katiba ni suala kubwa na la muhimu kwa kila mmoja wetu. Kila Mtanzania, kwakuwa Katiba ni sheria yetu mama, anapaswa kuilinda na kuitetea katiba yetu. Katiba inapotoa masharti ya kufuatwa, lazima yafuatwe. Katiba imetoa masharti ya kufuatwa na Spika anayetaka kujiuzulu. Ni lazima yafuatwe. Mbatia ameona hayakufuatwa. Amekwenda mahakamani kuitetea na kuilinda Katiba yetu iliyotoa masharti ambayo ameona yamekiukwa. Ni haki yake na anafanya jambo jema.

Viongozi wetu, wanapoapishwa, huapa kuilinda na kuitetea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Sheria zote nyinginezo (zinazotungwa na Bunge na zile Ndogondogo) hazipaswi kukinzana na Katiba. Pale zinapokuwa kimya, Katiba hutumika. Haipendezi kushabikia viongozi ambao hawaifuati Katiba yetu kwa minajili ya kuilinda na kuitetea kama walivyoapa. Tena, viongozi wenyewe ni wale wanaotokea kwenye Bunge ambalo ndilo linalotunga sheria.

Si sawa Athumani, aliyedhaminiwa na Musa kupata kazi kwa Ally, kuandika barua yake ya kuacha kazi akiielekeza kwa Musa huku akitoa nakala tu kwa Ally-mwajiri wake. Hapo, aliyepaswa kuandikiwa barua husika ni mwajiri ambaye ni Ally na nakala inaweza kuelekezwa kwa Musa ikimpendeza Athumani. Kimsingi, Mbatia ana haki na hoja za kufungua shauri lake Mahakama Kuu ya Tanzania kupata tafsiri ya kikatiba juu ya suala hilo. Atabezwa lakini atabaki na hoja yake.
Mkuu Learned Brother Petro mselewa, naunga mkono hoja kwa asilimia 100%, kilichofanyika ni kuhalalisha haramu na ubatili !.
P
 
Wanabodi,

Naomba kuanza kwa declaration of Interest

Kwa vile mimi ni mmoja wa waandishi wachache waliowahi kuitwa kuhojiwa na Kamati ya Bunge kwa maandiko yangu, ya kulituhumu Bunge kujipendekeza kwa serikali, hivyo inaweza kuonekana nafurahia kinachompata Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai!. No!. Huyu ni Mkuu wa Mhimili wa Bunge wenye jukumu la kuisimamia serikali, haitakiwa Spika kujipendekeza kwa Executive, inambidi Mkuu wa Executive amuogope na kumheshimu Mkuu wa Bunge na Mahakama, siungi mkono jinsi Job Ndugai alivyodhalilishwa vile pale juzi.

Hili ni bandiko la kupinga ubatili unaendelea katika hili sakata la Spika. Baada ya Spika wetu Job Ndugai kutoa yale matamshi ya ukweli ya kizalendo kwa taifa letu kuhusu mikopo na deni la taifa, halafu akaja kuikana kauli yake na kuomba msamaha batilifu, kwanza niliuliza, Viongozi wetu wanapofanya makosa ya wazi waishie tu kuomba msamaha kisha 'life as usual', au tujenge utamaduni wa kuwajibika kama enzi za Nyerere? kisha nikauzungumzia msamaha batilifu, Ndoa halali, ndoa batili na ndoa batilifu. Je, wajua pia kuna msamaha halali wa kweli, msamaha batili na msamaha batilifu? Msamaha ule ni batilifu! ambao ulikataliwa, na mara baada ya msamaha huo kukataliwa nikauliza tena Baada ya maneno haya ya Rais Samia, kama ni timamu, je, tumshauri to do "The needful?" au akomae nao, till they do him away?

Jana barua hii ya taarifa kwa umma toka kwa Spika kuwa ameandika barua ya kujiuzulu uspika

View attachment 2071447
Nashauri barua hii ikataliwe, Spika aandike a proper letter ya kujiuzulu kwenye a proper Bunge letterhead kama hii

Kikatiba, Spika wa Bunge akijiuzulu anatakiwa kufanya kutumia Ibara ya 149(1)(c) ya Katiba ya JMT inayosema iwapo Spika wa Bunge atajiuzulu, basi taarifa ya kujiuzulu aliyoiandika na kuitia sahihi yake ataiwasilisha kwenye Bunge.

Inakuwaje anaipeleka kwenye chama na Bunge lipokee nakala kutoka kwenye chama? . Msameheni bure tuu, Spika atakuwa amechanganyikiwa, maada kwa jinsi alivyokuwa anauringia na kuutambia, "mimi ni mhimili" halafu ghafla unatakiwa kuutema uspika, hata ningekuwa mimi, lazima mtu uchanganyikiwe!

Bunge ni mhimili, Spika anapatikana kwa mujibu wa katiba, na akijiuzulu pia anajiuzulu kwa mujibu wa katiba, hawezi kujiuzulu tuu hivi kienyeji enyeji kwa ubatili na kukubaliwa, hata kama ni kujiuzulu, then ajiuzulu kwa mujibu wa katiba, kama kifungu hiki kilivyoeleza

Hii tabia ya kuacha na kupuuzia mambo madogo madogo haya ya ubatili, it is now unbecoming, kuna siku tutajikuta tunatengeneza taifa la ubatili. Kama Katiba ndio sheria mama, na imeelekeza jinsi ya kufanyika kwa jambo fulani, there is no options and no negotiations katiba ifuatwe ajiuzulu properly kwa mujibu wa katiba na kujulia mafao yake manene ya 80% ya mshahara na marupurupu ya Spika.

Nakutakia Kustaafu Kwema, ndugu yangu na rafiki yangu, Job Ndugai.
Paskali
3. Japo Spika Mhe. JYN tayari ameisha jiuzulu uspika, kujiuzulu huko, japo ni kujiuzulu batilifu, lakini kujiuzulu ni kujiuzulu na Spika amejiuzulu, lakini kwa kuheshimu katiba, lazima ubatili katika barua hizo uondolewe kwa kuandikwa barua rasmi kwa mujibu wa katiba.
4. Bunge lipokee kimya kimya barua mpya ya kujiuzulu kwa Spika iliyoandikwa kwa mujibu wa katiba, kisha Bunge ndio litoe copy kwa CCM.
Hitimisho.
Namalizia kwa lile swali la msingi la uzi huu
Je wajua, haramu Isipoharimishwa Inageuka halali?, na batili Isipobatilishwa inageuka halali!. Je, Tanzania, tuhalalishe ubatili huu wa kujiuzulu kinyume cha katiba kwa mkuu wa mhimili wetu wa Bunge? Kama katiba imeelekeza jinsi ya kufanyika kwa jambo fulani, kuna sababu gani ya msingi ya kutofuata katiba na badala yake tukumbatie ubatili?

Jumatatu Njema.
Pascal
Habari njema kwa watu wote, pendekezo No. 3 na No. 4 Katika bandiko hili, limetekelezwa kwa asilimia 100% kama lililopendekezwa.
Hivyo sasa ule ubatilifu katika barua ya Kujiuzulu kwa JYN umeondolewa kama nilivyo shauri, na kuwasilishwa barua halali,
Hivyo ile taarifa ya JYN kwa waandishi wa habari, kuwa ameandika barua kwa Katibu Mkuu CCM, sasa imebatilishwa na imefutwa kwenye website ya Bunge, barua rasmi ya kujiuzuli ni hii kwa Katibu wa Bunge, na CCM kupewa nakala.
Hongera sana Bunge letu tukufu kuubatilisha ubatili huu. Sasa kwenye hili la Spika umebaki ubatili mmoja wa Naibu Spika, Dr. Tulia Akson kujiuzulu u Naibu Spika, kabla ya kugombea Uspika.
P
 
Habari njema kwa watu wote, pendekezo No. 3 na No. 4 Katika bandiko hili, limetekelezwa kwa asilimia 100% kama lililopendekezwa.
Hivyo sasa ule ubatilifu katika barua ya Kujiuzulu kwa JYN umeondolewa kama nilivyo shauri, na kuwasilishwa barua halali,

Hivyo ile taarifa ya JYN kwa waandishi wa habari, kuwa ameandika barua kwa Katibu Mkuu CCM, sasa imebatilishwa na imefutwa kwenye website ya Bunge, barua rasmi ya kujiuzuli ni hii kwa Katibu wa Bunge, na CCM kupewa nakala.
Hongera sana Bunge letu tukufu kuubatilisha ubatili huu. Sasa kwenye hili la Spika umebaki ubatili mmoja wa Naibu Spika, Dr. Tulia Akson kujiuzulu u Naibu Spika, kabla ya kugombea Uspika.
P
Barua hii imezungumzwa tu mahakamani na wakili mkuu wa serikali, bunge halijazungumza kama limeipokea au la, na halijaeleza kuwa limepokea lini barua hiyo. Kimsingi ni kuwa haieleweki kama barua hii imepokelewa na bunge au la.
 
Barua hii imezungumzwa tu mahakamani na wakili mkuu wa serikali, bunge halijazungumza kama limeipokea au la, na halijaeleza kuwa limepokea lini barua hiyo. Kimsingi ni kuwa haieleweki kama barua hii imepokelewa na bunge au la.
Kasome mapendekezo yangu hapa
kwenye uzi huu Je, wajua haramu isipoharimishwa inageuka halali? Na batili isipobatilishwa inageuka halali. Je, tuhalalishe ubatili huu kwa mhimili wetu wa Bunge? nilisema...

3. Japo Spika Mhe. JYN tayari ameisha jiuzulu uspika, kujiuzulu huko, japo ni kujiuzulu batilifu, lakini kujiuzulu ni kujiuzulu na Spika amejiuzulu, lakini kwa kuheshimu katiba, lazima ubatili katika barua hizo uondolewe kwa kuandikwa barua rasmi kwa mujibu wa katiba.
4. Bunge lipokee kimya kimya barua mpya ya kujiuzulu kwa Spika iliyoandikwa kwa mujibu wa katiba, kisha Bunge ndio litoe copy kwa CCM.
Hitimisho.
Namalizia kwa lile swali la msingi la uzi huu
Je wajua, haramu Isipoharimishwa Inageuka halali?, na batili Isipobatilishwa inageuka halali!. Je, Tanzania, tuhalalishe ubatili huu wa kujiuzulu kinyume cha katiba kwa mkuu wa mhimili wetu wa Bunge? Kama katiba imeelekeza jinsi ya kufanyika kwa jambo fulani, kuna sababu gani ya msingi ya kutofuata katiba na badala yake tukumbatie ubatili?

Jumatatu Njema.
Pascal
Habari njema kwa watu wote, pendekezo No. 3 na No. 4 Katika bandiko hili, limetekelezwa kwa asilimia 100% kama lililopendekezwa.
Hivyo sasa ule ubatilifu katika barua ya Kujiuzulu kwa JYN umeondolewa kama nilivyo shauri, na kuwasilishwa barua halali,
Hivyo ile taarifa ya JYN kwa waandishi wa habari, kuwa ameandika barua kwa Katibu Mkuu CCM, sasa imebatilishwa na imefutwa kwenye website ya Bunge, barua rasmi ni kwa Katibu wa Bunge, na CCM kupewa nakala.
Hongera sana Bunge letu tukufu kuubatilisha ubatili huu. Sasa kwenye hili la Spika umebaki ubatili mmoja wa Naibu Spika, Dr. Tulia Akson kujiuzulu u Naibu Spika, kabla ya kugombea Uspika.
P
 
Back
Top Bottom