Msamaha wa kodi kwa watumishi wa umma kufutwa. Imekaaje?

Hamna namna nikuyaondoa magamba madarakani hima hima wafanyakazi 2015 walimu muhahakishe mnafundisha watoto athari za mkoloni mweusi ccm na kuhujumu magamba katika uchaguzi mkuu ujaa kwanu nanyi mumehujumiwa vya kutisha na serikali ya magamba
 
Ukweli ni kuwa hiyo misamaha waliokuwa wanapewa wafanyakazi wa serikali tu na si wafanyakazi wote ni wa kibaguzi na haufai. Hivi kuajiriwa na serikali ni tofauti na kuajiriwa na mashirika ya umma, makampuni ya binafsi, kwa wahindi, wazungu au waswahili?

Serikali ni mwajiri kama waajiri wengine sasa kwanini wafanyakazi wake tu wapewe misamaha ya kuingiza magari? Ni hawa hawa wafanyakazi wa serikili ambao wanafanyakazi kwa uzembe mkubwa, kupoteza muda na mara nyingi hawapo maofisini au hawatekelezi majukumu na huduma zinazotolewa kwa wananchi kwa wakati. Eti wao ndo wapewe msamaha wa kodi?

Kwa hiyo tumesoma chuo kimoja, tumepata alama sawa, nakuzidi uwezo au unanizidi uwezo binafsi wa kutafakari na kutekeleza majukumu yangu. Wewe ukaajiriwa serikalini. Mimi nikaajiriwa kampnuni binafsi. Tukitaka kuagiza magari mimi sina msamaha wa kodi wewe unao eti kwa kuwa unafanya kazi serikalini! Ujinga na upendeleo wa wazi. Wafanyakazi wote ni wafanyakazi. si walioajiriwa na serikali tu.

Huwezi kusema misamaha yote ya kodi iondolewe kwa kuwa kuna misamaha inayotumika kuruzuku na kuhamasisha maendeleo ya maswala yanayohitaji kipaumbele. Cha muhimu ni kuangalia vipaumbele vinavotumika kusamahehe kodi ni sahihi.

Kwa mfano kwa sasa tanzania ilipofika kwenye uimarishaji wa uchimbaji madini hakun tena haja kusamehe kodi kwenye vifaa vya uchimbaji madini. Uhamasishaji umeshafanyika, wawekezaji watakuja iwe kuna au hakuna misamaha ya kodi kwenye sekta ya madini.

Na sisi wajasiriamali ambao tumesoma na nyinyi kuanzia msigi mpaka chuo! Nasi twahitaji msamaha!
 
Bajeti ya kuizika ccm ndio hiyo ishasomwa. Madhara ni mengi kuliko mafanikie. Kesho bajeti ya serikali ya 2015 by zitto tuitathmini maana ndio chaguo lijalo je wataweza maana hawa wa sasa washashindwa.
 
Na sisi wajasiriamali ambao tumesoma na nyinyi kuanzia msigi mpaka chuo! Nasi twahitaji msamaha!

Haya sasa. Wigo unapanuka na haina ubishi. Na niseme kama mfanyakazi anayelipwa mshahara wa serikali anapewa msamaha wa kodi eti kwa kuwa mshahara wake ni mdogo mkulima je! Kuna wafanyakazi wa taasisi binafsi, mabenki, mashirika ya umma, wajasiriamali, wavuvi, wafugaji na wakulima; Vipi wafanyakazi wa serikali tu wapewe msamaha wa kodi?
Nani alikuambia wafanyakazi wa serikali wanalipwa kidogo kuliko wafanyakazi wa sekta binafsi? Wepi wanalipwa vizuri, wafanyakazi kwenye makampuni binafsi ya wahindi na waswahili au serikalini? Sekta binafsi Haina maana ni sekta ya madini au TBL kama ilivo kwamba si kuwa kila mfanyakazi wa serikali ni mfanyakazi wa TRA.
 
Kama ungekuwa mzalendo wa kweli ungesema misamaha yote ifutwe.
Mtoa mada alichosema ni kuhusu utaratibu wa kuondoa msamaha kwa mfanyakazi wa serikali ambaye anapata msamaha baada ya miaka 4 na si wote wanaotumia huo msamaha.

Lakini wakati huo huo wanaacha misamaha kwenye makampuni hasa ya madini ambayo yanapata msamaha kila siku.

Kumbuka pia wafanyakazi ndio wanaoongoza kwa kulipa kodi ya mapato kuliko hayo makampuni.

Ungeeleweka kama ungedai misamaha ihusishe wafanyakazi wote.

Ila wewe kushangilia eti wafanyakazi kuondolewa ahueni ya kodi ni matatizo ya ...
Mimi siungi mkono misamaha ya kodi ambayo imekaa kibaguzi au upendeleo wowote usio na msingi.
 
Wanufaika wakubwa wa misamaha ya kodi walikuwa maafisa wa TRA, mfanyakazi asiye na jamaa anayemfahamu TRA faili linapigwa danadana hadi unajikuta unalipia storage charges za bandarini. Ili upate msamaha wa kodi lazima utoe rushwa za kutosha na pia kuna walimu walikuwa wanatumiwa na wafanyabiashara.
Lakini huu mtindo wa serikali ya CCM kushindwa kusimamia sheria na kudhibiti rushwa na kuishia kuadhibu wananchi si nzuri, mfano walishindwa kudhibiti uchakachuaji wa mafuta wakaishia kuadhibu walalahoi kwa bei ya mafuta, na hapa naona mfanyakazi wa serikaali anaadhibiwa. Mimi ingawa sio mfanyakazi wa serikali lakini naunga mkono ngazi za kati na chini serikalini wangesamehewa na wale wa juu wangelipa kama sisi wengine
 
Nimeshtushwa na kitendo cha Mgimwa kufuta msamaha wa kodi....

Hivi kumpa ofa mfanyakazi kama huyu msamaha wa kuagiza kagari kake ka kwendea kazini tena msamaha huo ni baada ya miaka minne kuna tatizo gani? au ndo njia ya kuwafundisha wale rushwa ili wawe na uwezo wa kuagiza magari mapya?

Lipeni kodi kwa pamoja tuchangie maendeleo ya nchi yetu. Acheni kulialia hovyo! Unalipwa mshahara halafu bado unataka upewe 'ofa'? Rushwa is a 'cult/sort of' na mla rushwa ataendelea kula rushwa tu regardless of what ..
 
Tukibishana Kama wanywa matatapu inakuwa haitusaidii lolote. Hiyo misamaha ya kodi kwa watumishi wa serikali ilikuwa ni zuga ya Viongozi wa serikali kuendelea kutukamulia ndimu machoni sisi makabwela. Wengi wao hao watumishi wa serikali ndio wanaopanda Mabasi matatu kila asubuhi kuja kazini na jioni kurudi majumbani. Watumishi hao waliopata misamaha ya kodi....asilimia 75 hata pikipiki hawawezi kumiliki.

Wanaoimiliki SERIKALI wanatumia mbinu Kama hizi kutupiga mchanga wa macho WADANGANYIKA. Kutwa wanauziana magari ya serikali (STK) kwa bei za ajabu. Kuna jamaa namfahamu, Baba yake ni mfanyakazi wa wizara fulani alinunua VX ya mwaka 2009 kwa Tsh 7,000,000/=. Hii kama sio mchezo mchafu ni nini!!!????

Hiyo misamaha ya kodi walijiwekea wenyewe. Wameona sasa WADANGANYIKA wameanza kuhoji matumizi na maamuzi ya SIRIKALI ndio wanaamua kututengenezea sinema mpya kwa kufuta misamaha kwa watumishi wa SIRIKALI .....Huku wakiacha makampuni Kama Barrick Gold wakivuna utajiri wetu kwa asilimia 0.0000 ya kodi. It make sense.
Nawakilisha....
 
Afadhali wafute tu, msamaha wenyewe ulikuwa sh ngapi bwana? Mpaka uupate unaweza kuta umetumia gharama sawa na bila msamaha. Sanasana wakubwa ndio walikuwa wana tunyonya kupiitia misamaha hiyo. Wafute kila msamaha. Iila kwanini sijaona serikali imechukkua hatuaa gani kuwabana wafanya biashara walipe kodi ipassavyo kama watumishi wa uma?
Mbona tunaweza kununua Ndege ya Raisi tunashindwa vp kununua software ya kusimamia ulipaji kodi wa kila mtu aishiye humu nchini? Angalia makampuni ya simu yanavyo kwepa kodi?
 
Kama ungekuwa mzalendo wa kweli ungesema misamaha yote ifutwe.
Mtoa mada alichosema ni kuhusu utaratibu wa kuondoa msamaha kwa mfanyakazi wa serikali ambaye anapata msamaha baada ya miaka 4 na si wote wanaotumia huo msamaha.

Lakini wakati huo huo wanaacha misamaha kwenye makampuni hasa ya madini ambayo yanapata msamaha kila siku.

Kumbuka pia wafanyakazi ndio wanaoongoza kwa kulipa kodi ya mapato kuliko hayo makampuni.

Ungeeleweka kama ungedai misamaha ihusishe wafanyakazi wote.

Ila wewe kushangilia eti wafanyakazi kuondolewa ahueni ya kodi ni matatizo ya ...

hujajibu hoja ya msingi. Kwamba exemption ilikuwa na dosari kwa kuwa ilinufaisha tabaka moja. Kwa nini iwe watumishi wa serikali tu? Hawa waliopo kwenye private sector, mashirika ya umma na taasisi mbalimbali si watanzania? Acha waondoe mimi ilikuwa inanikera sana hii
 
Nimeshtushwa na kitendo cha Mgimwa kufuta msamaha wa kodi kwa waagiza magari kwa wote waliokuwa wananufaika nao. Naomba tuelewane ni nani hasa msamaha huu ulikuwa unamfaidisha. Kwanza lzm tuelewe kuna Gvt officers na Gvt leaders.

Gvt leaders hawa ni wala nchi ambao kwenye package zao wanapewa transport, housing na mishahara ya juu kwa level za kiserikali. Hawa ndo hasa wanufaika wa semina, safari lukuki za nje na ndani ya nchi na marupurupu kibao. Kimsingi hawa ni wachache lkn ndio hao wanaomiliki mahekalu huko mbezi beach, oysterbay, masaki nk. hawa kumiliki gari sio issue, wana gari la serikali la kisasa lenye service na dereva bure, wanamiliki magari binafsi kibao nk.

Sasa hawa Gvt officers majority, ukiacha wingi wao ni wasomi wazuri tu, wengi huko serikalini, wakilipwa chini ya laki tano, wabangaizaji. Hivi kumpa ofa mfanyakazi kama huyu msamaha wa kuagiza kagari kake ka kwendea kazini tena msamaha huo ni baada ya miaka minne kuna tatizo gani? au ndo njia ya kuwafundisha wale rushwa ili wawe na uwezo wa kuagiza magari mapya?

Wahadhiri wetu wa vyuo vyote, walimu, na maafsa wa kawaida wamenufaika na kumuona Rais Mkapa kama mtu aliyejali kuinua hadhi zao. Nina uhakika watumishi hawa kilio chao mtakisikia kama alivyokianzisha Dr. Bana, achana na itikadi zake, ila na uhakika kama serikali haitakuwa sikivu lzm iadhibiwe kwa hili. Iweje bwana mahela Barrick asiguswe niguswe mimi mla chaki?

Ngoja tuone.
Hapo hapo kulikuwa na walimu wanamagari 4 lakini wanatembelea miguu!!shule nzima inaonekana walimu wake wote wanamagari!!watumishi wa serikali walisha fanya miradi!! lakini hata mwenye pikipiki hakuna sasa hapo unaweza kuona wapi kulikuwa na sababu
 
kwa vipi tutake huo msamaha uwahusu wafanyakazi tu na si wakulima pia? Mimi nafikiri kama kuna watu wanahitaji sana usafiri hasa hivi vipick up and the likes ni wakulima. Mimi ningeiona serikali ina akili sana kama ingefuta kodi zote za kuingiza any Pick up car. Ili wakulima waweze kuyanunua kwa wingi na kuweza kusafirisha kiurahisi mazao yao.
Hii habari ya miaka mingapi gari imetumika is just a ****. Kuna magari ya mwaka 2006 kwenye mitandao lakini yameshatembea km laki mbili, na kuna magari ya mwaka 1998 yenye km 30 elfu tu. Hapo gari chakavu ni lipi? Tuache porojo zisizokuwa na maana. Otherwise waongeze kodi on the basis of km ambazo gari limetembea na si huu ujinga wa miaka.
 
It is ok kufutwa as msamaha inatolewa kwa upendeleo, I remember watu kushikia bango kwamba y wafanyakazi wa Tanesco wanapata nafuu ya kununua umeme which was an incentive to it's staff and now y the Govt. servants should feel bad about it, wote tulipe kodi. My problem is the amount, it should be lowered a bit so that many servants should afford to import cars as now they have become a necessity in our life, the Govt. can get other taxes like road licences, fuel etc which are long run rather than getting big amount at once and discouraging people to buy cars.
 
Wenye nacho huongezewa na asiyekuwa nacho ata kidogo alicho nacho hupokwa!
 
Ni sawa kabisa, msamaha ulikuwa umekaa kiupendeleo, kwanini uwe kwa wafanyakazi wa serikali tu? Wamerudisha usawa.

Seconded!!

Kuna watanzania wengi sana wanafanya kampuni binafsi wanalipwa mishahara midogo kuliko ya serikalini lakini hawanufaiki na misamaha hii.

HAKI SAWA KWA WOTE. Source CUF.
 
Back
Top Bottom