Msamaha kwa wale wote waliotukosea/Tuliowakosea

Emoj

JF-Expert Member
Oct 9, 2015
837
1,282
Habari wapendwa.Katika maisha yetu naamini kwa namna moja ama nyingine kuna waliotukwanza au tuliowakwanza. Leo nataka tuwatangazie MSAMAHA. huenda ikawa ni rafiki/ X wako/ mume/mke/Jirani yako/wazazi wako/ndugu au mtu yeyote yule aliyepelekea moyo wako kujeruhika.
Ni kweli umeugua sana na vidonda alivyokuachia ,ni kweli amekukwaza sana but Today tutue hiyo mizigo tumeshikilia mioyoni mwetu.Inatosha sasa.
Najua ni ngumu kusamehe but Mungu/Allah ni mwamnifu mwombe tu akupe moyo wa kusamehe huyo aliyekukosea.
Tukija kwa wakristo(waisilamu naomba mnisaidie pia maandiko ya Quran yanayotutaka tuwasamehe waliotukosea) Biblia inasema "Utusamehe makosa yetu kama nasi tunavyowasamehe waliotukosea" na pia inasema "Mkiwasamehe waliowakosea nanyi mtasamehewa makosa yenu. Means kama mkristo usipo samehe, usipo muachilia huyo mtu aliyekukosea moyoni mwako maana yake na wewe Hutosamehewa na Mungu.
Nawasihi wote ndugu zangu SAMEHE ALIYEKUKOSEA.mpigie simu au mtafute alipo mtangazie msamaha.kama ikiwezekana pateni soda pamoja. Mwambie nimekusamehe/Nisamehe.na kama ulishawahi kumkosea mtu pls and pls mtafute mwombe msamaha hata kwa message, mpigie Omba msamaha.Najua unawaza sasa atanionaje !! si ataona najipendekeza kwake??.Mpendwa Whatever atakavyokufikiria but wewe umetengeneza na yeye.
Lets love one another. dunia hii tunapita.hakuna mbabe kwa hilo.
Mbarikiwe sana na kwa wale waislamu Ramadhan Kareem.
 
Mm km yupo niliyemkosea leo anisamehe...km mdada aje nimpige na busu kbs
 
  • Thanks
Reactions: SDG
eb93f6cd816cc989c86423d7de993d23.jpg
 
I think inategemea na ulimuachaje mtu na mliachana katika stage gani na extent ya damage kutokana na huko kuachana kwenu.
Siombi msamaha kwa uasherati. Labda niombe kwa Mungu coz yeye ndio nilimkosea.
 
Mbona huombi msamaha?
Sidhani kama kuna mtu nilijua kuwa nimemkosea na sikumwomba msamaha. Me nikikukosea nakuwa hadi kero aisee, ntaomba msamaha kama naomba kazi vile lol. And kwa wanaonikoseaga, huwa nawasamehe hata kabla hawajaniomba msamaha + wengine hawajawahi hata kuniomba msamaha. Ila nilishawasamehe na sina kinyongo nao kabisaaaa
 
Siombi msamaha kwa uasherati. Labda niombe kwa Mungu coz yeye ndio nilimkosea.
Hivi imagine umemchumbia mtu ghafla ukamkimbia na akanywa sumu akafariki au mwingine hadi anachanganyikiwa. But hutojuta kwa sababu ni uasherati? Sometimes japo tunashare dhambi ila kuna maumivu tunayowapa wenzetu na yanaweza kubadilisha maisha yako kabisa. There is no harm in asking for forgiveness
 
Back
Top Bottom