Msakila KABENDE
JF-Expert Member
- Dec 28, 2017
- 510
- 314
Wanajf, salaam!!
Nachukuwa fursa hii kuwapa habari nyepesi na nzito za kuelekea uchaguzi mdogo jimboni Buyungu baada ya kufanya tathmini kwa vyama vilivyojitokeza kuomba ridhaa ya kuchaguliwa.
(i). Mhe Eng Chiza (CCM) - napewa kipaumbele kikubwa cha kushinda uchaguzi huo kwa kuwa ana mambo mengi aliyosaidia wakati akiwa Mbunge (miundombinu ya kilimo, afya, elimu, umwagiliaji, barabara, na wilaya mpya nk. Huyu pia ana nafasi ya kushinda kwa kuwa wana Buyungu wanapenda kuona rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli anafanya kazi na mtu mwenye mtizamo chanya na wababaishaji,
(ii). Eliya (CHADEMA) - huyu ni mtu mwenye uzoefu katika udiwani hana sifa nyingi zinazompa nafasi ya ushindi. Hakuna jambo alilowahi kuanzisha kwa fikra na ubunifu wake. Ikiwa huyu atachaguliwa huenda jimbo la Buyungu likapata Mbunge asiyeweza majukumu ya kibunge kwa kuwa hata mbuzi huanzia nyumbani kula mazao - lakini pia diwani huyu hana agenda iwezayo kupimwa badala yake anajijenga ktk kutumia nafasi ya uchaguzi wa kura ya maoni iliyofanyika ndani ya CCM kitambo.
Binafsi namuona mtu huyu akiwa na udhaifu wa kuwa agenda yao ya zamani ya kupambana na ufisadi ndiyo kwa kasi kubwa hufanywa na Mhe Dkt John Pombe Magufuli - hivyo wanaingia ktk uchaguzi wakiwa hawana agenda muhimu,
(iii). Wasiwasi Kasigara (ACT Wazalendo) - huyu ana hasara kwa kuwa chama chake pekee hakina mizizi kokote jimboni. Lakini pia ni mtu aliyekuwa na historia yoyote katika jimbo la Buyungu. Kwa haraka huyu ni mtu ambaye hata shughuli za kibunge hawezi wala hazifahamu vizuri. Kwa ujumla CCM bado kinaonekana kung'aa kwa wapiga kura kutokana na jinsi kinavyojipambanua kwa kazi kubwa ya kuleta maendeleo jimboni.
Natumaini kuwa kama wananchi hawatadanganyika basi CCM inashinda katika uchaguzi huu - hata hivyo haimaanishi kuwa kazi ya kupata ushindi ni ndogo. Remains to be my observations.
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
Msakila Mussa KABENDE
Shuhuda jimboni Buyungu 2018
Nachukuwa fursa hii kuwapa habari nyepesi na nzito za kuelekea uchaguzi mdogo jimboni Buyungu baada ya kufanya tathmini kwa vyama vilivyojitokeza kuomba ridhaa ya kuchaguliwa.
(i). Mhe Eng Chiza (CCM) - napewa kipaumbele kikubwa cha kushinda uchaguzi huo kwa kuwa ana mambo mengi aliyosaidia wakati akiwa Mbunge (miundombinu ya kilimo, afya, elimu, umwagiliaji, barabara, na wilaya mpya nk. Huyu pia ana nafasi ya kushinda kwa kuwa wana Buyungu wanapenda kuona rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli anafanya kazi na mtu mwenye mtizamo chanya na wababaishaji,
(ii). Eliya (CHADEMA) - huyu ni mtu mwenye uzoefu katika udiwani hana sifa nyingi zinazompa nafasi ya ushindi. Hakuna jambo alilowahi kuanzisha kwa fikra na ubunifu wake. Ikiwa huyu atachaguliwa huenda jimbo la Buyungu likapata Mbunge asiyeweza majukumu ya kibunge kwa kuwa hata mbuzi huanzia nyumbani kula mazao - lakini pia diwani huyu hana agenda iwezayo kupimwa badala yake anajijenga ktk kutumia nafasi ya uchaguzi wa kura ya maoni iliyofanyika ndani ya CCM kitambo.
Binafsi namuona mtu huyu akiwa na udhaifu wa kuwa agenda yao ya zamani ya kupambana na ufisadi ndiyo kwa kasi kubwa hufanywa na Mhe Dkt John Pombe Magufuli - hivyo wanaingia ktk uchaguzi wakiwa hawana agenda muhimu,
(iii). Wasiwasi Kasigara (ACT Wazalendo) - huyu ana hasara kwa kuwa chama chake pekee hakina mizizi kokote jimboni. Lakini pia ni mtu aliyekuwa na historia yoyote katika jimbo la Buyungu. Kwa haraka huyu ni mtu ambaye hata shughuli za kibunge hawezi wala hazifahamu vizuri. Kwa ujumla CCM bado kinaonekana kung'aa kwa wapiga kura kutokana na jinsi kinavyojipambanua kwa kazi kubwa ya kuleta maendeleo jimboni.
Natumaini kuwa kama wananchi hawatadanganyika basi CCM inashinda katika uchaguzi huu - hata hivyo haimaanishi kuwa kazi ya kupata ushindi ni ndogo. Remains to be my observations.
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
Msakila Mussa KABENDE
Shuhuda jimboni Buyungu 2018