Msajili wa Vyama vya Siasa akutana na Maafisa Wakuu Jeshi la Polisi

Sirro bwana hivi inakuwaje mikutano ya CCM haina tishio la usalama ila inapokuwa watu wa opposition tu ndio kunakuwa na tishio la usalama...Mbatia alilia sana
 
Ukitaka uendeshe nchi kwa kusikiliza wapinzani wa serikali wanasemaje lazima upotee mama endelea kuchapa kazi hao wapuuzi wacha wasemeee mpaka watachoka
Mwanamke hawezi kujiremba akarembeka bila kioo cha kutazama kirakacho mpa muonekano halisi wa sura yake.

Haiwezekani kutumia taswira aliyonayo kichwani mwake jinsi alivyo.

Upinzani kwa serikali ndio kioo cha serikali katika kujitengeneza na kujiremba.
Kama wewe ni popoma ipo siku ungekuwa mwanamke utakuja kupaka lipstick kwenye nyusi.
 
Kama maofisa wake hawajui PGO..bora wangeanza na semina elekezi kabla ya kukutana na Msajili.

Na huyu msajili around mid 2000s alikuwa RM pale Kisutu. Rekodi yake ilikuwaje ... inaweza kutupa clues kwa tabia zake za sasa...
 
Hapo yanatafutwa mazingira kubana zaidi shughuli za vyama ya siasa, maana Sasa hakuna sheria ya kuzuia vyama vya siasa kufanya mikutano ie eti uchaguzi ukiisha hakuna mikutano ya kisiasa kwa vyama vya siasa labda vile vyenye uwakilishi maana yake kuwabana wapinzani wasifanye shughuli za kisiasa Sasa hapo utajiuliza hivi vyama ni wakati gani vitashawishi wanachama wapya, itakuweje kwenye kutoa elimu ya uraia,vipi kuiamsha serikali inapokua imelala kwenye masuala ya ufisadi, ubadhirifu na uwajibikaji.
Tanzania tukikubali tupelekwe wanapotaka tufike tuwe na chama dola na vyama vya upinzani visivyo na meno ndio mwanzo wa mwisho wa Tanzania ya ahadi itakua ni shamba la bibi, maana CCM ndiko yamejaa majizi na wenyewe wanajua ndio maana wanatumia nguvu kubwa kudhoofisha upinzani.
Sioni mantiki ya msajili wa vyama vya siasa kukutana na polisi wakati sheria ziko wazi, polisi hana uhalali wa kuwazuia wanasiasa kufanya kazi zao na msajili kazi yake kusajili vyama vya K

Hapo yanatafutwa mazingira kubana zaidi shughuli za vyama ya siasa, maana Sasa hakuna sheria ya kuzuia vyama vya siasa kufanya mikutano ie eti uchaguzi ukiisha hakuna mikutano ya kisiasa kwa vyama vya siasa labda vile vyenye uwakilishi maana yake kuwabana wapinzani wasifanye shughuli za kisiasa Sasa hapo utajiuliza hivi vyama ni wakati gani vitashawishi wanachama wapya, itakuweje kwenye kutoa elimu ya uraia,vipi kuiamsha serikali inapokua imelala kwenye masuala ya ufisadi, ubadhirifu na uwajibikaji.
Tanzania tukikubali tupelekwe wanapotaka tufike tuwe na chama dola na vyama vya upinzani visivyo na meno ndio mwanzo wa mwisho wa Tanzania ya ahadi itakua ni shamba la bibi, maana CCM ndiko yamejaa majizi na wenyewe wanajua ndio maana wanatumia nguvu kubwa kudhoofisha upinzani.
Sioni mantiki ya msajili wa vyama vya siasa kukutana na polisi wakati sheria ziko wazi, polisi hana uhalali wa kuwazuia wanasiasa kufanya kazi zao na msajili kazi yake kusajili vyama vya siasa
Kama Chama tawala, CCM huwa wanafanya sana hafla tofauti tofauti kwa madhumuni ya kuwafikia wananchi kwa kueleza maendeleo au ahadi ambazo serikali inatoa kwa wananchi. Mikutano ya hadhara ni ya kawaida sana kwao, vyombo vya habari vinatumika sana kueleza itikadi zao. Ukiangalia upande wa pili utagundua kwamba vyama vya upinzani havipati nafasi hizi za kujieleza kwa wananchi na kufanya shughuli zao za uenezi. Nina amini kwamba kama shughuli zinafanywa kwa amani basi ni muhimu na sawa kwao kupata fursa hizi.
 
Kama Chama tawala, CCM huwa wanafanya sana hafla tofauti tofauti kwa madhumuni ya kuwafikia wananchi kwa kueleza maendeleo au ahadi ambazo serikali inatoa kwa wananchi. Mikutano ya hadhara ni ya kawaida sana kwao, vyombo vya habari vinatumika sana kueleza itikadi zao. Ukiangalia upande wa pili utagundua kwamba vyama vya upinzani havipati nafasi hizi za kujieleza kwa wananchi na kufanya shughuli zao za uenezi. Nina amini kwamba kama shughuli zinafanywa kwa amani basi ni muhimu na sawa kwao kupata fursa hizi.
Shida nadhani ni kutoelewa Demokrasia ndio maana hivi vyama ambavyo havina dola vinaitwa vya upinzani badala ya kuwa vyama mbadala, wanasema ukitaka kumuua mbwa mpe jina baya kwaiyo wamekomaa na jina la upinzani ili ionekane kila wanachofanya wao ni kupinga tu kumbe sio kweli kazi ya hivi vya visivyo na dola kazi yake ni kutoa mawazo, dira, sera na mitazamo mbadala kitu ambacho ni kizuri kwa maendeleo
 
Ukitaka uendeshe nchi kwa kusikiliza wapinzani wa serikali wanasemaje lazima upotee mama endelea kuchapa kazi hao wapuuzi wacha wasemeee mpaka watachoka
Ni kuangalua wapinzani wanasemaje au kuangalia katiba na sheria zinasemaje?

Migogoro mingine inatafutwa pasipokuwa na sababu,katiba ipo clear, sheria ipo clear lakini kwa sababu zisizojulikana unaamua kuvunja vyote (katiba na sheria) halafu unatafuta njia/namna ya kuondoa migogoro hiyo hiyo

Wakati dawa ya tatizo ipo clear kabisa, KUFUATA KATIBA NA SHERIA!
 
Back
Top Bottom