Msajili wa vyama vya siasa adhibitiwe kabla hajaleta madhara kwa Taifa

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,271
Lengo la msajili wa vyama vya siasa ni kusajili na kuvilea vyama vyote kwenye misingi ya sheria bila kuleta ubaguzi wa aina yeyote.

Msajili wa vyama anatakiwa atambue kuwa chama cha upinzani kipo kisheria 'is a government in waiting', atambue pia vyama ni watu wenye mawazo tofauti, kwahiyo haiwezekani wote wakawa chama kimoja. Inapotokea mlezi anakwenda kinyume na malengo ni dhahiri watu hawatakubali na matokeo yake ni kusababisha uvunjifu wa amani.

Hadi sasa Msajili ameonyesha wazi na dalili ziko wazi kuwa hayuko kwa ajili ya kuvilea vyama bali kuua vyama hasa vinavyoonekana kutokubaliana na matakwa ya watawala. Angekuwa mlezi asingekubali sheria mpya ya vyama vya siasa inayokwenda kunyonga uhuru na haki ya vyama. Ameiua CUF sasa anataka kuiua ACT Wazalendo bila kuwa na sababu za msingi.

IMG_20190326_215852.jpg


Msajili asijidanganye hakuna chama kikubwa chenye usajili wa kudumu kitakachokubali kufutiwa usajili kwa utashi wa mtu mmoja pasipo kosa kuthibitishwa na mahakama. Mfano msajili atajilidhisha vipi watu wanaochoma bendera ni wafuasi wa chama fulani kama hana chombo cha kufanya upelelezi.

Tuendako ni giza, inabidi zitumike nguvu za ziada kumzuia as soon as possible, vyama vya siasa vikiendelea kumchekea vitaumizwa viungane kukemea, wanaharakati wakemee, wazee na viongozi wa dini wakemee, jumuiya za kimataifa zijulishwe, na wananchi wote wazalendo wanaoitakia mema nchi hii wamkemee msajili mapema kabla hajaliletea taifa vita ya wenyewe kwa wenyewe kutokana na ubaguzi anaouonyesha waziwazi.
 
Hata ungekuwa ww ndio msajili wa vyama vya siasa ungefanya kama yeye, tena huenda ungefanya vibaya zaidi yake. Sheria nzima iliyopita ya vyama vya siasa ndio chanzo cha yote hayo. Na amini usiamini sheria hiyo ni rasmi kwa cdm na Maalim Seif. Hiyo ACT ni kwakuwa Zitto kanunua ugomvi kwa kumpokea Maalim.

Alaaniwe Lowassa na kundi la viongozi wachache wa cdm waliompokea Lowassa baada ya kuchukua asali yake, hatimaye Lowassa akaingiza siasa za kikondoo ndani ya cdm matokeo yake ndio haya watu wameingia woga. Leo hii zinatungwa sheria zenye nia ovu kama enzi za makaburu na watu wako kimya tu.
 
Yuko kwenye experimenti kuona kama Tanzania kunaweza kutokea vurugu, wanauhakika watanzania ni wajinga na wanaweza kuburuzwa vyovyote.,
 
Hata ungekuwa ww ndio msajili wa vyama vya siasa ungefanya kama yeye, tena huenda ungefanya vibaya zaidi yake. Sheria nzima iliyopita ya vyama vya siasa ndio chanzo cha yote hayo. Na amini usiamini sheria hiyo ni rasmi kwa cdm na Maalim Seif. Hiyo ACT ni kwakuwa Zitto kanunua ugomvi kwa kumpokea Maalim.

Alaaniwe Lowassa na kundi la viongozi wachache wa cdm waliompokea Lowassa baada ya kuchukua asali yake, hatimaye Lowassa akaingiza siasa za kikondoo ndani ya cdm matokeo yake ndio haya watu wameingia woga. Leo hii zinatungwa sheria zenye nia ovu kama enzi za makaburu na watu wako kimya tu.
Labda kidogo umeongea bila woga kama mleta mada!
 
Hii "Plan B" imekuja baada ya ile ya kwanza iliyolenga kuuwa vyama vya upinzani kabla ya 2020 kushindikana na ndio, obviously, ilipelekea kujeruhiwa kwa Lissu pamoja na nunua nunua ya wabunge na madiwani.

Sasa hii nayo inaelekea kule kule kufeli na kwa kuwa kinyume cha ustaarabu ni ushenzi, then dunia ya wastaarabu hawataukubali huu ushenzi ufaulu..

Tunaiomba jumuia ya kimataifa iingilie kati kwa kuishinikiza huu utawala uheshimu katiba ambayo ina-guarantee uwepo wa vyama vingi ktk nchi la sivyo nchi hii iwekewe vikwazo kama ilivyowahi kuwekewa mataifa mengine yasiyoheshimu demokrasia na utawala wa sheria na ambazo zinaendesha mambo kinyume cha ustaarabu. No way out.
 
Ukizibiti gambas problems solved, ila upinzani lazima uwe na jeshi lao, hata la kuazima kutoka kenya sio mbaya vinginevyo upinzani utaendelea kupakatwa tu na gambas.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii "Plan B" imekuja baada ya ile ya kwanza iliyolenga kuuwa vyama vya upinzani kabla ya 2020 kushindikana na ndio, obviously, ilipelekea kujeruhiwa kwa Lissu pamoja na nunua nunua ya wabunge na madiwani.

Sasa hii nayo inaelekea kule kule kufeli na kwa kuwa kinyume cha ustaarabu ni ushenzi, then dunia ya wastaarabu hawataukubali huu ushenzi ufaulu..

Tunaiomba jumuia ya kimataifa iingilie kati kwa kuishinikiza huu utawala uheshimu katiba ambayo ina-guarantee uwepo wa vyama vingi ktk nchi la sivyo nchi hii iwekewe vikwazo kama ilivyowahi kuwekewa mataifa mengine yasiyoheshimu demokrasia na utawala wa sheria na ambazo zinaendesha mambo kinyume cha ustaarabu. No way out.

Hili la vikwazo kwenye mambo mengi ninaliunga sana mkono. Bila hivyo labda machafuko yatokee wangalau ndio suluhu itapatikana.
 
Ccm ndio tatizo wala sio Msajili

Siku watu tutakaposema ccm basi ndio itakuwa mwisho wa ujinga unaendelea..
Ni kweli Mkuu. Kuna kile kitengo ndani ya ccm kinachoitwa KAMATI YA SIASA UCHUMI NA FEDHA ndicho kinachotoa maagizo kwa chombo chochote au kwa Taasisi yeyote ile au kwa yeyote yule ndani ya ya chama au serikalini bila kujali cheo au Taaluma ya mtu bali wanahitaji utekelezaji tu. Hutoa maagizo hata kwa Mihimili mingine bila kujali adhari zitokanazo na maagizo yao. Dawa ni kupambana na ccm na sio Msajili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Baba akionyesha upendeleo kwa mtoto mmoja matokeo yake huwa watoto tengwa hujifariji kwa kuwa wahuni.

Tusubiri hii sheria ndo itakuwa kaburi la CCM. CCM inajiua yenyewe kupitia hii new gvt isiyokuwa na busara wala mipango ya kiutawala zaidi ya sifa tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kweli Mkuu. Kuna kile kitengo ndani ya ccm kinachoitwa KAMATI YA SIASA UCHUMI NA FEDHA ndicho kinachotoa maagizo kwa chombo chochote au kwa Taasisi yeyote ile au kwa yeyote yule ndani ya ya chama au serikalini bila kujali cheo au Taaluma ya mtu bali wanahitaji utekelezaji tu. Hutoa maagizo hata kwa Mihimili mingine bila kujali adhari zitokanazo na maagizo yao. Dawa ni kupambana na ccm na sio Msajili.

Sent using Jamii Forums mobile app

Hiyo kamati nguvu yao yote ni madaraka ya rais. Hiyo kamati ikashapanga mipango wanaagiza hizo taasisi kutekeleza amri hiyo, amri hiyo huitwa amri toka juu. Mkuu yoyote wa taasisi atakayepinga kushiriki hiyo dhuluma ajira yake inasitishwa kwa madaraka ya urais. Ndio maana piga ua ccm hawako tayari kuona mabadiliko yoyote ya madaraka ya urais kwani wanajua ndio hirizi ya wao kubaki madarakani.
 
Hata ungekuwa ww ndio msajili wa vyama vya siasa ungefanya kama yeye, tena huenda ungefanya vibaya zaidi yake. Sheria nzima iliyopita ya vyama vya siasa ndio chanzo cha yote hayo. Na amini usiamini sheria hiyo ni rasmi kwa cdm na Maalim Seif. Hiyo ACT ni kwakuwa Zitto kanunua ugomvi kwa kumpokea Maalim.

Alaaniwe Lowassa na kundi la viongozi wachache wa cdm waliompokea Lowassa baada ya kuchukua asali yake, hatimaye Lowassa akaingiza siasa za kikondoo ndani ya cdm matokeo yake ndio haya watu wameingia woga. Leo hii zinatungwa sheria zenye nia ovu kama enzi za makaburu na watu wako kimya tu.
Ni kweli kabisa huu ufisadi wa Kisiasa unawapa mafisadi ujasiri mana wanakula bata na familia zao kwa kusababisha maumivu kwa wengine.

Msajili ameshaona kuwa mambo yake yanamnyookea kwa kudhulumu vyama Mbadala. Haezi kuacha mana ndipo anapopatia umaarufu wake kwa kulivuruga Taifa.
Amini usiamini kama wanasiasa hawapati vikwazo vya kuwaumiza wao na familia zao wanaweza hata wakaamuru mabomu ya sumu na cooa halaiki ya watu. Watatumia watu wanaojipendekeza ndani ya Taasisi zote kuanzia Dola ,mahakama ,bunge,dini,waandishi ,tume ya uchaguzi.
Kuna Mkubwa mmoja wa vyombo vya dola alivunja katiba na kanuni za utumishi wa vyombo vya ulinzi kwa kunainisha wazi kuwa ni kada wa CCM na kusema Kidumu chama cha mapinduzi milele. Huku akisema wazi kuwa hapendi vyama vya Upinzani. Matokeo yake yalionekana kupata ulinzi wa cheo na wadhifa wake hata pale mabegi ya pesa za rushwa ili madini yatoroshwe yalipookamatwa chini ya himaya yake na utata mkubwa kuibuka.
Tofauti na yule mwingine ambaye hakuna hata mia iliyokua imekamatwa kama ushahidi wa rushwa ya kutoroshwa kahawa kimagendo ; yeye alipumzishwa pembeni kupisha uchunguzi mpaka sasa.

Watu wanaohatarisha amani ya nchi kwa kulinda maslahi yao ni hatari sana ndani ya serikali na hata vyama vya siasa. Tumemuona Lipumba ameua chama kwa maslahi yake.
Tunamuona Mbowe pia ameua demokrasia na moyo wa mapambano ya kudai demokrsia kwa sababu ya kung'ang'ania madaraka. Mbowe anataka Rais wa nchi aweke mazingira sawa ya kuendesha shughuli za kidemokrasia bila kujiuliza kuwa yeye ameweka mazingira sawa ya kidemokrasia ndani ya Chama chake cha Chadema!! Au amesahau kuwa neno msaliti alilianzisha yeye na sasa CCM na serikali yake wanalitumia kwa kila wasiyemtaka ?


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu Mutungi sasa amekuwa mfutaji na muadhibu wa vyama vya kisiasa badala ya kuwa msajili na mlezi wa vyama vya siasa. Asicheze na binadamu hatowaweza.
 
Back
Top Bottom