Msajili wa vyama vipi unaisakama Chadema kuhusu kuchagua Mwenyekiti wao, wakati UDP na TLP wenye wenyeviti wa kudumu huwagusi?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,480
30,152
Nimesoma kwenye vyombo vya habari, Mwenyekiti wa vyama vya siasa nchini, akiwaandikia barua Chadema na kuwapa muda hadi tarehe 7/10/2019 wajieleze ni kwanini asiwachukulie hatua kutokana na kukiuka kufanya uchaguzi wa chama chao??

Ameendelea kuelezea msajili huyo wa vyama kuwa muda wa kukaa madarakani kwa Mbowe umekwisha, kwa madai yake kuwa chama hiko kilifanya uchaguzi wake tarehe 14/9/2014 na hivyo kufanya chama hiko kikose uongozi halali ilipofika tarehe 15/9/2019

Nimekuwa nikijiuliza hivi huyu msajili wa vyama anaendelea kuisakama Chadema kwa misingi ipi??

Kama ni wenyeviti wa vyama waliokaa muda mrefu kwa kuzibunja Katiba ya vyama vyao, basi ni UDP, ambayo Mwenyekiti wake John Cheyo, ameendelea kukikalia kiti hicho na kukifanya kuwa cha maisha, kwani aliteuliwa kuwa Mweyekiti, tokea mwaka 1994

Vile vile bila kusahau chama cha TLP, ambacho pia Mwenyekiti wake, Augustine Mrema, amekishikkilia cheo hicho na kukifanya kama Mali yake binafsi!

Hivi msajili wa vyama unaweza kweli kuiandikia barua ya vitisho Chadema kwa kutochagua Mwenyekiti wake, wakati ukijua kuwa chama hicho nimekuwa kikipokezana vijiti vya Mwenyekiti, kwani tokea kianzishwe, nafasi hiyo imekakiwa kwa zamu na wenyeviti watatu, ambao ni Edwin Mtei, Bob Makani na hivi sasa, Freeman Mbowe

Hivi chama cha Chadema kitakuwa na tofauti gani na CCM, ambayo nayo imekuwa na wenyeviti watatu, tokea miaka hiyo ya kurejea kwa mfumo wa vyama vingi, ambao ni Benjamin Mkapa, Jakaya Kikwete na hivi sasa John Pombe Magufuli??

Hivi hii serikali mmeona haijatosha, kwa "kuwabambikia" kesi ya uchuchezi, viongozi wakuu wa chama cha Chadema na hivi sasa mnataka mtimize azma yenu ya kutaka kukifuta kabisa??

Huu ubabe wenu mnaoutembeza kwa chama kikuu cha upinzani nchini, cha Chadema, hakika msione kuwa wananchi hawaoni, Bali ni uvumilivu wao pekee ndiyo unaoifanya nchi hii iendelee kuwa na amani.

Siku uvumilivu huo utakapofika kikomo, hakika "damu" itamwagika nchi hii
 
Fahmi Davutwa hapa UPDP nawasiliana na mwenyekiti wa PPT MAENDELEO nipo hapa nawasiliana na Mbowe tumilikishwe tu hivi vyama.
 
Uwezo wa ccm nikutumia vyombo vya ulinzi na usalama vya uma kujinufaisha na kuvunja katiba

Ccm imeacha kushughulika na lengo kuu kimsingi, kutokomeza maradhi, umaskini na ujinga

Kwasasa ccm inapambana na hasa kuwapoteza wale wote wenye maono Bora kiuchumi, kijamii na kidemokrasia

Ccm ndio chimboko la
Elimu mbovu, zaidi ya miaka 50 ya uhuru
afya mbovu , zaidi ya miaka 50 ya uhuru
Miundombinu ya hovyohovyo kwa zaid ya miaka 50 ya uhuru

Bahati mbaya wanadhibiti siasa, wanasiasa na vyama vya siasa ambavyo vinaibuwa msukumo na changamoto ilikupata ushindani ambao ungetupekelea kupiga hatua za maendeleo ya kweli kwa kasi na kwa muda mfupi.

Bila ushindani tutabakia wajinga siku zote maana tutajitekenya nakucheka kwa takwimu feki za kiuchumi, Elimu, Afya nk

Kila siku tutabumba maendeleo katika makaratasi ilihali uhalisia tunaporomoka kwa kasi katika maisha halisi ya watanzania.
 
Wana Chadema baadhi wanapiga kampeni Mbowe aendelee kuongoza chama kama Mwenyekiti maana uongozi wake ni bora sana,Wanasema achukue form kugombea tena.Je sisi wana ccm tukipendekeza Mheshimiwa Raisi aongoze miaka 20 kuna ubaya?Mbona wao Mbowe hang'atuki?
Uwezo wa ccm nikutumia vyombo vya ulinzi na usalama vya uma kujinufaisha na kuvunja katiba

Ccm imeacha kushughulika na lengo kuu kimsingi, kutokomeza maradhi, umaskini na ujinga

Kwasasa ccm inapambana na hasa kuwapoteza wale wote wenye maono Bora kiuchumi, kijamii na kidemokrasia

Ccm ndio chimboko la
Elimu mbovu, zaidi ya miaka 50 ya uhuru
afya mbovu , zaidi ya miaka 50 ya uhuru
Miundombinu ya hovyohovyo kwa zaid ya miaka 50 ya uhuru

Bahati mbaya wanadhibiti siasa, wanasiasa na vyama vya siasa ambavyo vinaibuwa msukumo na changamoto ilikupata ushindani ambao ungetupekelea kupiga hatua za maendeleo ya kweli kwa kasi na kwa muda mfupi.

Bila ushindani tutabakia wajinga siku zote maana tutajitekenya nakucheka kwa takwimu feki za kiuchumi, Elimu, Afya nk

Kila siku tutabumba maendeleo katika makaratasi ilihali uhalisia tunaporomoka kwa kasi katika maisha halisi ya watanzania.
 
Nimesoma kwenye vyombo vya habari, Mwenyekiti wa vyama vya siasa nchini, akiwaandikia barua Chadema na kuwapa muda hadi tarehe 7/10/2019 wajieleze ni kwanini asiwachukulie hatua kutokana na kukiuka kufanya uchaguzi wa chama chao??

Ameendelea kuelezea msajili huyo wa vyama kuwa muda wa kukaa madarakani kwa Mbowe umekwisha, kwa madai yake kuwa chama hiko kilifanya uchaguzi wake tarehe 14/9/2014 na hivyo kufanya chama hiko kikose uongozi halali ilipofika tarehe 15/9/2019

Nimekuwa nikijiuliza hivi huyu msajili wa vyama anaendelea kuisakama Chadema kwa misingi ipi??

Kama ni wenyeviti wa vyama waliokaa muda mrefu kwa kuzibunja Katiba ya vyama vyao, basi ni UDP, ambayo Mwenyekiti wake John Cheyo, ameendelea kukikalia kiti hicho na kukifanya kuwa cha maisha, kwani aliteuliwa kuwa Mweyekiti, tokea mwaka 1994

Vile vile bila kusahau chama cha TLP, ambacho pia Mwenyekiti wake, Augustine Mrema, amekishikkilia cheo hicho na kukifanya kama Mali yake binafsi!

Hivi msajili wa vyama unaweza kweli kuiandikia barua ya vitisho Chadema kwa kutochagua Mwenyekiti wake, wakati ukijua kuwa chama hicho nimekuwa kikipokezana vijiti vya Mwenyekiti, kwani tokea kianzishwe, nafasi hiyo imekakiwa kwa zamu na wenyeviti watatu, ambao ni Edwin Mtei, Bob Makani na hivi sasa, Freeman Mbowe

Hivi chama cha Chadema kitakuwa na tofauti gani na CCM, ambayo nayo imekuwa na wenyeviti watatu, tokea miaka hiyo ya kurejea kwa mfumo wa vyama vingi, ambao ni Benjamin Mkapa, Jakaya Kikwete na hivi sasa John Pombe Magufuli??

Hivi hii serikali mmeona haijatosha, kwa "kuwabambikia" kesi ya uchuchezi, viongozi wakuu wa chama cha Chadema na hivi sasa mnataka mtimize azma yenu ya kutaka kukifuta kabisa??

Huu ubabe wenu mnaoutembeza kwa chama kikuu cha upinzani nchini, cha Chadema, hakika msione kuwa wananchi hawaoni, Bali ni uvumilivu wao pekee ndiyo unaoifanya nchi hii iendelee kuwa na amani.

Siku uvumilivu huo utakapofika kikomo, hakika "damu" itamwagika nchi hii
Kwanza unatakiwa ukiri ni kweli katiba ya chadema imevunjwa kabla ya kumwaga hiyo damu!
 
Mkuu CHADEMA yenyewe hujipambanua kwamba ni chama kikubwa cha upinzani. Kihalisia hivyo vyama ni vidogo sana kulinganisha na CHADEMA. CHADEMA imekuwa ikilalamika inanyimwa haki nyingi katika utawala wa sasa, hivyo basi walipaswa wawe makini na kuepuka makosa kama haya. Lakini pia ukishikwa na kupelekwa mahakamani kwa kesi ya wizi, huwezi sema mahakamani mbona mmemwacha fulani kwa sababu na yeye ni mwizi.
 
Nimesoma kwenye vyombo vya habari, Mwenyekiti wa vyama vya siasa nchini, akiwaandikia barua Chadema na kuwapa muda hadi tarehe 7/10/2019 wajieleze ni kwanini asiwachukulie hatua kutokana na kukiuka kufanya uchaguzi wa chama chao??

Ameendelea kuelezea msajili huyo wa vyama kuwa muda wa kukaa madarakani kwa Mbowe umekwisha, kwa madai yake kuwa chama hiko kilifanya uchaguzi wake tarehe 14/9/2014 na hivyo kufanya chama hiko kikose uongozi halali ilipofika tarehe 15/9/2019

Nimekuwa nikijiuliza hivi huyu msajili wa vyama anaendelea kuisakama Chadema kwa misingi ipi??

Kama ni wenyeviti wa vyama waliokaa muda mrefu kwa kuzibunja Katiba ya vyama vyao, basi ni UDP, ambayo Mwenyekiti wake John Cheyo, ameendelea kukikalia kiti hicho na kukifanya kuwa cha maisha, kwani aliteuliwa kuwa Mweyekiti, tokea mwaka 1994

Vile vile bila kusahau chama cha TLP, ambacho pia Mwenyekiti wake, Augustine Mrema, amekishikkilia cheo hicho na kukifanya kama Mali yake binafsi!

Hivi msajili wa vyama unaweza kweli kuiandikia barua ya vitisho Chadema kwa kutochagua Mwenyekiti wake, wakati ukijua kuwa chama hicho nimekuwa kikipokezana vijiti vya Mwenyekiti, kwani tokea kianzishwe, nafasi hiyo imekakiwa kwa zamu na wenyeviti watatu, ambao ni Edwin Mtei, Bob Makani na hivi sasa, Freeman Mbowe

Hivi chama cha Chadema kitakuwa na tofauti gani na CCM, ambayo nayo imekuwa na wenyeviti watatu, tokea miaka hiyo ya kurejea kwa mfumo wa vyama vingi, ambao ni Benjamin Mkapa, Jakaya Kikwete na hivi sasa John Pombe Magufuli??

Hivi hii serikali mmeona haijatosha, kwa "kuwabambikia" kesi ya uchuchezi, viongozi wakuu wa chama cha Chadema na hivi sasa mnataka mtimize azma yenu ya kutaka kukifuta kabisa??

Huu ubabe wenu mnaoutembeza kwa chama kikuu cha upinzani nchini, cha Chadema, hakika msione kuwa wananchi hawaoni, Bali ni uvumilivu wao pekee ndiyo unaoifanya nchi hii iendelee kuwa na amani.

Siku uvumilivu huo utakapofika kikomo, hakika "damu" itamwagika nchi hii
Huyu msajili ni kada mtiifu na mwaminifu wa ccm, anafanya kazi kwa kutekeleza maagizo ya mwenyekiti wa ccm. Yaani kwa ufupi kashikiwa akili.
 
Mkuu CHADEMA yenyewe hujipambanua kwamba ni chama kikubwa cha upinzani. Kihalisia hivyo vyama ni vidogo sana kulinganisha na CHADEMA. CHADEMA inasema inanyimwa haki nyingi sasa, hivyo wanapaswa wawe makini na vitu vidogovidogo kama hivi. Lakini pia ukishikwa na kesi ya wizi, huwezi sema mahakamani mbona fulani mmemwacha kwa sababu na yeye ni mwizi.
Najua kuwa mission yao haijakamilika......

Unakumbuka vigogo wa Lumumba wamekuwa wakijiapizaje??

Lazima Chadema iwe imekufa kwa hali yoyote ike ifikapo 2020!
 
Wana Chadema baadhi wanapiga kampeni Mbowe aendelee kuongoza chama kama Mwenyekiti maana uongozi wake ni bora sana,Wanasema achukue form kugombea tena.Je sisi wana ccm tukipendekeza Mheshimiwa Raisi aongoze miaka 20 kuna ubaya?Mbona wao Mbowe hang'atuki?

Miaka 20 kuiongoza ccm ni majukum yenu ccm wenyewe. Anaweza kuwa wa maisha mwenyekiti wa ccm mkiamua

Tunaongelea wenyeviti wa vyama..... weka akili hili usitoke nje ya mada
 
Kuna vitu chadema wanavisababisha wenyewe wakibanwa wanasingizia ccm.mfano suala la kufanya uchaguzi ccm wanahusikaje.pili kipindi jeshi la polis linazuia mikutano yao kinyume na sheria kwa nini hawakuandika barua kwa Mkuu Wa jeshi la polis rasmi na nakala kupeleka kwa msajili? Badala yake wanaishia kulalamika tu. Ni saws na hili la rais kuteua kada mwanaccm kuwa mkurugenzi Wa tume wako tu, kwa nini msifungue kesi?
 
Ungeweka katiba ya UDP tuone inasemaje kuhusu uenyekiti wa Cheyo.

Anachoangalia Msajili ni kilichopo kwenye katiba yenu wenyewe mliyompatia kwa hiyo mkiamua kutoa kabisa utaratibu wa kuchaguana,Msajili hana la kuhoji.

Huu utetezi wa mbona fulani as if katiba zote zinafanana ni uhayawani.
 
Hivi vyombo vya umma vinahofia nini endapo ccm ikiondoka madarakani?. Mkuu wa majeshi,polisi na jaji mkuu hata ccm kila siku inabadilisha, mafao yao yapo palepale. Hata kwenye ndoa bila ya upinzani wa mchepuko ndoa hainogi, ondoa ccm weka upinzani madarakani.



Ndukiiiii 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
 
Ungeweka katiba ya UDP tuone inasemaje kuhusu uenyekiti wa Cheyo.

Anachoangalia Msajili ni kilichopo kwenye katiba yenu wenyewe mliyompatia kwa hiyo mkiamua kutoa kabisa utaratibu wa kuchaguana,Msajili hana la kuhoji.

Huu utetezi wa mbona fulani as if katiba zote zinafanana ni uhayawani.
Wewe uliyeisoma Katiba ya UDP tueleze inaongelea nini kuhusu kuchagua Mwenyekiti wao??

Je wanasema akichaguliwa Mwenyekiti atakuwa wa maisha??

Kama Katiba yao ndivyo isemavyo, ni kwanini msajili wa vyama hatishi kukifuta, kwa kuwa chama hicho siyo cha kidemokrasia??
 
Wewe uliyeisoma Katiba ya UDP tueleze inaongelea nini kuhusu kuchagua Mwenyekiti wao??

Je wanasema akichaguliwa Mwenyekiti atakuwa wa maisha??

Kama Katiba yao ndivyo isemavyo, ni kwanini msajili wa vyama haingilii kati kwa kuwa chama hicho siyo cha kidemokrasia??
Hiyo ni kazi yako uliyeleta habari za TLP na UDP!

Aliyekuambia hayo ni majukumu ya Msajili ni nani?
 
Hiyo ni kachacliyeleta habari za TLP na UDP!

Aliyekuambia hayo ni majukumu ya Msajili ni nani?
Mimi nafahamu kuwa hakuna Katiba yoyote ya chama chochote cha siasa nchini, inayosema kuwa Mwenyekiti wake atakuwa wa maisha............

Sasa swali linarudi kwako, ni kwanini msajili wa vyama vya siasa havitishii kuvifuta vyama hivyo vya UDP na TLP na kila siku yeye ni kuking'ang'ania chama cha Chadema pekee??
 
Pole sana. Sijui ndio itakusaidiaje kusafisha huo ukandamizaji wenu?
Nia ya shetani ilikwisha fahamika kitambo lakini haitomsaidia kukubalika toka moyoni zaidi ya kuimarisha fashion ya unafiki ambao hivi sasa unatisha kuliko ilivyokuwa China wakati wa Mao tse tung.
Ukandandamizaji ni 'MBINU' ya waliyofilisika uwezo wa kuongoza kama historia ilivyokwisha thibitisha kwa makaburu/ Romania/Hitler/Sadam/Gadafi etc.
Kwanza unatakiwa ukiri ni kweli katiba ya chadema imevunjwa kabla ya kumwaga hiyo damu!
 
Back
Top Bottom