Msajili wa NGO's omba msamaha kwa kumkwaza Mh Rais

PANAFRICA

JF-Expert Member
Apr 2, 2012
335
496
Leo nimeona kwenye tovuti msajili wa NGOs akitoa taarifa kwa NGOs zote nchini kufanyiwa uhakiki kuanzia tarehe 21 August 2017- 31 August 2017.Uhakiki huo utafanyika kwenye makao makuu kanda kwa maana ya kanda ya mashariki,kati,kaskazini, ziwa na nyanda za juu kusini.
Kwanza nipongeze nia ya selkari ya kufanya uhakiki wa mashirika yasiyo ya kiselkari ni jambo jema kwa mstakabari na maslahi mapana ya usalama wa nchi yetu.
Wasiwasi wangu nikuwa zoezi hili litawakwaza sana wadau wa sekta ya NGO ambao watalazimika kusafiri kutoka wilayani, mikoani kwenda ngazi ya kanda, ukizingatia suala zima la raslimali muda, fedha na muda uliopangwa kwa zoezi hilo utaona kuwa ni kikwazo kikubwa kwa NGOs ambazo hutegemea zaidi ya hisani ya michango ya wananchama na wabia wa maendeleo.
Zoezi hili lisiporatibiwa kwa umakini na ustadi, linaweza kutengeneza mazingira na mianya ya rushwa kutokana na idadi kubwa ya NGOs zitakazo jitokeza kwa ajili ya uhakiki ndani ya muda wa siku kumi. Watu wamekuwa wakitumia fursa ya speed ya utendaji wa Rais kwa kutengeneza mianya ya rushwa.
Nakumbuka idara ya uhamiaji waliwahi kutangaza nafasi za kazi 200 waka shortlist watu 10,000 kwa ajili ya interview. likuja gundulika baadae kuwa ilikuwa ni kutengeneza mazingira ya rushwa, naomba tusifike huko, tusimkwaze Rais wetu, badala yake tuunge mkono jitihada zake kwa dhati.
Rais Magufuri akiwa Tanga juzi ameweka bayana kuwa watendaji wa Selkari wasiwe chanzo cha kero kwa wananchi, alisema yeye yupo, mawaziri wapo, wakuu wa mikoa wapo , wakuu wa wilaya wapo ili kushughurikia kero kwa namna yeyote ile. Wiki haijapita baada ya tamko la Mhe. Rais, msajili wa NGOs anaibuka na tamko kuwa viongozi wa NGOs wasafiri umbali wote huo bila kuzingatia uhalisia wa ghalama kwenda kwenye kanda kwa ajili ya uhakiki!!
Msajili anajua fika kuwa NGOs nyingi zinaendeshwa na wananchi, ili kusaidiana na Selkari kufikisha huduma na maendeleo kwa jamii ya watanzania, anajua fika kuwa ghalama za kusafiri kula na kulala ngazi ya kanda zingeweza kuboresha huduma kwa walengwa ndani ya jamii.

Pamoja na unyeti wa zoezi lenyewe ambalo naunga mkono mia kwa mia niombe mamlaka za juu ziangalie jinsi ya kufanya zoezi hili kwa umakini na ufanisi bila ya kuzua manu`guniko, pengine ni vyema walau zoezi hili likafanyika ngazi ya mkoa, amabapo Mhe. Rais amatuhakikishia kuwa selkari ipo na ina uwezo wa kutoa huduma kikamilifu bila kulazimika kufuata huduma hiyo ngazi ya kanda. Mwisho ni vyema Msajili wa NGOs na washauri wake wajipime katika hili kisha waungane na wale wote walio omba msamaha kwa kumkwaza Mhe. Rais.
 

Attachments

  • UHAKIKI_NGOs.pdf
    24.3 KB · Views: 100
Ndiyo katika zile jitihada za mhimili moja kuendelea kujichimbia chini zaidi, yule Kamanda maarufu nchini huita nanihii.

Kuna NGO zinatakiwa kufungiwa hapo maelekezo Toka juuu....sio bureee!!! Subiri utaelewa!! Kuna NGO zinalengwa!
 
Kuna NGO zinatakiwa kufungiwa hapo maelekezo Toka juuu....sio bureee!!! Subiri utaelewa!! Kuna NGO zinalengwa!
Kama kuna NGO ambazo hazifuati taratibu na zifungiwe, hapa hoja ni jinsi mchakato wa uhakiki kufanyika ngazi ya kanda, wakati ungeweza kufanyika ngazi ya mkoa hata wilaya kwa kuhakiki hata uwepo wa ofisi. Hii ya kutafuta barua toka wilayani itapelekea mianya ya rushwa hasa kwa briefcase NGOs ambazo hazina ofisi.Hili zoezi lingefanyika kwa umakini mkubwa kwa msajili kushirikiana na viongozi ngazi ya wilaya na mkoa kuhakiki hata maeneo ya ofisi zilipo na kufanya phyical mapping. Vinginevyo watu watajipigia hela kwa kisingizio cha kuendana na kasi ya Mhe. Rais huku wakisababisha kero zisizokuwa za lazima kwa wananchi.
 
Hii serekali huwa haikai na wadau husika kabla ya kutoa agizo na ndio maana maagizo yao yakitoka yanashindwa kutekelezeka zinabaki kelele tu. NGO iko huko endasaki manyara unamwambia aje kuhakiki Kilimanjaro, why asihakiki hapo manyara ambako kijiji, kata, tarafa na wilaya zinamjua?Mambo mengine ni kero tu, ila nina hisi kuna NGO zinatafutwa hapa na list tayari iko mezani.
 
Hii serekali huwa haikai na wadau husika kabla ya kutoa agizo na ndio maana maagizo yao yakitoka yanashindwa kutekelezeka zinabaki kelele tu. NGO iko huko endasaki manyara unamwambia aje kuhakiki Kilimanjaro, why asihakiki hapo manyara ambako kijiji, kata, tarafa na wilaya zinamjua?Mambo mengine ni kero tu, ila nina hisi kuna NGO zinatafutwa hapa na list tayari iko mezani.
Ndo shida ya kuzungukwa na washauri wanotanguliza matumbo kufikiri, huu ni mchongo wa wajanja fulani pale ofisi ya msajili, wengine wanakaribia kustaafu wanaangalia watoke vipi. Vinginevyo wajitokeze hapa janvini waeleze kwa nini wanafanyia uhakiki kwenye kanda badala ya mahala NGO zilipo. Hii ya kutengeneza msongamano wa watu ku scramble kwenye kanda ni ka mkakati fulani ka kujipatia chochote na kamesukwa kwa ustadi mkubwa. Unamwambia mtu sijui aje na vyeti vya usajili, mikataba ya washirika, unategemea kama mkataba una magumashi mwenye nao ataweza kukuletea just like that? ababe tu akuletee akijua una magumashi!! hiyo ni verification gani inayoacha maswali mengi ya kujiuliza?
 
Back
Top Bottom