Msajili wa Hazina Ndg. Lawrence Mafuru hajui au kashasahau lugha ya Taifa ya Kiswahili?

Pole ndugu.. unajua hata wale ambao kiingereza ni lugha yao ya kwanza huwa wanashangaa sana wanapotusikiliza au kusoma kingereza chetu wabongo! tunapendaga kutumia maneno magumu magumu ili kuonyesha kwamba tunajua sana hii lugha. Uliwahi kusoma lugha alizokuwa anatumia mzee "Punch" miaka ile pale chuo kikuu cha Dar? Hata maprofesa wetu ukisoma taarifa zao utashangaa sana kwani wanatumia maneno magumu ambayo hata wenye lugha yao ni nadra kuyatumia...
 
Press conference yake imeeleweka vizuri tu wala hakuna mwandishi wa habari aliyelalamika kuwa hajaelewa kilichosemwa.

Na ujumbe alioutoa ndiyo huyo ambayo kila mmoja ameusikia au kuusoma kupitia media mbalimbali.

Labda kama una lako binafsi dhidi ya huyu jamaa.

Hao waandishi wa habari unaowasema Kiswahili hawajui. Sasa watalalamikaje?
 
Mtaumia sana. Wanje alipokuwa mbunge alikuwa Kiswahili fasaha kabisa!!

Nani umemuona anamsifia Wenje hapa? Kwanza huko bungeni ndio upuuzi mtupu. Kila abatesimama ndio anajifanya ana elimu ile mbaya, sijui ni nani aliyewaambia usomi ni kuchomeka maneno ya kiingereza katikati ya kiswahili.
 
wewe jamaa utakuwa na wivu aisee. hivi kuna mtu hataelewa kile alichosema TR? mbona alikuwa akikisema kwa kiswahili na Kiingereza? labda kama hoja yako ni nje ya lugha hiyo.
 
Mod edit:kichwa cha habari kisomeke hivi:
Msajili wa Hazina Ndg. Lawrence Mafuru hajui au kashasahau lugha ya Taifa (Kiswahili) ?

Nimesikiliza na nimetazama video za huyu Msajili wa Hazina wakati anatoa taarifa kwa umma juu ya hali ya mzunguko wa fedha nchini ambao unaleta mtafaruku mkubwa ndani ya hii nchi ya watu zaidi ya milioni 50 na ninasikitika kusema kuwa huyu ndugu pamoja na jitihada zake za kutaka kutujuza sisi wananchi kuhusu hii kadhia ya ya fedha lakini mfano mbovu sana wa viongozi wetu.

Inawezekana vipi kuwa mtu mwenye dhamana kubwa kama Lawrence Mafuru aitishe mkutano na vymbo vya habari halafu anatumia zaidi ya asilimia 90 ya maneno yake kuongea maneno mengi ya Kiingreza kilichojaa misamiati migumu ya kiingereza ambacho Mtanzania wa kawaida hawezi kumuelewa? Naamini kabisa kuwa Mafuru nia yake haikuwa kutujuza yanayoendelea bali ni kutughilibu na maneno mengi ya kiingereza ambayo hayaeleweki.

Hili tatizo nimeliona sana kwa viongozi wetu wakiwepo Bungeni, wakiongea kwenye runinga au radio na mbaya zaidi mpaka miswada na sheria zetu nayo inaandikwa kwa kiingereza ambacho asilimia kubwa ya watanzania hawaelewi na inafanana sana mikataba mibovu ya kilaghai ya wakoloni.

Nikirudi kwa huyu Ndugu Lawrence Mafuru, je hajui kuongea Kiswahili fasaha cha kueleweka au mbwembwe ya kutaka kutuvuruga na kutughilibu tusielewe haya mambo nyeti ya kitaifa?

Wito kama tumefikia hatua ya kuwapa madaraka wasiojua lugha ya Taifa bas serikali iajiri watu kutoka BAKITA kwenye kila idaya ya serikali ili mawasiliano awe mopes kwa na wananchi

Na kama imeshindikana naomba Ndugu Magufuli toa agizo kuwa hawa watu wa serikali waongee kwa kikswahili ili wananchi wapate kuwaelewa na wasiojua Kiswahili wapelekwe kwenye kozi maalum ya kujua hii lugha ya Taifa (kwa gharama zao)

Ushahidi wa ghilba ya Lawrence Mafuru huu hapa:


Acha kulalamika hovyo, kama hujui omba msaada ili usaidiwe.
Labda alitaka kumficha "on behalf of myself".........

Kwa baadhi ya mambo baada ya kugundua ni mweupe kwa kimalikia.........
 
Mkuu ebu mpe mifano ya maneno
Liquidity na suffocation kama lugha ya kibenki kwa Kiswahili.
Kijana kajieleza vizuri sana bila maringo kama hawa tunaowasikia kila siku kwenye Radio na kuwaona kwenye TV. Watu STD Seven ukiwasikia wanavyochanganya lugha utapatwa kichefu chefu ila huyu kaeelezea vizuri kwa kutulia ila kuna Jargon ambazo ni za kibiashara na huwezi kuzitranslate lazima aseme kwa lugha ya mama.
 
Hayo ni mambo ya kitaalamu, kaeleza kutokana na taaluma yake aliyochukua muda mwingi na garama kusoma... sasa yule ambaye wakati anaenda shule yeye ndio anavuta shuka kumrithisha bwana usingizi amsaidieje?

garama - gharama
 
Mkuu ulivyo ripoti hapo juu umekuza sana tofauti kabisa na ukweli. Inatokeaga lakini, kuchukizwa tu na mtu anavyoongea au alivyo au anavyoonekana.
 
Nani alikwambia ukimbie umande? :D:D:D By the way, kiswahili hakina misamiati ya kutosheleza kuelezea hayo mambo ya kitaalam aliyokuwa anayazungumzia.
Mfano neno 'liquidity' kwa kiswahili ni 'maji maji' kwa hiyo kama angezungumza kwa Kiswahili lugha ya taifa angesema kuwa
'benki nyingi zina kosa hewa (suffocate) kwa kuwa hazina maji maji ya kutosha, kitu ambacho kwa Mbongo wa kawaida angesema kuwa kama benki zinakosa hewa kwa kuwa hazina maji maji ya kutosha, si waende DAWASCO? :(:(:(
aaisee.. Wewe ushaifunga hii thread.. Asante kwa kuniondolea stress
 
Back
Top Bottom