Msajili Tafadhali Bwana! Uliisoma Barua ya Lipumba Kujiuzulu?

Kuna mambo mengine yanapotokea inabidi uhoji kama akili zimezidi akili au ni kitu gani tena. Hivi kweli Msajili na wale wote ambao wanakubali Lipumba kurudia cheo chake ni kwamba hawajali kabisa kuwa maneno yana nguvu na maana? Lipumba ni miongoni mwa viongozi wabovu waliowahi kutokea - namuweka kundi moja na yule fulani - na ubovu huo naweza kusema sasa umekamilika.

Mtu mzima unaposimama kuchukua msimamo na ukamaanisha kuuchukua msimamo huo ni lazima uwe na ujasiri (nilitaka kutumia lile neno la Kiingereza lenye maana ya mipira) wa kuisimamia. Hii ni kweli hasa kama msimamo huo una matokeo ya kitaifa kabisa.

Ati kwamba Lipumba aliandika barua ya kutengua barua ya kujiuzulu na hivyo basi barua ile ya kujiuzulu haikuwa na nguvu tena! Sijui ni genius gani huyo anayetaka watu wakubali uongo kuwa ni kweli. Barua ya Lipumba kujiuzulu iliweka ni siku gani kujiuzulu huko kunaanza, haikusema kunasubiria sijui maamuzi ya chombo gani kingine. Angalau hivi ndivyo ambavyo nimeweza kuamini baada ya kusoma 'ushauri, maoni na maagizo' ya Msajili wa Vyama vya Siasa.

Sasa kama Lipumba alimaanisha uamuzi wake ule, na akaweka manyanga chini, barua yake ya "kutengua" ilikuwa ikiwa imechelewa. Mtu mwenye utimamu wa akili hawezi kutengua barua ya kujiuzulu wakati alisha effect kujiuzulu huko. Barua yake ya kujiuzulu ingekuwa inasubiri maamuzi kama Lipumba angeendelea kubakia ofisini na kufanya kazi zake kama kawaida akisubiria "chombo" kingine kuridhia uamuzi wake.

Kama Mwenyekiti wa Taifa wa chama alijua kwa hakika kabisa kuwa muda wa kikao hicho cha chama haukuwepo na asingeweza kusubiri na akaamua kuachilia ngazi na hivyo kueffect kujiuzulu kwake. Sasa baada ya kuongoka hawezi kuandika kutengua barua ya kitu ambacho tayari kimefanyika.

Mtu anapofunga ndoa na akapewa zile baraka za mwisho na kutangazwa ni "mume na mke" hawezi kugeuka na kusema anataka kutengua uchumba! Uchumba ulishapita ipo ndoa. Lipumba alipojiuzulu alijiuzulu in fact siyo kwa kumsingizia. Sijui msajili aliwahi kuona precedence ya wapi ya mtu kutengua kujiuzulu kwake nafasi yake baada ya kuiacha hiyo nafasi na kwenda kwenye shughuli nyingine!

Baraza Kuu lingeweza kumrudisha Lipumba kama lingetaka kwa kusema kuwa halikuridhia; lakini ukimya wake ni kuridhia tosha kwa sababu Lipumba alishaondoka na kukiachilia kiti cha Uenyekiti. Sasa unamrudisha vipi kwa kusema ati "alitengua". Ina maana hakuuacha uenyekiti wakati sote tulishuhudia kwa maneno yake (alipozungumza na waandishi wa habari) na alipohojiwa akiwa Kigali kuwa ameondoka Uenyekiti tuliingiwa na viwavi jeshi kwenye akili zetu kuwa hatukumuelewa?

Msajili tafadhali bana!

TAHARIRI YA ZAMAMPYA
Silence does not constitute acceptance na ipo case law on that.
 
Sheria ni msumeno,Kosa alilofanya sefu ni kushindwa kuthibitisha kujiuzulu kwa Lipumba haraka iwezekanavyo
Wajanja wametumia loophole kurudi tena na ndio katiba yao inavyotaka hata uandike barua,useme umejiuzulu leo huku tena ukiwa uchi kusisitiza,katiba ya cuf inataka mamlaka iliokuteua ithibitishe hilo tena kwa kura
Sefu kachelewa kufanya hilo,alikuwa bize na urais wa Zanzibar
Mkuu barua ya lipumba haikuwa ya kusudio la kujiuzulu, na alijiuzulu kweli kwa kukabidhi ofisi. Madai ya kurudi ofisini ni ujinga unao eleweka na jamii za akina lipumba.
 
Lakin ule mkutano wa CUF uliovunjika.kabla ya kuvunjika ulipitisha kukubali kujiudhuru kwa lipumba
Unazungumzia mkutano ambao umekuwa ruled kuwa ulikuwa batili? kwa kuitishwa bila kuruhusu wajumbe halali kuwepo na kuwepo kwa wajumbe bandia
 
"unapokosa macho ya kutizamia,tumia masikio kusikia..ukikosa macho wala masikio,tumia mdomo kunena yaliyo ya busara utakomboka"..poor prof.amekosa vyote,anatumia ngozi na pua kwa matumizi yasiyo sahihi..
 
mkuu MM,naona umeanza kuwa yule MM tuliaemfaham miaka 2 iliyopita..hongera nawe kwa kuziona sarakasi hizi za hawa vihiyo.
 
majaji Uchwara, Imagine ni watu wangapi wamedhurika na hukumu za jaji huyu katika proceedings za kimahakama???
 
Sababu kubwa ya yeye kujiondoa cuf wakati ule hakua tayari kumpigia debe mh Lowassa katika nafasi ya Urais uchaguzi umeshaisha na Mh Lowassa ameshashindwa na yeye sasa analudi kwenye nafasi yake iliyokuwa wazi kwa muda wote yeye alipokuwa hayupo madarakani
Lowassa kwani kashaondoka ukawa?
 
Kama unakumbuka hotuba ya Mwalimu Nyerere akielezea namna waziri mmoja wa Uingereza aliyekuwa na kashfa ya kuchepuka na binti wa mtaani hungeandika haya. Mwalimu alisema waziri yule alipoandika barua ya kujiuzulu PM wa wakati ule hata hakumjibu bali aliteua mwingine nafasi hiyo. Mbona yule waziri baada ya mwaka hakurudi kuvunja ofisi kuwa yeye bado waziri kwa vile barua yake haikujibiwa?
Mtu mzima anageuka kitandani tuu sio kauli na maamuzi yake. Pro-pesa asituletee utoto hapa.
Rufaa ya waziri ni kwa Raisi...hawezi kwenda popote.
 
Nilivyosoma barua ya Msajili wa vyama vya siasa,nilimuambia mtoto wangu asome kwa bidii lakini asijekufanya kazi serikalini. Uko watu wanajitoa ufahamu na kufanya mambo ya aibu nje ya taaluma zao.
Leo hii Jaji kabisa anashindwa kuelewa barua ya kujiuzulu yenye tarehe na siku?
Nilisikitiswa sana na uyo msajili.

Mwanangu alikuwa na ndoto za kusoma sheria. Lakini baada ya kusoma ULE UPUUZI WA BARUA YA MSAJILI basi nilimpa angalizo. Asee mwanangu ni bora awe mwanasayansi kama Magufuli kuliko kusomea sheria.
 
Mwanangu alikuwa na ndoto za kusoma sheria. Lakini baada ya kusoma ULE UPUUZI WA BARUA YA MSAJILI basi nilimpa angalizo. Asee mwanangu ni bora awe mwanasayansi kama Magufuli kuliko kusomea sheria.

Asome sheria lakini asiajiriwe serikalini. Uko watu wanaweka taaluma pembeni na kuwa makapuku.
 
Kama unakumbuka hotuba ya Mwalimu Nyerere akielezea namna waziri mmoja wa Uingereza aliyekuwa na kashfa ya kuchepuka na binti wa mtaani hungeandika haya. Mwalimu alisema waziri yule alipoandika barua ya kujiuzulu PM wa wakati ule hata hakumjibu bali aliteua mwingine nafasi hiyo. Mbona yule waziri baada ya mwaka hakurudi kuvunja ofisi kuwa yeye bado waziri kwa vile barua yake haikujibiwa?
Mtu mzima anageuka kitandani tuu sio kauli na maamuzi yake. Pro-pesa asituletee utoto hapa.
Hii quote ya mwisho wa reli...inatumika sana kule
 
Ila ujiulize pia je kamati kuu ya cuf ilikaa na kuijadili na kisha kuikubali kuwa wameridhia lipumba kujiuzulu kwa mujibu wa taratibu? Usishike unapotaka tu, shika pia isipotaka ili uzi wako uwe impartial.

MM ni moja kati ya vichwa makini,naomba kuhoji unaelewa toroka uje? Ukipanda bangi uanvuna bangi.CUF wanavuna walichopanda subiri wakubwa zao.
 
Mkuu barua ya lipumba haikuwa ya kusudio la kujiuzulu, na alijiuzulu kweli kwa kukabidhi ofisi. Madai ya kurudi ofisini ni ujinga unao eleweka na jamii za akina lipumba.
Leo nimemsikiliza makamu wa msajili wa vyama vya siasa, kasema lipumba aliwasilisha batua ya kujiuzulu na Seif anajua hilo.
 
Back
Top Bottom