Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,144
Msaidizi wa Nchimbi ajiengua adai amedhalilishwa
Na Musa Juma, Tarime
JINAMIZI la tuhuma za ufisadi alizoibua mjumbe wa Halmasharui Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), Nape Nnauye ndani ya Umoja wa Vijana (UVCCM) linazidi kuitafuna jumuiya hiyo baada ya aliyekuwa katibu wake mkoa wa Tanga, Mwita Waitara, kutangaza kujiuzulu uongozi.
Waitara aliwaambia waandishi wa habari jana kwenye hoteli ya G-five mjini hapa kuwa hatua hiyo imelenga kupinga uamuzi wa mwenyekiti wa UV-CCM, Dk. Emmanuel Nchimbi kumhamishia makao makuu ya jumuiya hiyo kuwa karani wake.
Alisema uhamisho huo sio wa heri bali unalenga kumdhalilisha kutokana na kupinga agizo la uongozi wa jumuiya hiyo makao makuu lililomtaka awaombe radhi watuhumiwa wa ufisadi baada ya kamati ya utekelezaji ya UVCCM mkoa wa Tanga kutoa tamko la kutaka wawajibishwe.
Nchimbi anataka kunidhalilisha kutokana na msimamo wangu wa kupinga mafisadi na kumuunga mkono Nape Nnauye na sitarudi nyuma na sitaenda makao makuu Dar es Salaam UV-CCM labda nikiwa nimekufa, aliapa Waitara.
Waitara alieleza kuwa ameamua kukataa kuomba kuwaomba radhi watuhumiwa hao wa ufisadi kwa kuwa anaamini tamko lililotolewa na kamati hiyo lilikuwa halali na sio batili.
"Kama tamko hilo lilikuwa baya waliopaswa kuomba radhi ni kamati ya utekelezaji mkoa na mimi," alieleza na kubainisha:
"Wakati mimi wananifanyia haya, mwenyekiti wa UV-CCM mkoa wa Tanga ambaye pia ni katibu mwenezi wa mkoa, Emmanuel Kiondo, ambaye hata katika kikao cha Baraza Kuu la Taifa alimuunga mkono Nape, wameshindwa kumgusa."
Waitara alitaja sababu nyingine za kukataa kwenda kuwa karani wa Dk. Nchimbi ni nafasi hiyo kutokuwa ya kikatiba na kwamba elimu yake ni kubwa kuliko makatibu wengi wa jumuiya hiyo.
"Mimi ni msomi na nina shahada. Makatibu wenye elimu ya aina hiyo ndani ya UVCCM ni wawili, siwezi kwenda kuwa karani lakini pia nafasi hiyo haipo kikatiba," alieleza.
Alisema aliamua kujiunga na UV-CCM mara baada ya kumaliza Chuo Kikuu cha Dar es Saalam na kutunukiwa shahada ya Ualimu wa Sayansi ili kujiendeleza kisiasa na si kwenda kuwa karani.
Alidai kuwa kitendo cha kuitwa makao makuu ya UV-CCM ni hila ya Dk. Nchimbi kutaka kumfukuza kwa aibu kwenye jumuiya hiyo kama alivyofanya kwa Nape Nnauye, ambaye alivuliwa uanachama na Baraza Kuu kwa madai kuwa alisema uongozi wakati alipotuhumu kuwa mkataba wa uwekezaji wa jengo la makao makuu ya UV-CCM haukupitishwa na vikao halali.
Hawa wanataka kunifukuza, nimegundua hilo na Dar es Salaam siendi... mimi ni msomi na nina msimamo... elimu yangu na uwezo wangu sio mtu wa kukaa kama karani na kusambaza chai kwenye vikao wakati kuna makatibu lukuki wenye elimu ya kidato cha nne tu na shule ya msingi, alisema Waitara.
Waitara, ambaye alikuwa rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam (Daruso), anapinga kushushwa cheo akisema wakati wote wa utendaji wake hajawahi kufanya kosa lolote na kuandikiwa barua yoyote ya kuonywa na umoja huo.
"Baada ya kujiunga na UV-CCM ilikuwa niwe katibu wa mkoa wa Dar es salaam, lakini kutokana na Nchimbi kunipiga vita ndio walinipeleka Tanga. Lakini sikupinga na nilifanya kazi kwa nguvu zangu zote," alisema Waitara.
Waitara alibainisha kuwa ataendelea kupinga mradi wa Jengo la Umoja wa Vijana na anapinga kamati ya kuchunguza mradi huo tata kuongozwa na Andrew Chenge, ambaye anatajwa kwenye kashfa ya ununuzi wa rada, na mwenyekiti wa bodi ya wadhamini wa umoja huo, Edward Lowassa, ambaye alijiuzulu wadhifa wake wa Waziri Mkuu kutokana na kuhusishwa kwenye kashfa ya utoaji zabuni kwa kampuni ya ufuaji umeme wa dharura ya Richmond.
Alisema anashangaa hivi sasa, badala ya viongozi wa umoja huo kujitokeza katika kampeni za ubunge hapa Tarime, wanajishughulisha na upangaji wa safu za viongozi kwenye uchaguzi ujao.
Na Musa Juma, Tarime
JINAMIZI la tuhuma za ufisadi alizoibua mjumbe wa Halmasharui Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), Nape Nnauye ndani ya Umoja wa Vijana (UVCCM) linazidi kuitafuna jumuiya hiyo baada ya aliyekuwa katibu wake mkoa wa Tanga, Mwita Waitara, kutangaza kujiuzulu uongozi.
Waitara aliwaambia waandishi wa habari jana kwenye hoteli ya G-five mjini hapa kuwa hatua hiyo imelenga kupinga uamuzi wa mwenyekiti wa UV-CCM, Dk. Emmanuel Nchimbi kumhamishia makao makuu ya jumuiya hiyo kuwa karani wake.
Alisema uhamisho huo sio wa heri bali unalenga kumdhalilisha kutokana na kupinga agizo la uongozi wa jumuiya hiyo makao makuu lililomtaka awaombe radhi watuhumiwa wa ufisadi baada ya kamati ya utekelezaji ya UVCCM mkoa wa Tanga kutoa tamko la kutaka wawajibishwe.
Nchimbi anataka kunidhalilisha kutokana na msimamo wangu wa kupinga mafisadi na kumuunga mkono Nape Nnauye na sitarudi nyuma na sitaenda makao makuu Dar es Salaam UV-CCM labda nikiwa nimekufa, aliapa Waitara.
Waitara alieleza kuwa ameamua kukataa kuomba kuwaomba radhi watuhumiwa hao wa ufisadi kwa kuwa anaamini tamko lililotolewa na kamati hiyo lilikuwa halali na sio batili.
"Kama tamko hilo lilikuwa baya waliopaswa kuomba radhi ni kamati ya utekelezaji mkoa na mimi," alieleza na kubainisha:
"Wakati mimi wananifanyia haya, mwenyekiti wa UV-CCM mkoa wa Tanga ambaye pia ni katibu mwenezi wa mkoa, Emmanuel Kiondo, ambaye hata katika kikao cha Baraza Kuu la Taifa alimuunga mkono Nape, wameshindwa kumgusa."
Waitara alitaja sababu nyingine za kukataa kwenda kuwa karani wa Dk. Nchimbi ni nafasi hiyo kutokuwa ya kikatiba na kwamba elimu yake ni kubwa kuliko makatibu wengi wa jumuiya hiyo.
"Mimi ni msomi na nina shahada. Makatibu wenye elimu ya aina hiyo ndani ya UVCCM ni wawili, siwezi kwenda kuwa karani lakini pia nafasi hiyo haipo kikatiba," alieleza.
Alisema aliamua kujiunga na UV-CCM mara baada ya kumaliza Chuo Kikuu cha Dar es Saalam na kutunukiwa shahada ya Ualimu wa Sayansi ili kujiendeleza kisiasa na si kwenda kuwa karani.
Alidai kuwa kitendo cha kuitwa makao makuu ya UV-CCM ni hila ya Dk. Nchimbi kutaka kumfukuza kwa aibu kwenye jumuiya hiyo kama alivyofanya kwa Nape Nnauye, ambaye alivuliwa uanachama na Baraza Kuu kwa madai kuwa alisema uongozi wakati alipotuhumu kuwa mkataba wa uwekezaji wa jengo la makao makuu ya UV-CCM haukupitishwa na vikao halali.
Hawa wanataka kunifukuza, nimegundua hilo na Dar es Salaam siendi... mimi ni msomi na nina msimamo... elimu yangu na uwezo wangu sio mtu wa kukaa kama karani na kusambaza chai kwenye vikao wakati kuna makatibu lukuki wenye elimu ya kidato cha nne tu na shule ya msingi, alisema Waitara.
Waitara, ambaye alikuwa rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam (Daruso), anapinga kushushwa cheo akisema wakati wote wa utendaji wake hajawahi kufanya kosa lolote na kuandikiwa barua yoyote ya kuonywa na umoja huo.
"Baada ya kujiunga na UV-CCM ilikuwa niwe katibu wa mkoa wa Dar es salaam, lakini kutokana na Nchimbi kunipiga vita ndio walinipeleka Tanga. Lakini sikupinga na nilifanya kazi kwa nguvu zangu zote," alisema Waitara.
Waitara alibainisha kuwa ataendelea kupinga mradi wa Jengo la Umoja wa Vijana na anapinga kamati ya kuchunguza mradi huo tata kuongozwa na Andrew Chenge, ambaye anatajwa kwenye kashfa ya ununuzi wa rada, na mwenyekiti wa bodi ya wadhamini wa umoja huo, Edward Lowassa, ambaye alijiuzulu wadhifa wake wa Waziri Mkuu kutokana na kuhusishwa kwenye kashfa ya utoaji zabuni kwa kampuni ya ufuaji umeme wa dharura ya Richmond.
Alisema anashangaa hivi sasa, badala ya viongozi wa umoja huo kujitokeza katika kampeni za ubunge hapa Tarime, wanajishughulisha na upangaji wa safu za viongozi kwenye uchaguzi ujao.