MCHUMA MBOGA
Member
- Mar 29, 2012
- 18
- 10
Katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo 30.03.2012 kuanzia saa kumi jioni huko uwanja wa michezo Patandi Arumeru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa magamba kama vile Mkapa, Lowassa, Wasira, Nnape, Sophia Simba, Katibu Mkuu wa magamba Mukama wabunge mbalimbali bila kumsahau mgombea wao Siyoi Sumari na kumalizika saa kumi na moja kamili jioni.
Watu waliojitokeza ni wakina mama wachache na watoto kadhaa na vijana wa green guards ambao idadi yao karibu ililingana na idadi ya watu kutoka vyombo vya ulinzi na usalama ambao leo walikuwa wengi sana kuliko kawaida.
Baada ya kumaliza mkutano wao magamba wakitumia magari MENGI ya kifahari ya TOYOTA LAND CRUISER GX V8 waliondoka na kutimua vumbi wakielekea Usa River na walipofika kwenye makutano ya barabara ya kwenda Moshi - Arusha ndipo balaa lilipowakuta kwani walikutana na kundi kubwa la watu ambao idadi yao ni karibu mara tatu ya wale waliokuwa kwenye mkutano wa kampeni hapo Patandi na kuanza kuwazomea kwa kuwaita mafisadi na kuwaonyesha alama ya "V".
Walipoona hivyo msafara wa mgamba ukaongeza spidi na kutokomea kuelekea Usa River.
Source: Nilikuwepo pale in person.
Watu waliojitokeza ni wakina mama wachache na watoto kadhaa na vijana wa green guards ambao idadi yao karibu ililingana na idadi ya watu kutoka vyombo vya ulinzi na usalama ambao leo walikuwa wengi sana kuliko kawaida.
Baada ya kumaliza mkutano wao magamba wakitumia magari MENGI ya kifahari ya TOYOTA LAND CRUISER GX V8 waliondoka na kutimua vumbi wakielekea Usa River na walipofika kwenye makutano ya barabara ya kwenda Moshi - Arusha ndipo balaa lilipowakuta kwani walikutana na kundi kubwa la watu ambao idadi yao ni karibu mara tatu ya wale waliokuwa kwenye mkutano wa kampeni hapo Patandi na kuanza kuwazomea kwa kuwaita mafisadi na kuwaonyesha alama ya "V".
Walipoona hivyo msafara wa mgamba ukaongeza spidi na kutokomea kuelekea Usa River.
Source: Nilikuwepo pale in person.