Msafara wa Makamba wamwagiwa mchanga FFU waingilia-Singida

Lunyungu

JF-Expert Member
Aug 7, 2006
8,873
1,894
Makamba na Tambwe na wapambe wao majuzi walipata adha na adhabu toka kwa wananchi wa Singida kwa kuitwa waongo na kumwagiwa mchanga wakati wanaondoka toka maeneo ya mikutano yao. Hivi karibuni Tambwe na Makamba na CCM nzima wamekuwa wakihaha kila kona ya Nchi kujaribu kuzima sumu iliyo mwagwa kwa wananchi juu ya kuibiwa mali zao .

Walikuwa wakiondoka ambapo wananchi walisema mnatudanganya maisha ni magumu na hatuwataki wakaanza kuwamwagia mchanga ndipo FFU walipofika na kuokoa jahazi hilo. Katika kutapata kwa CCM wamekuwa wakifanya mabadiliko kwa kuwahamisha makatibu wao wa Chama ambao ni wasemaji sana na kuwapeleka maeneo ambayo CCM ina wakati mgumu ikiwamo Pwani ambako Katibu wao Sofia Kishindo kahamishiwa hapo toka Mbarari. Pwanim imekuwa moto baada ya wazazi na vijana kuhoji uhalali wa wao kukosa Elimu na kuuza vitu vidogo vidgo na kuishia katika kuwa madereva na utingo wa magari .
CCM inahaha baada ya kugundua kwamba sasa watu wamechoka na wanaelewa vya kutosha .
 
Natumaini kutakuwa na mabadiriko katika safu ya uongozi ccm ili kuleta maendeleo ndani ya chama hadi ndani ya serikali !
 
Lunyungu ukowapi siku hizi? nnaona unatuletea data on the spot.

nnaamini wananchi wanaanza kuchoka kuchezewa na wana siasa.

kuna nchi moja nilikaa wanafunzi wa kitz wakawa wanapasiana mwana dada wa nchi hiyo,mara leo jamaa unajidai kafa akitimiza malengo anachubua, anazuka mwengine na gia nzuri tu na yeye akijiset anachubua, aliposhtuka mwana dada akawachukia maforeigner wote.

sasa wananchi si ccm tu kama wengi wanavyotaka ifahamike bali vyama vyote sasa wanazomewa.

na jukumu la maendeleo ni letu sote vyama vyote si kazi utongozaji tu tukipata tunawasanifu basi. pemba kuna cuf nn wamefanya? au ukiwa huna serikali hata kisima huwezi kuwachimbia? chadema nn wamefanya?

sasa tuwaambie ukweli tuchapeni kazi na tukubali makosa yetu. tukae pamoja kubuni tutoke vp, sio kufitinishana kwa wananchi
 
Lunyungu ukowapi siku hizi? nnaona unatuletea data on the spot.

nnaamini wananchi wanaanza kuchoka kuchezewa na wana siasa.

kuna nchi moja nilikaa wanafunzi wa kitz wakawa wanapasiana mwana dada wa nchi hiyo,mara leo jamaa unajidai kafa akitimiza malengo anachubua, anazuka mwengine na gia nzuri tu na yeye akijiset anachubua, aliposhtuka mwana dada akawachukia maforeigner wote.

sasa wananchi si ccm tu kama wengi wanavyotaka ifahamike bali vyama vyote sasa wanazomewa.

na jukumu la maendeleo ni letu sote vyama vyote si kazi utongozaji tu tukipata tunawasanifu basi. pemba kuna cuf nn wamefanya? au ukiwa huna serikali hata kisima huwezi kuwachimbia? chadema nn wamefanya?

sasa tuwaambie ukweli tuchapeni kazi na tukubali makosa yetu. tukae pamoja kubuni tutoke vp, sio kufitinishana kwa wananchi

tukiwa na watu wengine 5 hapa JF naamini tutapiga hatua 10 mbele zaidi ya hapa tulipo !
 
Na baada ya kuzomewa, zitafuata ajali.

Mawaziri wa ccm wameanza kuogopa hizi za safari za kwenda mikoani kutetea wizi na ufisadi. Makamba afadhali urudi Lumumba utulie. Wenzako wanakumbana na hasira ya MUNGU huko mikoani!
 
Tatizo ni kwamba ikishaingia ktk mioyo ya wananchi kuwa chama hakifai na ikaonekana wazi kwamba balaa loote la ugumu wa maisha linasababishwa na viongozi ambao wanakumbatiwa na chama basi ujue mwisho wa chama hiko kupata ridhaa ya wananchi hauko mbali sana.

Ikiwa viongozi wetu hawa hawa ambao walisomeshwa bure kwa kodi za baba zetu tena bure na kupatiwa kazi bila zengwe halafu leo wanabadili kila kitu kana kwamba kuna wateule wachache ambao watasomeshwa kwa mikopo basi mjue kwamba nchi haiko mbali saana na kuuzwa.

ikiwa viongozi wetu wooote walioko madarakani sasa wanaridhia na kulichangamkia vilivyo azimio la zanzibar basi mjue kuwa uozo unaoliua taifa hautatibika kamwe labda kwa kukubaliana kutokubaliana. au kukabiliana

ikiwa viongozi wetu haswa wabunge ambao wanakazania kugombea kwao walikozaliwa au asili ya kabila zao basi mjue kuwa ukabila unabisha hodi kwa kasi ya ajabu.

Ikiwa viongozi wa kitaifa wanatoa kipaumbele kikubwa ktk dhifa au matukio ya kidini nchini basi mjue kuwa great divide i-mlangoni.

Ukiona serikali inatumia mawaziri kukabiliana na upinzani ktk hoja na badala ya kuwchia ma Rc na Dc's basi mjue serikali haijui wajibu wake wa utendaji bora.

ukiona makada wa upinzani wanapokelewa mikono miwili na ccm na kupewa nafasi nyeti basi mtambue kuwa ccm imeishiwa viongozi hivyo wananunua viongozi kutoka upinzani.

Hivyo basi sishangai sana wala sitamwonea huruma mzee wangu makamba na ujumbe wake kwani tunayoyaona siyo wanayotuhubiria. Wana tudanganya mchana kweupeee.

Maisha bora hayaji kwa ubingwa wa kukusanya kodi, yatakuja kwa kuwapatia fursa walipa kodi kwa kuondoa urasimu na kuwajali zaidi ili waweze kuchangia vizuri shibe za viongozi wetu.

I hate politics
 
Hii "sera" ya kuzomea na kumwagia mchanga inafanyakazi wakifanyiwa CCM tu wakifanyiwa wapinzani tunaambiwa kuna watu wametumwa na wanalipwa na CCM.

Mwaka huu kazi kweli kweli...
 
Hii "sera" ya kuzomea na kumwagia mchanga inafanyakazi wakifanyiwa CCM tu wakifanyiwa wapinzani tunaambiwa kuna watu wametumwa na wanalipwa na CCM.

Mwaka huu kazi kweli kweli
...

hehee,kumbe umeona hilo mkuu ! si hata JK alipoenda kupokelewa watu wakasema watu wale wamekodishwa !
 
Natumaini kutakuwa na mabadiriko katika safu ya uongozi ccm ili kuleta maendeleo ndani ya chama hadi ndani ya serikali !

Kada, safari bado ni ndefu. Tuna kazi sana ktk kubadili watu kama Makamba na Tambwe.
Tukaze buti.
 
Hii "sera" ya kuzomea na kumwagia mchanga inafanyakazi wakifanyiwa CCM tu wakifanyiwa wapinzani tunaambiwa kuna watu wametumwa na wanalipwa na CCM.

Mwaka huu kazi kweli kweli...

Lakini nani ana uhakika na uanachama wa hawa waliomwaga mchanga? Huenda wakwa ni Wabongo wasio na vyama.
 
Na baada ya kuzomewa, zitafuata ajali.

Mawaziri wa ccm wameanza kuogopa hizi za safari za kwenda mikoani kutetea wizi na ufisadi. Makamba afadhali urudi Lumumba utulie. Wenzako wanakumbana na hasira ya MUNGU huko mikoani!

..eeh!dada,mswalie mtume!

..hayo ni mapenzi ya allah na si hasira zake!

..kama ni hasira,zitakuwa za bin adam na si za allah!

..asaalam aleykhum!
 
Ama kweli ukipenda kupita kiasi inakuwa balaa hata kipofu unaita chongo mimi siamini kama pamoja na ufisadi woooote huo ambao unaojulikana ndani na nje ya Tz bado kuna watu wanamkumbatia JK na chama chake
 
JK na chama chake

..JK hana chama chake na hata kuwanacho!

..ccm aliikuta,na ataiacha,na wengine wataendelea nayo!

..watanzania tutaendelea kuwapo hata kama ccm,chadema,cuf,nccr,tlp,n.k....vitakufa!au kupotea!

..kama kuna mtu alipaswa kusemwa kwamba ccm ni yake[zidumu fikra za mwenyekiti!] ni kambarage[rip],lakini hii leo yuko wapi?
 
..JK hana chama chake na hata kuwanacho!

..ccm aliikuta,na ataiacha,na wengine wataendelea nayo!

..watanzania tutaendelea kuwapo hata kama ccm,chadema,cuf,nccr,tlp,n.k....vitakufa!au kupotea!

..kama kuna mtu alipaswa kusemwa kwamba ccm ni yake[zidumu fikra za mwenyekiti!] ni kambarage[rip],lakini hii leo yuko wapi
?

natamani haya maneno yako makini yangewekwa kwenye sticky ! lakini huko vya wa Mchimbawima havikai !

Huu ndio ujumbe ninaojaribu kuufikisha lakini watu wapi ! lakini nawapa muda kuelewa !

ai garantii yu zati huu seidi zati wili neva kam agein !
 
Hongera wananchi wa Singida. Naomba na wananchi wa sehemu zingine za nchi kuigamfano wa MUSOMA, TARIME MANYARA na sasa Singida. Hiyo ndiyo inaitwa Demokrasia ya kweli.Naona fahari kuwa wananchi kwa wananchi kugundua DOMOKAYA. Utamaduni wa kujua kupanga sentensi za kusema umepitwa na wakati. Kila kiongozi atakachosema basi awe na uhakika kuwa kitatekelezwa. Baada ya Hapo Uwajubikaji uanze kufuata mkondo wake. Kiongozi akizomewa basi ajiuzulu. Hafai. waajiri ni wananchi na wamekuzomea unangoja nini Ofisini? Ondoka!!
 
Back
Top Bottom