H-K
Senior Member
- Nov 7, 2014
- 106
- 23
Hii imetokea Jana(17-5-15) mida ya mchana katika wilaya ya Iramba maeneo ya misigiri ambapo watu walikua kwenye msafara wa kwenda kumpokea mkuu wa wilaya ya Iramba kwaajiri ya kufanya mkutano kama mgeni rasmi.
Kijana mmoja aliyetambulika kwa jina la MAULIDI aliyekuwa akiendesha bodaboda kupata ajali kwenye msafara huo kutokana na kuendesha pikipiki hiyo kwa kasi na mbwembwe za kumlaki muheshimiwa, alianguka karibu na daraja na kupoteza uhai papo hapo.
Mwanamke mmoja nae amevunjika mkono na wanaume wawili wamejeruhiwa vibaya wote wakipata ajali ya kuanguka na bodaboda zilizokua kwenye msafara.
Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya kiomboi na majeruhi wamelazwa katika hospitali hiyo.
PICHA za tukio sikufanikiwa kuzipata.
Kijana mmoja aliyetambulika kwa jina la MAULIDI aliyekuwa akiendesha bodaboda kupata ajali kwenye msafara huo kutokana na kuendesha pikipiki hiyo kwa kasi na mbwembwe za kumlaki muheshimiwa, alianguka karibu na daraja na kupoteza uhai papo hapo.
Mwanamke mmoja nae amevunjika mkono na wanaume wawili wamejeruhiwa vibaya wote wakipata ajali ya kuanguka na bodaboda zilizokua kwenye msafara.
Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya kiomboi na majeruhi wamelazwa katika hospitali hiyo.
PICHA za tukio sikufanikiwa kuzipata.