Msaada: Xiaomi redmi a8 inakwama kwama

kid ink tz

JF-Expert Member
Dec 1, 2016
307
320
Habari za muda wakuu,

Nina Xiaomi redmi a8 imeanza kuniletea shida toka jana.

Kuna muda inakuwa ina staki kama sec 5 hivi au inakuwa nzito ku touch.

Haina shida yoyote kwenye kioo.

Naomba msaada wa aliyewahi kukutana na changamoto hii au anayefanamu namna ya kukabiliana nayo tafadhali.
 
Mara nyingi ni Tatizo la storage simu ikifanya hivyo.

Wakati inafanya hivyo unakuwa huja Un install app ama kurun kitu chochote kinachohamisha file kubwa?
 
Aiseee hili tatizo ni shida najaribu Ku clear cache mara Kwa mara na Ku uninstall baadhi ya apps lakini baada ya muda tatizo linarudi pale pale yaani apps hasa Telegraph unakuta yenyewe tu inachukua space hadi ya 4 GB

Na ni apps lazima niwenazo
Mara nyingi ni Tatizo la storage simu ikifanya hivyo.

Wakati inafanya hivyo unakuwa huja Un install app ama kurun kitu chochote kinachohamisha file kubwa?
 
Aiseee hili tatizo ni shida najaribu Ku clear cache mara Kwa mara na Ku uninstall baadhi ya apps lakini baada ya muda tatizo linarudi pale pale yaani apps hasa Telegraph unakuta yenyewe tu inachukua space hadi ya 4 GB

Na ni apps lazima niwenazo
Unamaanisha huko kunata ama app zina chukua space kubwa? Kama ni Tatizo la app kama whatsapp ama telegram kuchukua space kubwa ni kwamba kuna junks kibao ulizotumiwa, ulizotuma, thumbnail etc.

Solution ni kuzifuta mwenyewe manual.

Fungua file manager kisha Tafuta folder la app husika ingia ndani utakuta media vitu kama picha, video, sent images, video etc futa visivyo na maana.
 
Back
Top Bottom