Msaada wenye uelewa juu ya hili swala.

BabaMorgan

JF-Expert Member
Dec 18, 2017
4,041
10,463
Ni hali ambayo sio Mimi tu inanitokea bali wengi wetu. Ni jinsi ya kufanya maamuzi tuseme unajikuta una chaguzi mbili kwa mfano upo kwenye mawazo ya kujenga Nyumba au kununua gari unaweza kuwaza kununua gari ila baada ya muda ukajiona ulifanya maamuzi ya kipuuzi ni heri ujenge nyumba lakini ukikaa tena baada ya muda flani mawazo yanabadilika unawaza kununua gari na hii hali inakuwa aina mwisho unaweza kufanya kimoja wapo na bado ukaendelea kujilaumu kwa nini umefanya kitu flani badala ya kitu kingine. Wataalamu wa elimu ya akili naombeni msaada jinsi ya kukabiliana na hii hali maana madhara yake ni kujikuta ufanyi chochote kwenye muda unaostahili.
 
unajihisi hauna akili?
mimi nahisi haujui tu ukitakacho maishani,kuna siku hata mke uliye nae na watoto utahisi haukutakiwa uwe nao,fanya unachokipenda mkuu,tuna muda mchache sana wa kuishi,unatakiwa uifurahie kila nukta ya uhai uliyopewa,we are not permanent here!
 
Ukiona hivyo ujue hauna vipaumbele katika jambo lako kwa kukuuliza tu kati ya gari na nyumba unapendelea nini?changanua faida za gari na hasara zake,kisha changanua faida na hasara za nyumba ukiona hasara za gari ni chache basi nunua gari na ukiona hasara za nyumba ni chache kuliko za gari basi jenga nyumba mkuu
 
Ni hali ambayo sio Mimi tu inanitokea bali wengi wetu. Ni jinsi ya kufanya maamuzi tuseme unajikuta una chaguzi mbili kwa mfano upo kwenye mawazo ya kujenga Nyumba au kununua gari unaweza kuwaza kununua gari ila baada ya muda ukajiona ulifanya maamuzi ya kipuuzi ni heri ujenge nyumba lakini ukikaa tena baada ya muda flani mawazo yanabadilika unawaza kununua gari na hii hali inakuwa aina mwisho unaweza kufanya kimoja wapo na bado ukaendelea kujilaumu kwa nini umefanya kitu flani badala ya kitu kingine. Wataalamu wa elimu ya akili naombeni msaada jinsi ya kukabiliana na hii hali maana madhara yake ni kujikuta ufanyi chochote kwenye muda unaostahili.
HUNA MSIMAMO MANA YAKE KIMAAMUZI, FANYA MAAMUZI SAHIHI KWA WAKATI SAHIHI..UKIWA UNASITASITA HUTAFANYA CHOCHOTE
 
Ukiona hivyo ujue hauna vipaumbele katika jambo lako kwa kukuuliza tu kati ya gari na nyumba unapendelea nini?changanua faida za gari na hasara zake,kisha changanua faida na hasara za nyumba ukiona hasara za gari ni chache basi nunua gari na ukiona hasara za nyumba ni chache kuliko za gari basi jenga nyumba mkuu
Kwenye gari na Nyumba ni mfano tu ila mambo yapo mengi labda niseme kilichonipelekea kuandika Uzi kuna jamaa kanishauri nianze kutumie kilevi nipo na tafakari kati ya bangi na pombe lipi litakuwa chaguo sahihi.
 
Kwenye gari na Nyumba ni mfano tu ila mambo yapo mengi labda niseme kilichonipelekea kuandika Uzi kuna jamaa kanishauri nianze kutumie kilevi nipo na tafakari kati ya bangi na pombe lipi litakuwa chaguo sahihi.
huku ndo unaingia chaka kabisa...
usijiingize kwenye kilevi chochote..
 
Kwenye gari na Nyumba ni mfano tu ila mambo yapo mengi labda niseme kilichonipelekea kuandika Uzi kuna jamaa kanishauri nianze kutumie kilevi nipo na tafakari kati ya bangi na pombe lipi litakuwa chaguo sahihi.
ukiona hivyo ujue unakaribia kupauka ubongo
 
Ukiona uko hivyo fanya uwe unatembe na coin..kabla ya kuamua unairusha juu kichwa , mwenge...itakayoangukia unachukua hio hio
 
Kwenye gari na Nyumba ni mfano tu ila mambo yapo mengi labda niseme kilichonipelekea kuandika Uzi kuna jamaa kanishauri nianze kutumie kilevi nipo na tafakari kati ya bangi na pombe lipi litakuwa chaguo sahihi.
Daah Aisee
 
idea inaanza kabla ya kushika hela,manake ukishazipata ni kutekeleza idea tu,,ila wewe ukishapata hela ndo idea nyiingi zinakuja..ndo mana hali hiyo inakutokea
 
Kwenye gari na Nyumba ni mfano tu ila mambo yapo mengi labda niseme kilichonipelekea kuandika Uzi kuna jamaa kanishauri nianze kutumie kilevi nipo na tafakari kati ya bangi na pombe lipi litakuwa chaguo sahihi.
vuta bangi upate ukichaa wa kuyaona maendeleo ya Magufuli
 
Back
Top Bottom