Msaada wenu jamani

myhny

Senior Member
May 27, 2014
123
23
Kuna rafiki yangu alifiwa na baba ake toka akiwa standard 2.

Walikuwa wawili tu katika family yeye na mdogo wake mama yao alijitahidi sana kuwalea pasipo na ushirikiano kwa upande wa baba yake wamekuwa sasa wakubwa.

Mmoja akawa kapata mchumba akampeleka kwao huyo mwanaume alikuwa na kazi yake.

Na walipanga baada ya huyo binti kumaliza chuo mwaka wa mwisho waowane ila nyumbani kaishajitambulisha baada ya huo mwaka kuisha yule kaka akawa kaacha kazi kutokana na mambo ya ugomvi kazini sasa ndugu zake upande wa baba hawataki tena yule mwanaume amuoe eti kisa hana kazi.

Kwa mama yake yuko radhi kwa lolote anaomba ushauri
 
...wanapendana?....kama jibu ni ndio......amalize shughuli,,,,kanisani , bomani ama msikitin....
 
Sijaelewa kama upande wa mama wa baba wa yupi? Huyo mwanaume au mke mtarajiwa?
 
Kwan kuoa mpk uwe na kazi?...maisha hayana formula unaemdharau leo hana kazi kesho unakuta kakuacha mbali kimaisha.
 
kupendana wanapendana na wanavumiliana ila kwa mwanamke ndugu wa baba ake ndo hawamtaki kisa hana kazi
 
Hao ndugu wa upande wa baba siku zote walikuwa wapi hadi binti ameshakua sasa ndo wanaingilia bora amsikilize mama yake tu ambae amewalea watoto peke yake
 
Namkumbuka Prof. Mmoja wakati tunakaribia kumaliza kozi mahali akasema "usione ndugu na wanaokuzunguka wanakutazama wakitabasamu, ukafikiri wanafurahia maendeleo yako..hao hawatabasamu ila wanakuonesha kuwa meno yao yapo tayari yanasubiria uwape cha kutafuna pindi umalizapo"Mlipaswa kuelewa hao wanaokataa walitegemea huu ndio wakati wa kupata pata visenti vya mkwe ila kwa kuwa hana kazi wanaona bora wagome angalao aje mwente hela. Usifikiri wanamjali sana huyo binti (yaani wewe) na wanahofia maisha yako ya baadae. Kama ingelikua hivyo wangehusika sana kukulea.Fungua masikio yako usikie ila UAMUZI ni wako wala sio wa mama wala hao wengine..
kupendana wanapendana na wanavumiliana ila kwa mwanamke ndugu wa baba ake ndo hawamtaki kisa hana kazi
 
Nashukuru sana jamani kwa mawazo yenu kuna kitu nimekisoma apo awali nilikuwa sijakijua
 
ikiwa wanapendana jamaa aendelee, ajue hao ndugu hawaolewi anaolewa binti...
 
Kwani vibaya mtu kuniomba ushauri .na mimi nimeleta kwenu ili nipate msaada zaidi sababu hapa kunawatu wamenizidi kimawazo ;umri;
 
Back
Top Bottom