Msaada waungwana anayejua dawa ya meno

KAHIMERIA

JF-Expert Member
Jan 1, 2021
293
351
Anayeijua dawa ya jino /meno mbali na kung'oa anisaidie maana nimeng'oa naona sasa yanaisha

Karibuni..
 
Dawa ya Jino ni kuling'oa tu,

Ulijaribu kufuatilia root cause inayo kusababishia matatizo ya meno? au ulikua una ng'oa tu na kusubiri lingine tena liume nalo ung'oe?
 
Ukiwa unasukutua, usiwahi kutema lile povu la dawa ya meno, lizungushe mdomoni walau kwa dk 5 ndio uje kulitema.

Ukiwa unafanya hivyo, mara mbili au tatu kwa siku niamini mimi itakusaidia sana.
 
Mwez ulioisha lilintesa sana
Limetoboka, kama bahati jamaa nliyekuwa naye ana jamaa yake mtaalam wa miti shamba ikiwemo ya jino

Alintengenezea
Nikawa naweka mdomon dk 15
Baada ya hapo nakaa tena dk 10
Naswaki maisha yanaendelea

Ni asubuh na usiku wakat wa kulala.

Sasa niko flesh
Ila amesisitize niwe natafuna vimigogo flani ivi sjui vinaitwaje
Meno yanakuwa meupe.

Hapo ulipo jaribu kuuliza uliza utapa tu.

Au wewe hujichanganyi vilingeni?
Kama hujichanganyi kitaa itakuwa shida hivi vitu.

Kila la kheri ktk kutatua hiyo shida.
 
Kama linauma au linalegea, chukua limao,kitunguu maji,pili na tangawizi changanya na maji kidogo kisha chuja tumia hayo maji kusukutua mara 2 tu hakuna jino la kung'oa wala halitauma
 
Tafuta mdalasini usage upate unga wake then changanya na Asali mbichi uwe unaweka hapo lilipotoboka baada ya wiki moja leta mrejesho

Sent from my Infinix X606B using JamiiForums mobile app
 
Tafuta mafuta ya habat sauda Kisha chukua pamba safi,ichovye kwenye hayo mafuta then weka hiyo pamba yenye mafuta kwenye jino....nakupa dk 45 tu utasahau hayo maumivu.

Faida nyingine ya haya mafuta ukiyapaka kwenye fizi zilizovimba haipiti dk ishirini utaona zile fizi zimepasuka na utahisi majimaji flan ya chumvi hv mdomoni kuashiria uvimbe umepasuka, hapo maumivu na Hilo jino na fizi kwisha habari yake Yan maumivu yanazima ghafla.

Hii sijaambiwa ila nimethibitisha Mimi mwenyewe.Tafuta hayo mafuta mkuu.
 
Ipo dawa nimetumia mwenyewe nipo poa


meno.jpg
 
Mwez ulioisha lilintesa sana
Limetoboka, kama bahati jamaa nliyekuwa naye ana jamaa yake mtaalam wa miti shamba ikiwemo ya jino....
Kama limetoboka shida huwa linahifadhi mabaki ya chakula na kinywa huwa kinanuka sana bora uende kwa wataalamu uzibwe ndio uendelee na hiyo dawa yako.
 
Tafuta mafuta ya habat sauda Kisha chukua pamba safi,ichovye kwenye hayo mafuta then weka hiyo pamba yenye mafuta kwenye jino....nakupa dk 45 tu utasahau hayo maumivu.Faida nyingine ya haya mafuta ukiyapaka kwenye fizi zilizovimba haipiti dk ishirini utaona zile fizi zimepasuka na utahisi majimaji flan ya chumvi hv mdomoni kuashiria uvimbe umepasuka....hapo maumivu na Hilo jino na fizi kwisha habari yake Yan maumivu yanazima ghafla.Hii sijaambiwa ila nimethibitisha Mimi mwenyewe.Tafuta hayo mafuta mkuu.
Haya mafuta yanapatikana wapi mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom