Msaada - Wapi nawezapata wataalamu wabobezi wa kumfanya mgonjwa wa AIDS anywe dawa?

Natania

JF-Expert Member
Dec 25, 2012
262
217
Habari zenu!

Tafadhali naomba msaada wa ushauri. Nina ndugu yangu (wa kike - miaka 50) ambaye ni mwathirika wa UKIMWI (miaka kama minne sasa toka apime). Shida ni kuwa huwa hataki kunywa dawa. Akiacha kunywa dawa hali yake inakuwa mbaya sana.

In fact huwa anachanganyikiwa kabisa. Tumempeleka hospitali ya wagonjwa wa akili Mirembe -Dodoma karibu mara mbili. Akiwa huko Hospitali ana-recover haraka sababu anakunywa dawa (ARV na zile nyingine za kutibu psychosis) kwa lazima - shida ni kuwa akirudishwa nyumbani (na huwa anarudishwa mapema kabla hata haja-recover vizuri) anakuwa hataki tena kunywa dawa, mkilazimisha anaishia kutoroka!

Kwa sasa amekuwa kama mtu aliyechanganyikiwa - haamini tena kuwa anaumwa ukimwi bali anaamini amerogwa, mara anaamini ni hali ya hewa na anazungumza mambo ambayo hasa unajua amechanganyikiwa.

Kwa wale wanaojua namna nzuri ya kuwasaidia wagonjwa wa aina hii (mbali na kuwapeleka hospitali za rufaa za mikoa ama mirembe) naomba ushauri tafadhali. Kama kuna Hospitali private ambayo ina-specialists (kwa mikoa ya Dar, Moro, ama Dom) wa hali kama hii ya ndugu yangu tafadhali naomba contact zao!

Tafadhali kama una-ushauri mwingine usisite ku-shirikiana nami.

Natanguliza shukrani.
 
Huwa wanachomwa ARV’s ya sindano ina dumu miezi 3, kuna improvements nilisikia nyingine inadumu miezi 18. Hizo mara nyingi hutokewa kwa wasioweza kufuatilia dawa za kila siku.

Nenda nae kwenye kitengo mjue options zilizopo.
Ooh! Shukrani, hii ndiyo naisikia leo! Nitafuatilia! Ubarikiwe Sky Eclat!
 
Habari zenu!

Tafadhali naomba msaada wa ushauri. Nina ndugu yangu (wa kike - miaka 50) ambaye ni mwathirika wa UKIMWI (miaka kama minne sasa toka apime). Shida ni kuwa huwa hataki kunywa dawa. Akiacha kunywa dawa hali yake inakuwa mbaya sana.

In fact huwa anachanganyikiwa kabisa. Tumempeleka hospitali ya wagonjwa wa akili Mirembe -Dodoma karibu mara mbili. Akiwa huko Hospitali ana-recover haraka sababu anakunywa dawa (ARV na zile nyingine za kutibu psychosis) kwa lazima - shida ni kuwa akirudishwa nyumbani (na huwa anarudishwa mapema kabla hata haja-recover vizuri) anakuwa hataki tena kunywa dawa, mkilazimisha anaishia kutoroka!

Kwa sasa amekuwa kama mtu aliyechanganyikiwa - haamini tena kuwa anaumwa ukimwi bali anaamini amerogwa, mara anaamini ni hali ya hewa na anazungumza mambo ambayo hasa unajua amechanganyikiwa.

Kwa wale wanaojua namna nzuri ya kuwasaidia wagonjwa wa aina hii (mbali na kuwapeleka hospitali za rufaa za mikoa ama mirembe) naomba ushauri tafadhali. Kama kuna Hospitali private ambayo ina-specialists (kwa mikoa ya Dar, Moro, ama Dom) wa hali kama hii ya ndugu yangu tafadhali naomba contact zao!

Tafadhali kama una-ushauri mwingine usisite ku-shirikiana nami.

Natanguliza shukrani.
Humu JF mtafute mtu anaitwa Deception ni kazi ndogo sana hyo
 
Humu JF mtafute mtu anaitwa Deception ni kazi ndogo sana hyo
Nimesoma kidogo mijadala kumhusu huyu mheshimiwa -naona kuna-sintofahamu ya kutosha! Anyway, ngoja nimtafute, asante kwa kujali mkuu!
 
Huwa wanachomwa ARV’s za sindano ina dumu miezi 3, kuna improvements nilisikia nyingine inadumu miezi 18. Hizo mara nyingi hutolewa kwa wasioweza kufuatilia dawa za kila siku.

Nenda nae kwenye kitengo mjue options zilizopo.
Mmh bei sio ghali kweli Mkuu?
 
Kama umewahi kufuatilia mijadala ya deception bas jib unalo mwenyewe mtoa mada ila tu unajifanya kuwa mgumu kuelewa
 
Huwa wanachomwa ARV’s za sindano ina dumu miezi 3, kuna improvements nilisikia nyingine inadumu miezi 18. Hizo mara nyingi hutolewa kwa wasioweza kufuatilia dawa za kila siku.

Nenda nae kwenye kitengo mjue options zilizopo.

Mleta mada fuata ushauri huo...


Cc: mahondaw
 
Kwa Dar es salaam nenda Hindu Mandal mwone Dr Muya .

As a family mumpe assurance kuwa mtamsadia kwa hali na mali and don't let her see u kuwa mmepanick kupita kiasi inaongeza psychosis level.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom