mbwadinho
Senior Member
- Jun 29, 2016
- 180
- 102
Habari zenu wakuu naomba kuuliza mimi na mdogo wangu tulipata mgao wa mirathi kila mmoja alipata nyumba 1 na nyumba nyingine 1 tulishare sasa hati zote za nyumba alichukua baba yetu mdogo kwasababu kwa kipindi hicho tulikuwa bado tunasoma vilevile tulikuwa bado wadogo sasa kwa sasa nimekuwa mtu mzima nina umri wa miaka 26 .Ajabu sasa nilipomfuata baba mdogo kwa ajili ya kuomba kukabidhiwa hati za nyumba yangu 1 anadai nisubiri kwanza bado mdogo wako anasoma chuo ingawa nilimwambia mbona kila mtu ana nyumba yake aliyokabidhiwa isipokuwa hiyo moja tuliyoshare na mdogo wangu kwann usinikabidhi hiyo moja wakati hiyo nyingine tukisubiri mdogo wangu amalize chuo .ajabu ni kwamba anakataaa anasisitiza mpaka mdogo wangu amalize chuo na chuo bado miaka 3 .Naomba msaada wenu wa hatua zipi za kisheria nifuate