akatanyukuile
JF-Expert Member
- Sep 13, 2019
- 314
- 308
Habari za mda huu wana jamvi mm sijambo na mungu ameonesha utukufu wake.
Bila kuwachosha ninaomba nijikite kwenye mada lengwa. Mimi ni kijana ambaye bado ninahangaika na maisha. Nimefika mjini kama kimbilio langu baada ya kuhitimu chuo 2015 kada ya ualimu na kukosa ajira. Sikubweteka nilijitosa mtaan ili niweze kujikwamua mimi pamoja familia yangu inayonitegemea kwa asilimia kadhaa.
Mimi ninakaa kinondoni tegeta, nilipo zichanga kwa takiribani mwaka na unusu niliweza kupata pesa kiasi cha milioni tatu na nusu hiv ambazo zilikua kwenye account yangu bila kazi. Wazo likanijia nn nifanye na pesa yangu hiyo, niliweza kupata ushauri wakasema ninunue kiwanja angalau niweze kuanza ujenzi hata kama kitakua chumba kimoja ila kingelitosha kwani hali ya kukodi ni ngumu bora niwe kwenye kibanda changu.
Tatizo linakuja kwenye kiwanja hicho, niliponunua nilikua makini ilibidi wauzaji niwapeleke selikari za mitaa ambao kiuhalisia ndio wamekasimishwa madaraka ya kusimamia aridha kwenye mitaa yao.
Tangu ninunue yapata mwaka sasa na miezi kadhaa, sikuawai kuona mtu anakuja kudai eneo ni lake, nimekua nikifanya shughuli tofauti bila bugudha, juzi kati tu ndipo nilipopata vijisent kadhaa nikasema sasa ni wakati wa kuweka kajumba japo kadogo ila kangeniondolea adha ya kodi.
Niliweka msigi nikiwa katikati kwenye ujenzi wakaja vijana waliojitambulisha wanatokea katani yaani ni watendaji ndani ya office ya katibukata hivo wakaniomba vibali vya ujenzi, nilikua sina hivo wakasema itabidi nisimamamishe ujenzi nianze taratibu za kutafta vibali hivyo.
Nilitii sheria na kuanza ufuatiliaji wa vibali nikawaomba wanisaidie taratibu zip zinaanza kufatwa, waliweza kuniambia yakua zipo form zinapatikana office ya mtendaji kata kwa shillingi laki mbili kama fain ya kuanza ujenzi bila taratibu. Kwavile nilikua na nia ya kujenga sikusita nikaitoa kwa huyo afisa, na kuniruhusu kuendelea na kutafuta watu wa kusain maeneo yao wakiwemo afisa mtendaji wa kijini pamoja na diwani kata. Mziki ndipo ukaanza nilipo peleka kwa afisa aligoma kusain na kudai eneo langu lina mgogoro, nikawaomba wanipe chanzo cha mgogoro hawakunipatia ila nikiwaambia wanisainie hawataki wanadai eneo lilishauzwa hivo nimepigwa. Mpaka ninapoandika hapa sielewi nianzie wapi,
Maombi, ninajua jukwaa hili ni penyewe, mnisaidie nifate taratibu zipi kwani nimeishajawa na woga ninashindwa kuendelea na baadae mwenye eneo akaja kama wanavo dai , pili mm nitamshitaki nani hapo kwani aliyeniuzia anadai nani amekusumbua na sina la kumjibu, hivo nilikua ninaomba mnisaidie ikiwezekana wale wanaousiika na aridhi tuwasiliane ili mnipe mwanga maana ninaona ninaelekea kudhurumiwa,
Kiwanja kipo mabwe pande mtaa wa mbopo,. Ninaomba mnisamehe kwa kuandika maelezo marefu sana ila nikatika hali ya kuwaweka saw hali ninayoipitia.
Karibu.
Bila kuwachosha ninaomba nijikite kwenye mada lengwa. Mimi ni kijana ambaye bado ninahangaika na maisha. Nimefika mjini kama kimbilio langu baada ya kuhitimu chuo 2015 kada ya ualimu na kukosa ajira. Sikubweteka nilijitosa mtaan ili niweze kujikwamua mimi pamoja familia yangu inayonitegemea kwa asilimia kadhaa.
Mimi ninakaa kinondoni tegeta, nilipo zichanga kwa takiribani mwaka na unusu niliweza kupata pesa kiasi cha milioni tatu na nusu hiv ambazo zilikua kwenye account yangu bila kazi. Wazo likanijia nn nifanye na pesa yangu hiyo, niliweza kupata ushauri wakasema ninunue kiwanja angalau niweze kuanza ujenzi hata kama kitakua chumba kimoja ila kingelitosha kwani hali ya kukodi ni ngumu bora niwe kwenye kibanda changu.
Tatizo linakuja kwenye kiwanja hicho, niliponunua nilikua makini ilibidi wauzaji niwapeleke selikari za mitaa ambao kiuhalisia ndio wamekasimishwa madaraka ya kusimamia aridha kwenye mitaa yao.
Tangu ninunue yapata mwaka sasa na miezi kadhaa, sikuawai kuona mtu anakuja kudai eneo ni lake, nimekua nikifanya shughuli tofauti bila bugudha, juzi kati tu ndipo nilipopata vijisent kadhaa nikasema sasa ni wakati wa kuweka kajumba japo kadogo ila kangeniondolea adha ya kodi.
Niliweka msigi nikiwa katikati kwenye ujenzi wakaja vijana waliojitambulisha wanatokea katani yaani ni watendaji ndani ya office ya katibukata hivo wakaniomba vibali vya ujenzi, nilikua sina hivo wakasema itabidi nisimamamishe ujenzi nianze taratibu za kutafta vibali hivyo.
Nilitii sheria na kuanza ufuatiliaji wa vibali nikawaomba wanisaidie taratibu zip zinaanza kufatwa, waliweza kuniambia yakua zipo form zinapatikana office ya mtendaji kata kwa shillingi laki mbili kama fain ya kuanza ujenzi bila taratibu. Kwavile nilikua na nia ya kujenga sikusita nikaitoa kwa huyo afisa, na kuniruhusu kuendelea na kutafuta watu wa kusain maeneo yao wakiwemo afisa mtendaji wa kijini pamoja na diwani kata. Mziki ndipo ukaanza nilipo peleka kwa afisa aligoma kusain na kudai eneo langu lina mgogoro, nikawaomba wanipe chanzo cha mgogoro hawakunipatia ila nikiwaambia wanisainie hawataki wanadai eneo lilishauzwa hivo nimepigwa. Mpaka ninapoandika hapa sielewi nianzie wapi,
Maombi, ninajua jukwaa hili ni penyewe, mnisaidie nifate taratibu zipi kwani nimeishajawa na woga ninashindwa kuendelea na baadae mwenye eneo akaja kama wanavo dai , pili mm nitamshitaki nani hapo kwani aliyeniuzia anadai nani amekusumbua na sina la kumjibu, hivo nilikua ninaomba mnisaidie ikiwezekana wale wanaousiika na aridhi tuwasiliane ili mnipe mwanga maana ninaona ninaelekea kudhurumiwa,
Kiwanja kipo mabwe pande mtaa wa mbopo,. Ninaomba mnisamehe kwa kuandika maelezo marefu sana ila nikatika hali ya kuwaweka saw hali ninayoipitia.
Karibu.