Msaada wa tiba au ushauri kwa maumivu makali ya kichwa na mgongo kwa mwanamke aliyejifungua kwa operation

Nkondo 2

Senior Member
Oct 10, 2016
163
127
Ndugu wana jukwaa naomba msaada kwa mke wng ambaye amejifungua kwa operation leo n siku ya tano (5) anasumbuliwa na maumivu makali sana ya kichwa, shingo na mgongo inayopelekea hata kukaa anashndwa muda mwingi anakuwa amelala tu.

Hospital tumeruhusiwa juzi kwa kupewa vidonge vya ant pain (diclofenac) huku tukihakikishiwa ataendelea vzr kwan hiyo n hali ya kawaida lakini imekuwa kinyume hali imekuwa mbaya mnoo muda wote analia tu kwa maumivu hata kumhudumia mtoto hawezi.

Huu ni uzao wake wa kwanza, naomba msaada ndgu zangu nimsaidieje?
 
Anywe maji ya kutosha
Asizungumze zungumze
Sababu ya maumivu hayo Ni kutopewa drip za kutosha na kutopata muda wa kupumzika Mara baada ya kupata faham
 
Jaribu kumeza vitunguu swaum punje 5 usiku unapoll na punje 3 ukiamka kwa siku 7 unywe lita2-3 za maji kwa siku. Usisahau kuja kuleta feedback. Utahisi mapigo ya moyo kwenda mbio, usiogope ni kawaida ukiona kero punguza idadi ya punje
Asnte kwa ushaur ndgu.
 
Pia jaribu kumkanda mgongoni na kichwani kwa kutumia mafuta ya karafuu,au olive.
 
Kwanza ajikaze, asilale Sana, jion na asubuhi atembee hata azunguke ndani, maji anywe mengi ya kutosha.

Halo ikizidi kuwa mbaya amwone daktari!!
 
Nkondo 2, Habari!

Poleni, hilo linalomkuta mkeo ni moja ya tatizo ambalo huwakumba wanawake wengi waliofanyiwa upasuaji wa uzazi (c/s).. Maranyingi ni kutokana na zile sindano zinazochomwa chini ya kiuno.

Tatizo la mkeo litaisha japo maumivu huwa yanarudi kwa mbali hasa kipindi cha baridi huko mbeleni.

Ushauri wetu afyakliniki ni kuwa fika hospital kwa huduma zaidi iwapo hali hiyo itaendelea kwa zaidi ya wiki 2.

Asante na Karibu
 
Pole sana ukitoka operation huwa hawaruhusu kuongea seems mgonjwa wako alianza kuongea baada ya kutoka na hayo ndo madhara yake. Afanye mazoezi ya kutembea, anywe maji mengi sana kitaacha chenyewe. Hyo sindano kuuma huwa ni shida kwa walio chomwa sindano ya mgongo. Hapo atafte wale wakufanyisha mazoezi ya misuli. Nilishaapa sitaruhusu Dr anachoma sindano ya mgongo bora anizime kabisa.
 
Habari!

Poleni, hilo linalomkuta mkeo ni moja ya tatizo ambalo huwakumba wanawake wengi waliofanyiwa upasuaji wa uzazi (c/s).. Maranyingi ni kutokana na zile sindano zinazochomwa chini ya kiuno.

Tatizo la mkeo litaisha japo maumivu huwa yanarudi kwa mbali hasa kipindi cha baridi huko mbeleni.

Ushauri wetu afyakliniki ni kuwa fika hospital kwa huduma zaidi iwapo hali hiyo itaendelea kwa zaidi ya wiki 2.

Asante na Karibu
Asnten!!
 
Pole sana ukitoka operation huwa hawaruhusu kuongea seems mgonjwa wako alianza kuongea baada ya kutoka na hayo ndo madhara yake. Afanye mazoezi ya kutembea, anywe maji mengi sana kitaacha chenyewe. Hyo sindano kuuma huwa ni shida kwa walio chomwa sindano ya mgongo. Hapo atafte wale wakufanyisha mazoezi ya misuli. Nilishaapa sitaruhusu Dr anachoma sindano ya mgongo bora anizime kabisa.
Shukrani
 
Jaribu kumeza vitunguu swaum punje 5 usiku unapoll na punje 3 ukiamka kwa siku 7 unywe lita2-3 za maji kwa siku. Usisahau kuja kuleta feedback. Utahisi mapigo ya moyo kwenda mbio, usiogope ni kawaida ukiona kero punguza idadi ya punje
Vitunguu saumu vinasababisha damu kuwa nyepesi kwa mwenye kidonda haruhusiwi kunywa au anatarajia kufanyiwa operesheni
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom