Msaada wa Subaru Forester au BMW 3 SERIES, X3

Emmado

JF-Expert Member
Dec 2, 2010
209
214
Wakuu polen na majukumu!!

Naomba ushauri wenu ... nichukue gari gani kati ya gari tajwa hapo juu... {subaru forester, Bmw 3 series au x3...
ushauri huo naomba ulenge kwenye
>>> ulaji wa mafuta
>>>gharama za vipuri
>>>uimara wa gari
>>>upatikanaji wa mafundi wa kuaminika

NB: MATUMIZI YA GARI YATAKUA NI OFF-ROAD KIDOGO

ASANTENI SANA!!
 
Sijui off road unamaanisha nini hasa, ila 3 series haifai kwenye hilo. Iko chini saana na suspension ni sporty. Kwenye Forester na X3, binafsi nitakwenda Forester, model ya kuanzia mwaka 2008. X3 ya kwanza haikuwa nzuri kuvile, ni kama jamaa walikuwa wanajifunzia hapo kuingia kwenye segment ya small SUVs. Ila Forester 2nd and 3rd gen ziko poa.

Ulaji wa mafuta, X3 iko vizuri, kama utachukua ya engine ndogo. Forester iko juu kidogo kwenye mafuta sababu ya AWD.

Kwenye off roading, the Forester is a clear winner hapo.
 
Sijui off road unamaanisha nini hasa, ila 3 series haifai kwenye hilo. Iko chini saana na suspension ni sporty. Kwenye Forester na X3, binafsi nitakwenda Forester, model ya kuanzia mwaka 2008. X3 ya kwanza haikuwa nzuri kuvile, ni kama jamaa walikuwa wanajifunzia hapo kuingia kwenye segment ya small SUVs. Ila Forester 2nd and 3rd gen ziko poa.

Ulaji wa mafuta, X3 iko vizuri, kama utachukua ya engine ndogo. Forester iko juu kidogo kwenye mafuta sababu ya AWD.

Kwenye off roading, the Forester is a clear winner hapo.
Hata mimi nimeshindwa kuzielewa foresta za 2008 zinataka kufanana na RAV4 nahisi toleo zuri la foresta ni kuanzia 2003,04,05
car_image.jpeg
car_image.jpeg
 
Kama ni mm hapo sina chaguo kabisaaa yote ni Luxury Car hayo. Hakuna gari ya kazi hapo. Subaru Engine yake ikizingua huwa hairudi Kama Zamani. Pia Spare Zake zipo Juu sanaaa. Na KIBONGO BONGO Hakuna Mafundi Wazuri wa Subaru.
 
Ach
Kama ni mm hapo sina chaguo kabisaaa yote ni Luxury Car hayo. Hakuna gari ya kazi hapo. Subaru Engine yake ikizingua huwa hairudi Kama Zamani. Pia Spare Zake zipo Juu sanaaa. Na KIBONGO BONGO Hakuna Mafundi Wazuri wa Subaru.
Acha uongo wewe jamaa,spare za subaru zipo nyingi na kuna maduka yapo special kwa ajili ya subaru tu nenda mtaa Livingstone kariakoo,mwenge,posta kote utapata spare zake.

Spare zake ni genuine hamna za kuchakachua kama TOYOTA
 
Hata mimi nimeshindwa kuzielewa foresta za 2008 zinataka kufanana na RAV4 nahisi toleo zuri la foresta ni kuanzia 2003,04,05View attachment 1052933View attachment 1052933
Unajua Forester zina soko kubwa saana US. Sasa kule wanapenda gari za juu. Walikuwa wanalalamika saana kuwa hizi models before 2008 ni basically a wagon tu imeinuliwa. Sio SUV. Haina space ya kutosha. Ndio maana ikabidi waikuze kidogo.
 
Sijui off road unamaanisha nini hasa, ila 3 series haifai kwenye hilo. Iko chini saana na suspension ni sporty. Kwenye Forester na X3, binafsi nitakwenda Forester, model ya kuanzia mwaka 2008. X3 ya kwanza haikuwa nzuri kuvile, ni kama jamaa walikuwa wanajifunzia hapo kuingia kwenye segment ya small SUVs. Ila Forester 2nd and 3rd gen ziko poa.

Ulaji wa mafuta, X3 iko vizuri, kama utachukua ya engine ndogo. Forester iko juu kidogo kwenye mafuta sababu ya AWD.

Kwenye off roading, the Forester is a clear winner hapo.


Off-road ... nimemaanisha pia natumia kwenye barabara za vumbi ..
 
Unajua Forester zina soko kubwa saana US. Sasa kule wanapenda gari za juu. Walikuwa wanalalamika saana kuwa hizi models before 2008 ni basically a wagon tu imeinuliwa. Sio SUV. Haina space ya kutosha. Ndio maana ikabidi waikuze kidogo.
Nimekusoma mkuu
 
Sijui off road unamaanisha nini hasa, ila 3 series haifai kwenye hilo. Iko chini saana na suspension ni sporty. Kwenye Forester na X3, binafsi nitakwenda Forester, model ya kuanzia mwaka 2008. X3 ya kwanza haikuwa nzuri kuvile, ni kama jamaa walikuwa wanajifunzia hapo kuingia kwenye segment ya small SUVs. Ila Forester 2nd and 3rd gen ziko poa.

Ulaji wa mafuta, X3 iko vizuri, kama utachukua ya engine ndogo. Forester iko juu kidogo kwenye mafuta sababu ya AWD.

Kwenye off roading, the Forester is a clear winner hapo.
Huifahamu x3 2011 kuendelea sio gari ya kulinganisha na foresta labda Kama budget inasumbua

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Prado na X3 wapi na wapi?

Kwanza Prado ya mwaka upi?

Sent using Jamii Forums mobile app
Jamaa kasema anataka gari inayoweza kwenda off road. Prado is a proper 4x4 kuliko X3 yoyote.

2nd Gen Prado, ie nafikiri zilianza kutoka 2002 mpaka 2007 au 2008 unaweza kuipata kwa bei ya chini ya x3 ya 2011. Na kwa mtazamo wangu, yatakuwa ni maamuzi ya maana kuliko kununua x3
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom