mchakachuaji192
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 366
- 68
wadau poleni na mihangaiko inayotuweka mjini, naomba mwenye ujuzi au uelewa wa malighafi inayotumika katika utengenezaji wa vioo anijulishe jamani, na je hapa kwetu Tanzania kuna kiwanda kinachohusika na utengenezaji wa vioo au ndio hadi tuagize ughaibuni? Je kama malighafi zinapatikana kwa urahisi ni kikianzishwa hapa Tanzania kinaweza kulipa? Ninasema hivi utengenezaji wa vioo kutokana na kuwa ni miongoni mwa bidhaa muhimu zinazotumika miongoni mwa shughuli za ujenzi wa hasa wa siku hizi na kwa baadae nahisi itakuwa inalipa sana, naomba ushauri wako VS mchango wa mawazo kwa katika hili jambo,