Msaada wa mawazo: Mwanamke amemuuza mtoto wangu kwa siri

BABA SANIAH

JF-Expert Member
Oct 20, 2013
4,494
5,690
Habari zenu wote kwa pamoja,

Nitaandika kwa kifupi ili nisiwachoshe wasomaji katika jukwaa hili.

Nimezaa na dada fulani hivi mtoto mmoja, tangia pregnancy mpaka mwisho nilimhudumia kwa hali na mali kutokana na kile nilichojaaliwa kwenye uwezo wangu na hadi mtoto anafika mwaka mmoja.

Baada ya hapo alinitaarifu mtoto anampeleka kwa dada yake nami nikasema no problem, so long nilikutanishwa nae na matumizi yote ya mtoto sasa nikawa napeleka kwa dada mtu, kwakuwa yeye ndio yuko na mtoto.

Lakini nikaanza kupata mashaka, kwanini dada mtu amlee mtoto ambae si wake, nikaanza kutumia intelijensia yangu niliyopata. Baada ya kukamilisha upelelezi nikagundua kumbe mtoto wangu kauzwa bila ya mimi kufahamishwa. Kwamba kulikua na makubaliano ya siri sirini.

Makubaliano yalikua dada mtu kwa kuwa hana mtoto na jamaa anaeishi nae anataka mtoto basi wakauziana wa kwangu ili aendelee kulinda ndoa yake kwa jamaa, nikatumia mbinu nikawatisha wakaenda kituo cha polisi kushitaki, tukaitwa wote, mimi baba wa mtoto halali mama wa mtoto halali
mama wa mtoto aliepewa baba wa mtoto aliebambikiziwa.

Kila mtu akaeleza anavyojua mama wa mtoto halali akasema mtoto wangu alikufa yule wa dada yake mama wa mtoto bandia, mtoto amezaa na mumewe alivodai baba wa mtoto bandia, ananishangaa mimi kudai mtoto wakati si wangu maamuzi yaliyofikiwa, tukapime DNA. DNA ikionyesha mtoto ni wangu na nina uhakika asilimia zote.

Je kuna haja ya kumwachia nafasi mtoto akamsalimu mama yake wakati alimuuza nikipata ushindi hapa mali zangu yaani mtoto watanipa baada ya muafaka wa suala hili kuna haja ya kuendelea kuwa na mahusiano ya kifamilia na kindugu na hiyo familia.


Ahsanteni, nawasilisha.
 
Nazichanga,nimelipa 100000
bado 200000 mpaka january 2018 inshaalah ntakua nimelipa na vipimo ,
ntawajuza tu,humu,
 
Wakubwa wapo humu kweli kwa umri wangu hili zito kwa kweli lakin ingekua mm ningesha ua wote hata kwa shiriki
Kwani huna watoto wengine? Mbona unakua nashida ya watoto kama husimamishi vizur. Komaa tuu tafuta mke mwingine oa kisha atakuzalia mtoto mzuri tuu huyo achana nae utapoteza muda wako bure kama hela zako hazina kazi mpe hata mama yako atakushukulu sana tuu tena milango yarizk itafunguka sana mpk ushsngae. Mtoto kitu gani bwana. Ila kama huna uzazi jinyime ukamchukue mtot wako km unao mpotezee tuu utaliwa pesa zako bure
 
Dogo huyu kuna kipindi mpaka ada za chekechea nishamlipia sana tu.
***** zao mademu wengine,wasengerema kweli aisee
Jiangalie nawewe usioneshe uzaifu sana kwa madem. Kama umependwa pendeka sio uwachezee afu utukane madada wa watu. Penda dem mmoja. Mtoto utawapata tuu.
 
Kwani huna watoto wengine? Mbona unakua nashida ya watoto kama husimamishi vizur. Komaa tuu tafuta mke mwingine oa kisha atakuzalia mtoto mzuri tuu huyo achana nae utapoteza muda wako bure kama hela zako hazina kazi mpe hata mama yako atakushukulu sana tuu tena milango yarizk itafunguka sana mpk ushsngae. Mtoto kitu gani bwana. Ila kama huna uzazi jinyime ukamchukue mtot wako km unao mpotezee tuu utaliwa pesa zako bure
Soma tena ulichokiandika....sitaki kuamini umekusudia ulichoandika.
 
Snowhite,ni kwamba kwa mfano Nizae na wewe kama ni mwanamke,halafu umpe mtoto dada yako,aseme kazaa na mumewe.
Iko hivyo.
 
Snowhite,ni kwamba kwa mfano Nizae na wewe kama ni mwanamke,halafu umpe mtoto dada yako,aseme kazaa na mumewe.
Iko hivyo.
lakini mtoo umesema alikaa kwa mamake mwaka mzima!
ningeelewa kama angejifungua tu na kumpa dadake!
najiuliza huyo mwanaume wamembambikiaje motto wa mwaka?
 
Umeuliza swali la mbele sana, ungesubiri kwanza vipimo vya DNA, usijidanganye tu una uhakika mtoto ni wako, jiandae kisaikolojia kupokea majibu yeyote, usije ukafa kwa presha baada ya kuambiwa majibu.
 
Back
Top Bottom