Msaada wa Makadirio ya gharama kutoka Tanzania kwenda Marekani kupiati njia zifuatazo

LUKAMA

JF-Expert Member
May 28, 2017
1,081
1,271
Kama kichwa cha habari kinavo jieliza, nimeona habari moja toka BBC kuhusu raia wa Afrika magharibi sana sana Nageria wanaojilipua na kuvuka mpaka kwenda America japo kuwa njia ni hatari sana kwani watu wengi wanafia njiani na wengi pia wanafanikiwa kufika.

Njia wanazopita

Safari inaanzia Nageria hadi Ecuador kwa ndege kwa sababu sheria za uhamiaji sio ngum sana katika nchi hi baada ya hapo wanachua basi hadi Colombia, wakishafika hapa wanchua Botti hadi sehem inayoichwa Darian Gap, sasa kuanzia hapa mziki unapokuja kwasababu unatembea kwa mkuu hadi kuitafuta mexico ukiwandani ya msitu mnene wenye wanyama wakari, walanguzi wa madawa ya kulevya na majambazi, ukisha toboa hapa basi ukombele ya safari mambo yanakua mazuri kwa habari ya usalama.

Nimeona watoto wadogo, wakinadada, vijana wakiume na wazee jinsia zote, wengine wameondoka na familia yote toka Afrika na kujaribu bahati yao kwenda U.S.A.

wakuu nilikuwa naomba mchanganuo wagharama kama na mimi naweza fanya namna ya kujilipua niende kwa Trump nikasake maisha mazuri , ukiona watu wana risk maisha ujui huko kuna asali na maziwa, watu wa finance wanasema the high the risk, high the return.

Nadhani wengi wandugu zetu kuto mataifa ya africa magharibi wamefanikwa kwa sababu ya kutoongopa risk ya kwenda mataifa yalioendelia kusaka noti.

Wenye ueliwa na njia hii anaweza kushare hapa tukapata ujuzi wa kwenda kutafuta fusa kwenye nchi zilizo endelia kama U.S.A
 
Nimesoma makala moja inaweza kukuchua miaka ata 15 ndani kambi ukisubili kupata kibari cha kuingia USA wana kambi zao na wametunga sheria kama unaomba ifadhi USA basi uwe umepitia nchi mbili ziwe zime kupa ifadhi USA hiwe ya tatu
 
Vijana wengi wanadhania maisha ya Marekani ni kula bata tu, ukweli ni kwamba kama huna kazi maisha ni magumu sana. Nisingekushauri uweke rehani maisha yako kuelekea usikokujua kwani kufanya hivyo ni kujitakia kifo!! Nyumbani ni kuzuri kama ukiamua kufanya kazi kwani huwezi kufa njaa kutokana na jinsi tunavoishi!!! Marekani ni unyama unyama tu hakuna cha undugu!

Vijana msidanganyike na haya mnayoona kwenye sinema haya ni maigizo tu na sio uhalisia wa maisha huko majuu!!! Huko Los Angeles marekani kuna sehemu inaitwa SKID ROW, huko vijana wa Bongo wangeona maisha yalivyo sidhani wangetamani hata kuzamia kwenda marekani kwani ni shidaaa!! Vijana chapeni kazi nyumbani msihangaike.
 
Kuzamia ni kujitoa maisha yako kama liwalo na liwe potelea mbali japo wabongoo wengine wanaweza kujifariji kuwa nyumbani ni kuzuri ila hawajui maisha ya wenzao hapa bongoo huwa ni shida kiasi gani mpaka mtu ana amua kufanya maamuzi hayo wewe kama unashamba pambana nalo kama unabiashara ongeza ubunifu kama umeajiriwa kitengo kizuri hongera zako
 
Kuzamia ni kujitoa maisha yako kama liwalo na liwe potelea mbali japo wabongoo wengine wanaweza kujifariji kuwa nyumbani ni kuzuri ila hawajui maisha ya wenzao hapa bongoo huwa ni shida kiasi gani mpaka mtu ana amua kufanya maamuzi hayo wewe kama unashamba pambana nalo kama unabiashara ongeza ubunifu kama umeajiriwa kitengo kizuri hongera zako
Hakuna cha shida ni tamaa tu ya kutaka kuishi maisha ambayo huna uwezo nayo
kwa mfano jamaa huyo ili hadi kufika huko Darian gap aanze kutembea mpk afike mexico hapo tuseme si chini ya laki 5 labda anayo (kadirio la chini)

sasa mbona laki 5 ni mtaji mzuri wa kuanzia na bodaboda ya mkopo bank
Ukikamilisha vigezo akiwa na bodaboda yake na akijituma akiweka tamaa za ujana pembeni na akiwa na matumaini katika boda yake kama hayo ya kwenda marekani
Ndani ya miaka 3 ana bajaji zake mbili

akijituma zaidi ndani ya miaka 10 anatia timu LAS VEGAS kula bata akiwa bonge la boss

Maisha ni kujituma lazima uanze chini kwenda juu haina haja ya kurisk maisha wakati bongo fursa kibao hata za mtaji wa laki 2 sema tunachagua kazi wkt tunasahau job zingine japo tunaona hazina hadhi lakini lazima tuzipitie kama daraja ili upate mtaji walaki 5 km upo katika familia duni lazima Uanze na bizness ya mtaji wa laki 1 kufikia mtaji laki 5 ukuvushe ufike mtaji wa milioni
 
Nimesoma makala moja inaweza kukuchua miaka ata 15 ndani kambi ukisubili kupata kibari cha kuingia USA wana kambi zao na wametunga sheria kama unaomba ifadhi USA basi uwe umepitia nchi mbili ziwe zime kupa ifadhi USA hiwe ya tatu
umesoma wapi hilo mkuu???
 
Haimaanishi ukifika kwenye hiyo kambi ndio unapata access Ya kuingia US.unasililizia miaka na miaka.
 
shkurani wote kwamajibu yenu, me naomba msaada wa gharama kama naweza nikajaribu bahati yangu, mbona huyo mama kaweza sembuse mimi kidume cha nguvu sina watoto kama mama hapo juu
 
Back
Top Bottom