Msaada wa luku

Vitus mkumbee

Member
Nov 1, 2010
22
1
Wazee naombeni msaada mimi nikinunua umeme wa 30000 haumalizi hata mwezi na sina matumizi makubwa nina frig moja tu na inatumika siku moj moja.taa nimefunga energ sever sina jiko wala nini tatizo nini? Wire ring ni mpya au kuna mautundu maana nackia huko dar wengine wananunua umeme wa 500
na unamaliza mwezi mzima kama kuna maujanja tupeane jamani.
 
wewe bora una tatizo hilo mimi nahitaji LUKU ya digital nimeshatuma mail tanesco wanipe utaratibu na cost bila majibu na ukionda ofisini foleni ya kufa mtu mwenye msaada niambie na bei
 
Umeme wa 30,000 sio mwingi saaana.
Unaweza ukapiga mahesabu nini kinakula sana kama ifuatavyo.
1. Zima kila kitu.
2. Washa kitu unachotaka kupima.
3. Angalia jinsi ile indiketa la Luku inavyoblink hesabu blinks in 5 min.
4. Zidisha Blinks X 12 kupata blinks in one hour.
5. Kwenye luku imeandikwa blinks ngapi ni unit moja e.g blinks 1000 =1 unit (Sijui actual number sipo karibu na Luku)
6. Blink per hour / 1000 = Units per hour

Hivyo utakuwa umejua kifaa hicho kinakula Unit ngapi kwa saa.

Pia ushauri mwengine ni kuzima vitu kama TV/Radio/DVD player kwenye switch ya ukutani maana hivi vitu vinakula umeme hata kama vipo off.
 
Pia ushauri mwengine ni kuzima vitu kama TV/Radio/DVD player kwenye switch ya ukutani maana hivi vitu vinakula umeme hata kama vipo off.

Mkuu hii kitu nilikua siijui ndio maana utakuta nazima kilakitu lakini nikirudi na kuangalia luku nakuta imekula ka unit
 
Ndo maana Shirika letu linataka kutufia! Yaani unataka upewe ujanja ili uwaibie TANESCO? Hebu tuwe makini na nchi yetu jamani fuata ushauri uliopewa wa kupima kifaa kimoja kimoja ili ujue ni kipi kinachotumia umeme mwingi wazo la kupewa maujanja siliungi mkono kabisa!! Zaidi nitakwambia endele kulipa hiyo pesa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom