Msaada wa kutoa sumu mwilini na kupungua

Allydasmartboy001

JF-Expert Member
Jul 14, 2018
599
206
Habari zenu ndugu zangu, mimi ni kijana wa umri wa miaka 22 ila na urefu wa 183cm,uzito wangu nin 95KG. Kiukweli na uzito mkubwa kiasi cha kwamba kuna muda nikitembea sana naona shida hasa jua likiwa kali (ingawa ukinitizama kwa kuwa kidogo mrefu utaona kama na mwili wa kawaida ). Ninaonaga matangazo kabla haujaanza kufanya mazoezi unaitajika uondoe sumu kwanza mwilin ili upungue haraka bila hvyo utafanya mazoez na usione chochote.

Sasa naomba njia ya kundoa sumu mwili. Na ninaomba vyakula vizur kwa ajili ya kupungua nilisoma kitabu cha Dr. Berg cha YOUR BODY TYPE moja ya principle anakwambia usile sugar au carbohydrate. Swali langu hapa n moja nitakula nini? Maana kila tunda ninalo liona ni carbohydrate au kuna matunda ambayo siyo carbohydrate? Kwa wataalamu naombeni mpangirio mzur wa chakula ili nione matokeo mapema kwasababu huu mwili naona ubako elekea hypertension inaniita maana naziona dalili kabisa za hypertension.

Asanteni sana kama kuna mtu ana mpangilio mzuri wa chakula labla atataka anicheck basi number yangu ya whatsapp ni 255713696164
 
Fanya mazoezi ya kutosha,you are still a very young man,sioni kwanini usifanye mazoezi kila siku kwa muda usiopungua nusu saa mpaka mwili utoe jasho...
 
Yaani usile Carbohydrate kabisa?. Haki ya nani wewe unatafuta kifo. Unajua kazi kuu ya carbohydrate mwilini ni kutoa nishati ,unaambiwa hata Metabolism ya Fats/Lipids na Protein haiwezekani bila Carbohydrate kuwepo.

Nina ushahidi wa shemeji yangu aliyewahi ingizwa mkenge kwa kufuata ushauri huo akaonja joto la jiwe Kwani ndani ya siku tatu baada ya kuacha vyakula vya wanga aliishiwa nguvu kiasi cha kushindwa hata kutembea.

Nijuavyo Mimi hapo ni kupunguza kiwango cha fats na carbohydrate na kuongeza kiwango cha protein kwasababu protein haitunzwi mwilini japo utazisulubu figo unless uwe unakunywa Maji mengi Sana.
 
Fanya mazoezi.
Tumia vinywaji vyenye uwezo wa kuondoa sumu mwilini mfano green smoothie..inasaidia mno kuondoa sumu mwilini na kupunguza huku ukifuatilia ulaji mzuri na wenye kukuletea matokeo chanya mwilini mwako
 
Fanya mazoezi.
Tumia vinywaji vyenye uwezo wa kuondoa sumu mwilini mfano green smoothie..inasaidia mno kuondoa sumu mwilini na kupunguza huku ukifuatilia ulaji mzuri na wenye kukuletea matokeo chanya mwilini mwako
Aongeze Himalayan salt na turmeric
 
Fanya mazoezi.
Tumia vinywaji vyenye uwezo wa kuondoa sumu mwilini mfano green smoothie..inasaidia mno kuondoa sumu mwilini na kupunguza huku ukifuatilia ulaji mzuri na wenye kukuletea matokeo chanya mwilini mwako
Nisaidie nifahamu SUMU MWILINI ni vitu gani, vipo wapi, viliingiaje na vikitoka vinafananaje?
 
Yaani usile Carbohydrate kabisa?. Haki ya nani wewe unatafuta kifo. Unajua kazi kuu ya carbohydrate mwilini ni kutoa nishati ,unaambiwa hata Metabolism ya Fats/Lipids na Protein haiwezekani bila Carbohydrate kuwepo.

Nina ushahidi wa shemeji yangu aliyewahi ingizwa mkenge kwa kufuata ushauri huo akaonja joto la jiwe Kwani ndani ya siku tatu baada ya kuacha vyakula vya wants aliishiwa nguvu kiasi cha kushindwa hata kutembea.

Nijuavyo Mimi hapo ni kupunguza kiwango cha fats na carbohydrate na kuongeza kiwango cha protein kwasababu protein haitunzwi mwilini japo utazisulubu figo unless uwe unakunywa Maji mengi Sana.
Sawa kiongiz wangu nimekuelewa sana tuu
 
Miaka 22 una 95Kg? Aiseeeeee 26 yrs nilikuwa na 57Kg!! Mambo ya kukataza kula ni uzushi cha msingi zingatia unacchoingiza kiwe kidogo kuliko unachotoa!! Fanya mazoezi sana kula kama kawaida!! Kuna watu nawajua wanafukia balaa alafu wembamba tu....Kama ushagundua mwili wako ni wa kufutuka basi jichoshe sana,usikae kizembe zembe.
 
Badili mfumo WA maisha yako kabisa.. Kuanzia chakula.. Kula wanga kidogo, Jitahidi matunda na mboga mboga kwa wingi... Anza mazoezi Kama ni kukimbia ongeza muda na Umbali kila siku. ..anza sasa ukichelewa kisukari kipo mlangoni
 
Mkubwa kama vipi mlo wako mmoja kula matunda peke yake huku ukizingatia kufanya mazoezi ya kawaida tu sio kama Yale ya kina Mwakinyo
 
miaka 22 ila na urefu wa 183cm,uzito wangu nin 95KG.
Hapo upo urefu wako ni futi 6 (183cm) . Uzito wa 95kg unakaribia kufikia kiwango cha juu cha ubwanyenye kufuatana na kimo chako. Kimo chako uzito wa chini usipungue 67kg ukawa kimbaumbau na usizidi 100kg.

Ideal Body Mass Based on BMI
height (cm)minimum weight (BMI=20)obesity (BMI=30)
18367.0100.5
18467.7101.6
18568.5102.7
18669.2103.8

mimi ni kijana wa umri wa miaka 22 ila na urefu wa 183cm,uzito wangu nin 95KG.
Graph ikionesha uzito kwa urefu ambapo ukiwa 77kg - 82 kg utakuwa na wastani mzuri wa uzito wenye afya njema umbaumbau upo mbali na pia ubwanyenye tipwa tipwa upo mbali.

Line chart of ideal weight in kg for dressed men aged 25 and above, in function of height in cm with shoes and skeleton. For an average skeleton, and height of  157, weight varies from minimum 53.3 to maximum 58.2 kg. For 160 cm, minimum  54.9, maximum 60.3. For 165 minimum 57.6, maximum 63. For 170 minimum 60.7, maximum 66.6. For 175 minimum 64.2, maximum 70.6. For 180 minimum 67.8, maximum 74.5. For 185 minimum 71.4 maximum 79. For 190 minimum 75.3, maximum 83.5. For 195 minimum 79.8, maximum 87.9.

Ideal weight in kg for dressed men of average skeleton, aged 25 and above, as a function of height in cm with shoes
 
Eat foodstuffs zenye low caloric value; avoid animal fats maana ziko saturated, kwepa sana sweet drinks (use water --- glasi 8-10/siku), zingatia consistency katika ulaji na epuka snacking.
 
Back
Top Bottom