Msaada wa kutatua hili tatizo la tumbo

kwisha

JF-Expert Member
Sep 9, 2021
1,666
4,365
Jambo ndugu zangu

Mimi Nina tatizo la tumbo ambalo nimesha jiuliza maswali mengi sipati jibu and sometime nimesha anza kuhisi Kama nimerogwa. Mimi tumbo langu linavurugika.

Kuna muda nahisi kama vile Kuna mtu ana kwaruza ndani ya tumbo langu na linanguruma saana na ninatoa hewa chafu yaani na Jamba sana.

Nina pata choo vizuri tu ili tatizo mara nyingi linakuja pale ninapo kuwa na mawazo mengi Yaani Nina hisi tumbo lime jaa saana na Linavimba au ni kila cha kula chochote ambacho kimelala.

Na shindwa kuelewa kama ili ni tatizo gani.
 
Nenda hospital mkuu, pia uwe unakoroga magadi husaidia kuondoa gesi, Mimi Kuna kipindi tumbo ka Hilo lilikuwa linanisumbua mtani wangu akanipa dawa ya asili mpaka Leo imebaki historia
Nilienda kwa bahati mbaya waliniambia sina tatizo lolote la tumbo niko sawa ni mimi tu kubadirisha style yangu ya kuishi hapo ndipo nachanganikiwa.
 
Nilienda kwa bahati mbaya waliniambia sina tatizo lolote la tumbo niko sawa ni mimi tu kubadirisha style yangu ya kuishi hapo ndipo nachanganikiwa.
Tafuta dawa za asili Mimi lilinitesa Hadi mtu akanipa dawa za asili gesi kwishney
 
Nilihenda kwa bahati mbaya wali ni ambia sina tatizo lolote la tumbo Niko sawa
Ni mimi tu kubadirisha style yangu ya kuishi
Apo ndipo na changanikiwa
Nenda tena kajaribu kuangalia vidonda vya tumbo hasa peptic ulcers ambao mara nyingi husababishwa na bacteria aina ya Helicobacter Pylori mara nyingi ndo huwa na hizo dalili.
Lakini pia zingatia mfumo wako wa ulaji huenda ndiyo ikawa sababu kubwa ya wewe kupitia hilo tatizo hebu nenda hospitali au maabara kubwa ujaribu kufanya hivyo nilivyokwambia kwanza..
 
Nenda tena kajaribu kuangalia vidonda vya tumbo hasa peptic ulcers ambao mara nyingi husababishwa na bacteria aina ya Helicobacter Pylori mara nyingi ndo huwa na hizo dalili.
Lakini pia zingatia mfumo wako wa ulaji huenda ndiyo ikawa sababu kubwa ya wewe kupitia hilo tatizo hebu nenda hospitali au maabara kubwa ujaribu kufanya hivyo nilivyokwambia kwanza..

Inaweza ikawa kweli mana hata mm nilikuwa na tatizo hili tumbo lilikua linasumbua na kuunguluma mara kwa mara ilifikia hatua kila siku asubuhi linaunguluma sana nilienda kwa dokta akanambia ni dalili ya vidonda vya tumbo ila pia husababishwa na stress zinazopelekea kutokula chakula kwa mda mwafaka
 
Una vidonda vya tumbo, una bloating, una constipation, lakini pia digestion lane au track yako ipo congested au toxic.

Hiyo kitu haitibiwa kwa dawa za hospital ikaondoka na kukuacha na amani. Dawa ni kucheki diet yako na kurekebisha iweze kwenda sawa na mahitaji ya mwili wako.
 
Una vidonda vya tumbo, una bloating, una constipation, lakini pia digestion lane au track yako ipo congested au toxic.

Hiyo kitu haitibiwa kwa dawa za hospital ikaondoka na kukuacha na amani. Dawa ni kucheki diet yako na kurekebisha iweze kwenda sawa na mahitaji ya mwili wako.
Doctor kasema

Sent from my Infinix X572 using JamiiForums mobile app
 
Doctor kasema

Sent from my Infinix X572 using JamiiForums mobile app
Haya ni matatizo ya kiafya ambayo yanatokana na changamoto za mabadiliko ya mfumo wa maisha na ulaji.

Mimi nimefuatilia sana hii kitu na inawakuta watu wengi sana hadi vitoto vidogo masikini.

Na mahospitalini hata madaktari wenye taaluma hii kitu inawatoa knock out sababu si kitu cha maambukizi bali ni swala la tabia. Kutibu hii hali unahitaji kuwa makini zaidi na namna unakula kuliko namna unakwenda hospital
 
Haya ni matatizo ya kiafya ambayo yanatokana na changamoto za mabadiliko ya mfumo wa maisha na ulaji.

Mimi nimefuatilia sana hii kitu na inawakuta watu wengi sana hadi vitoto vidogo masikini.

Na mahospitalini hata madaktari wenye taaluma hii kitu inawatoa knock out sababu si kitu cha maambukizi bali ni swala la tabia. Kutibu hii hali unahitaji kuwa makini zaidi na namna unakula kuliko namna unakwenda hospital
Na namna tunakula ndo penye changamoto zaidi.
Tunakula kushiba hatuzingatii balance diet.

Kula kwa afya iwe moja ya vipaumbele.

Sent from my Infinix X572 using JamiiForums mobile app
 
Haya ni matatizo ya kiafya ambayo yanatokana na changamoto za mabadiliko ya mfumo wa maisha na ulaji.

Mimi nimefuatilia sana hii kitu na inawakuta watu wengi sana hadi vitoto vidogo masikini.

Na mahospitalini hata madaktari wenye taaluma hii kitu inawatoa knock out sababu si kitu cha maambukizi bali ni swala la tabia. Kutibu hii hali unahitaji kuwa makini zaidi na namna unakula kuliko namna unakwenda hospital
Hivi kwa nini vitabu vya dini havijaandika namna ya kula ili tusiumwe, au namna ya kujitibu kiasili haya magonjwa? Napata mashaka sana na hizi dini, kazi yake ni kusema usifanye hivi, toa sadaka, saidia masikini nk
Ila tukiumwa dini haina majibu, inakwambia tu tenda mema ili ukifa uende peponi na nyoko nyoko zingine za dini
 
Hivi kwa nini vitabu vya dini havijaandika namna ya kula ili tusiumwe, au namna ya kujitibu kiasili haya magonjwa? Napata mashaka sana na hizi dini, kazi yake ni kusema usifanye hivi, toa sadaka, saidia masikini nk
Ila tukiumwa dini haina majibu, inakwambia tu tenda mema ili ukifa uende peponi na nyoko nyoko zingine za dini
Mmmmmmhmn nadhani vimeongea ila kwa mafumbo sana. Ila ubongo una namna yake ya kukuelekeza namna ya kutafuta tiba lishe kwa kutumia mifumo yake ya ufahamu.

Kwa mfano kuna muda unajiskia una hamu ya kula chakula cha aina fulani bila hata wewe kuchagua. Ukifuata ile kitu utaona mwili unajibalance.

Shida ni huwa tunabagua vyakula. Ulaji wetu una haribu ile system na matokeo yake mwili unaanza kujenga tamaa na vyakula ambavyo si vya kuimalisha bali vya kuharibu mwili.
 
Haya ni matatizo ya kiafya ambayo yanatokana na changamoto za mabadiliko ya mfumo wa maisha na ulaji.

Mimi nimefuatilia sana hii kitu na inawakuta watu wengi sana hadi vitoto vidogo masikini.

Na mahospitalini hata madaktari wenye taaluma hii kitu inawatoa knock out sababu si kitu cha maambukizi bali ni swala la tabia. Kutibu hii hali unahitaji kuwa makini zaidi na namna unakula kuliko namna unakwenda hospital
Toa ushauri mtu anapaswa alaje
 
Back
Top Bottom