Msaada wa kupata talaka kwa imani ya kiislam kwa mwanamke

minji

JF-Expert Member
Sep 2, 2016
2,751
4,933
Wanajamii naamin mu wazima na mmeamka salama. Kama uzi unavyojieleza hapo juu nina dada angu aliolewa kwa imani ya dini kiislamu. Alikaa kwenye ndoa yake kwa muda wa miaka 7 alijaliwa kupata watoto wawili ila alishindwa sababu ndoa yao haikuwa na amani hata kidogo, ilijaa vipigo na mambo mengi ambayo nashindwa kuyaandika.

Mwanamke aliamua kuondoka kama miaka 2 na nusu iliyopita na kuamua kurudi kwao na yule mwanaume aliamua kuoa mke mwingine hiyo haikuwa tabu kwa ndugu yetu sababu aliamua kuondoka kabisa. Sasa shida imekuwa ni moja yule mwanaume hataki kutoa talaka, dada angu anamuomba sana talaka yake yule mwanaume anamwambia atamkomesha hampi talaka.

Sasa tulikuwa tunauliza, je BAKWATA wanaweza toa talaka akipeleka malalamiko yake au mpaka aende mahakamani? Kwa yeyote mwenye uelewa wa hili suala ninaomba atusaidie kuhusu hili naamin humu kuna watu wa aina mbali mbali tutapata muafaka.
 
Mwambie dada alipeleke tatizo lake Bakwata,ni bora zaidi kuanzia huko kwasababu umesema ni ndoa iliyofungwa kwa imani ya dini ya kiislam.
 
Mwambie dada alipeleke tatizo lake Bakwata,ni bora zaidi kuanzia huko kwasababu umesema ni ndoa iliyofungwa kwa imani ya dini ya kiislam.
Ndio ilifungwa kwa iman ya dini ya kiislam na dada alibadir dini na kuwa muislam,asante sana tutamshauri afanye hivyo
 
Ndoa ni ngumu na yahitaji uvumilivu yy la misingi aelekee bakwata ndio haki yake itapatikana,ktk imani yake upo mwongozo wa ndoa na ni yapi yanayobatilisha ndoa,kwa kuwa yy(Dada) yamemfika kooni akifikisha malalamiko yake yatapimwa na ikioneka ipo sbb ya kubatilisha ndoa hiyo hapo yatakayofuatwa kwa misingi ya imani yake,akumbuke imani iliyotumika kuunganisha ndoa yake na ndo hiyo itakayotumika kubatilisha ndoa yake,imani yake haiko kwa ajili ya kufurahisha mabadiliko/matakwa ya binadamu INA misingi isiyobadilika na maelekezo sahihi juu ya maisha yake.
 
Ndoa ni ngumu na yahitaji uvumilivu yy la misingi aelekee bakwata ndio haki yake itapatikana,ktk imani yake upo mwongozo wa ndoa na ni yapi yanayobatilisha ndoa,kwa kuwa yy(Dada) yamemfika kooni akifikisha malalamiko yake yatapimwa na ikioneka ipo sbb ya kubatilisha ndoa hiyo hapo yatakayofuatwa kwa misingi ya imani yake,akumbuke imani iliyotumika kuunganisha ndoa yake na ndo hiyo itakayotumika kubatilisha ndoa yake,imani yake haiko kwa ajili ya kufurahisha mabadiliko/matakwa ya binadamu INA misingi isiyobadilika na maelekezo sahihi juu ya maisha yake.
Asante kwa ushauri
 
ndoa si kulazimishana aende bakwata kuna sheria maalum katika uislam ya kesi kama hizi,na itakuwa wepesi sana hyo ndoa kuvunjika,laa akienda mahakamani ndoa haivunjiki na hatoweza kuolewa ndoa nyengine ya kiislam,zaidi atakuwa anazini tu.
 
Kwanini Hugo mume akatae kutoa talaka ? Kwani msaafu unasemaje mwanamme katili akikataa kutoa talaka ?
 
aende kwa kadhi wa eneo alipo!aandae na mahari ya kumrudishia mume kiasi kilekile alichopewa yeye mwanamke.
la kuongezea makadhi wengi akishaona hivyo anapata chansi ya kuomba amuoe au amkule hayo mawili ategemee mojawapo
 
Akirudisha mahari watoto watakua wa nani?au nao atatakiwa awarudishe kwa baba yao?
aende kwa kadhi wa eneo alipo!aandae na mahari ya kumrudishia mume kiasi kilekile alichopewa yeye mwanamke.
la kuongezea makadhi wengi akishaona hivyo anapata chansi ya kuomba amuoe au amkule hayo mawili ategemee mojawapo
 
Mahakama ya Kadhi kama inafanya kazi,ustawi wa jamii au bakwata ndo suluhu ya kumnusuru huyo ndugu......
 
Kwa mujibu wa sheria lazima uanzie baraza la usuluishi na kwa muislam baraza la usuluishi ni bakwata ikishindikana kusuruishwa bakwata watakupa karatasi ya kwenda nayo mahakamani kwa ajili ya kuvunja ndoa na kupewa haki yako ya taraka huo ndio utaratibu kisheria
 
miaka miwili na nusu bila kushiriki tendo la ndoa si ni TALAKA tayari? anaweza fanya mambo mengine hata kuolewa...
au unamaanisha unattaka msaada wa kugawana mali? waliyochuma?....
 
hivi mwanaume tu ndio hutoa talaka?mwanamke hawezi kumwita mahakamani na kumpa talaka?hivi kweli hakuna mwanaume anayedai talaka?maana nawaona wanawake tu wakilialia!
 
Alipochukua uamuzi wa kwenda kwao kwa kweli hiyo haikuwa njia ya busara kwake....wakati tabia ya MME wake ya vipigo vya mara kwa mara, alitakiwa taarifa hizi kuzifikisha kwa WASHENGA wa Mme wake....pengine wangeweza kumkanya na Mme kuweza kubadili tabia...

Kama alitoa taarifa kwa Washenga na hatua kutochukuliwa....angeenda kuwaambia watu wa karibu na Mme wake....mfano Makaka ,Wajomba na hata WAZAZI wake kama wapo....na hata WALEZI..

Kama SULUHU ikiwa ngumu (kwa maana Mme hasikii na kuendeleza vipigo) ndio sasa angeenda kwenye MABARAZA ya usuluhishi ya kijamii....mfano kwa mjumbe wa mtaa...mwenyekiti wa mtaa na hata kwa diwani wa kata (ikiwa kama kweli unataka kuinusuru na kubadili tabia ya MWENZAKO.

Ukiona tabia haibadiliki na vipigo vinazidi elekea sasa ofisi za bakwata zilizo jirani yako, elezea masahibu yako (kero yako) na hatua ulizo pitia katika kutafuta suluhu....

Nina amini BAKWATA wata/wangemuita muhusika (Mme wake) na hapo angeulizwa sababu ya vipigo....angekanywa ...na laiti akitamka hakutaki na ndio sababu ya vipigo....ni matumaini Taraka ingeandikwa..

Vinginevyo kama vipigo vinasababishwa na Mme MLEVI ...Mwanamke yuko huru kudai taraka yake(akishindwa kumsamehe)

Hatua alizo chukua Mwanaume za kuoa Mke mwingine na kukomalia kutoa taraka kwa Mke aliye kimbilia kwao yuko sahihi...kwa maana yeye Mme angali anamtambua mkimbizi kama MKE WAKE HALALI WA NDOA....

Namshauri Mwanamama arudi kwa Mme wake watunze na kulea watoto wao..

Akijidanganya nae kuolewa na mtu mwingine...hakika ndoa hiyo itakuwa BATILI (sio halali)

Nakaribisha mawazo/ushauri.
 
aende kwa kadhi wa eneo alipo!aandae na mahari ya kumrudishia mume kiasi kilekile alichopewa yeye mwanamke.
la kuongezea makadhi wengi akishaona hivyo anapata chansi ya kuomba amuoe au amkule hayo mawili ategemee mojawapo
Kumbe unaweza rudisha mahari ile ile aliyopewa na akapewa taraka naona hii njia ni nzuri zaid
 
miaka miwili na nusu bila kushiriki tendo la ndoa si ni TALAKA tayari? anaweza fanya mambo mengine hata kuolewa...
au unamaanisha unattaka msaada wa kugawana mali? waliyochuma?....
Hataki chochote toka kwa huyo mwanaume aliyopitia yanatosha kabisa anachohitaji ni taraka pekee ili awe huru na nafsi yake sababu hana mpango wa kurudi kwa mumewe kabisa sasa anafanya biashara zake tuu
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom