Msaada wa kununua mali ya serikali

munyiha

Member
Nov 23, 2020
12
12
Habari wana jukwaa.

Naomba kufahamishwa utaratibu wa kufwata kununua/kujimilikisha mali ya serikali.kuna magari mabovu yapo kwenye ofisi za harimashauri nataka niyanunue kama chuma chakavu.

Natanguliza shukrani.
 
Kwa kawaida yanatakiwa kuuzwa kwenye mnada wa wazi uliotangazwa kwa muda wa angalau wiki mbili kabla. Ila kwa jamii yetu hii ya upigaji sitashangaa kusikia huwa yanauzwa tu kinyemela. Nenda kwenye hiyo Halmashauri ukaulizie watakupa utaratibu.
 
Nimesikia kuna njia ya kununua bila mnada kutangazwa
Kwanza nenda tengeneza figisu na Accounting officer wa ofisi husika mweleze nia yako akikuelewa unaandika barua Kwa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha (Hazina) kupitia kwa Accounting officer husika yeye ata sign na kuweka comment za imepitishwa, utaipeleka Wizarani utasikilizai majibu. kama vipi kule nako unaeza tengeneza ularo fresh maana normally MK ata ichannel Barua wahakiki mali wa serikali (huko ndo unatakiwa kutenegenza figisu.

Baada ya hapo utasubiri majibu .... ukiwa umeweka fresh unakamata hizo ndinga kilaini jamaa wanabaki wanashangaa. yupo Jmaa yangu mmoja alinunua zile land cruser za Ma-DAS kizembe ivo, wajuba wakaanza kumwonea wivu!!
 
Back
Top Bottom