Msaada wa kumpata huyu ndege!!

wa stendi

JF-Expert Member
Jul 7, 2016
24,685
26,779
Wakuu poleni na weak and!!!naombeni mwenye kujua kwa hapa dar ni wapi naweza kupata yule ndege anaetoboa mashimo kwenye gogo la mti mkavu!! Huyu ndege huwa ana kichwa kikubwa kidogo na manyoya ya kichwa ni ya rangi nyekundu na mgongoni anakuwa na madotidoti meusi kama ya kanga pori!!
 
Tuambie kwanza unamuitaji kwa ajiri ya nn?Uku nilipo wapo wengi sana..ni swala la kuwaambia vijana tu wanakuletea.
 
Haya maisha yalivyo magumu watu watauliza kila aina ya vitu vya ajabu kwa maagizo ya matabibu jadi. Tusubirie kuulizwa wapi anapatikana bundi jike, machozi ya samaki, maziwa ya kuku n.k
 
Wakuu poleni na weak and!!!naombeni mwenye kujua kwa hapa dar ni wapi naweza kupata yule ndege anaetoboa mashimo kwenye gogo la mti mkavu!! Huyu ndege huwa ana kichwa kikubwa kidogo na manyoya ya kichwa ni ya rangi nyekundu na mgongoni anakuwa na madotidoti meusi kama ya kanga pori!!
Woodpecker
 
Huyo dege kama yeye kumpata kazi sana, ila mimi nina baadhi ya unga wa viungo vyake kama ifuatavyo

1. Kichwa na nyusi zake
2. Kidevu na taya ya juu
3. Manyoya mgongoni mchanganyo na za kisogoni
4. Uti wa mgongo ulo changanywa na ncha ya mdomo unaotumika kutobolea
5. Ubongo ulochanganywa na fuvu lake
6. Mfupa paja na kucha moja anayotumia kunolea mdomo wake
7. Manyoya ya nyuma yalosagwa na udongo wa uliotoka chini ya mti wenye kitanda cha nyani
8. Utumbo wake uliopamoja na nyongo yake ila umechanganywa na samaki wa nchi kavu ambao hupatikana ghuba ta uajemi kwa shughuri maalumu
9. Macho yake yalochanganywa na machozi ya samaki aina papa pamoja na gesi ya kijambo cha nguluwe mjamzito nyakati za usiku
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom