KUNO NA KUNO
Member
- Jul 11, 2014
- 7
- 2
Wandugu wapendwa. Salamu nyingi sana.
Mimi ni mwanachama wa JF kwa kitambo sasa. Nina ombi ninaloomba waungwana mnisaidie. Nimeandika mswada wa kitabu kinaitwa Harakati za Fungate, Lizame Tugawane Mbao. Kitabu hiki kina mambo mengi ya kijamii (sana) kinazungumzia mtu mmoja aliyezaliwa kijijini tena kusikofika hata magari, ni maskini kuanzia unyayoni hadi kwenye unywele! Akapata bahati ya kufaulu, babake akashindwa kumsomesha, ikafikia mzee wake akapelekwa mbele ya baraza ashtakiwe kwa kushindwa kusomesha mtoto wake wakati ana mifugo hasa mbuzi na kuku, ikabida auze kuogopa kufungwa. Pia huyo bwana akapata ufadhili wa kigeni kwenda kusoma nje, akiwa huko akawa anawaza tu watu wake kijijini na tabu za maisha, alipomaliza masomo akarudi nchini, ila akabadili mfumo wa maisha akalewa na madaraka, akasahau kwao akajichanganya na maisha ya peponi....
huo ni muhtasari tu, natamani waungwana, mkiweo JF mnisaidie kuchapisha kitabu hiki kiifikie jamii. Naomba kuwasilisha wandugu!
kwa mawasiliano tafadhali tuwasiliane kwa disabilityhabari@gmail.com au 0777004455
Mimi ni mwanachama wa JF kwa kitambo sasa. Nina ombi ninaloomba waungwana mnisaidie. Nimeandika mswada wa kitabu kinaitwa Harakati za Fungate, Lizame Tugawane Mbao. Kitabu hiki kina mambo mengi ya kijamii (sana) kinazungumzia mtu mmoja aliyezaliwa kijijini tena kusikofika hata magari, ni maskini kuanzia unyayoni hadi kwenye unywele! Akapata bahati ya kufaulu, babake akashindwa kumsomesha, ikafikia mzee wake akapelekwa mbele ya baraza ashtakiwe kwa kushindwa kusomesha mtoto wake wakati ana mifugo hasa mbuzi na kuku, ikabida auze kuogopa kufungwa. Pia huyo bwana akapata ufadhili wa kigeni kwenda kusoma nje, akiwa huko akawa anawaza tu watu wake kijijini na tabu za maisha, alipomaliza masomo akarudi nchini, ila akabadili mfumo wa maisha akalewa na madaraka, akasahau kwao akajichanganya na maisha ya peponi....
huo ni muhtasari tu, natamani waungwana, mkiweo JF mnisaidie kuchapisha kitabu hiki kiifikie jamii. Naomba kuwasilisha wandugu!
kwa mawasiliano tafadhali tuwasiliane kwa disabilityhabari@gmail.com au 0777004455