Msaada wa kisheria

Luthar

JF-Expert Member
Jul 29, 2011
519
105
Habari zenu ndugu wasomaji ni matumaini yangu mu wazima wa afya .Kuna dada yangu kapelekwa polisi na wenzake kisa wamemkopeshea pesa. Tulienda polisi kumwekea mthamana lakini askari walisema hiyo pesa anayo shitakiwa nayo nikubwa sana mil 18 walewalio mkopeshe kila moja alimkopeshea kwa muda wake pesa jumla ni kama milion 6 lakini chakushangaza wameungana wote watatu wakasema wamempa mil 18 Alafu akuna kitu walichowekeana mthamana dada kaachiwa maelezo kashatoa kwa mpelelezi kila siku tunaambiwa turudi polisi kisa kwamba wale wanawake bado hawaja toa maelezo yao ushauri please
 
Ivi kesi za madai zinaanzia polisi siku izi au tayari washamshtaki mahakama ya mwanzo ndo..mh bado sijaelewa.
Shemeji Ruttashobolwa ebu come zis way...
 
Last edited by a moderator:
Ivi kesi za madai zinaanzia polisi siku izi au tayari washamshtaki mahakama ya mwanzo ndo..mh bado sijaelewa.
Shemeji Ruttashobolwa ebu come zis way...
iyo ni janja tu ya kumpa pressure mdaiwa alipe deni ndo maana kila siku wanaambiwa warudi polisi eti wadai hawajatoa maelezo
 
Habari zenu ndugu wasomaji ni matumaini yangu mu wazima wa afya .Kuna dada yangu kapelekwa polisi na wenzake kisa wamemkopeshea pesa. Tulienda polisi kumwekea mthamana lakini askari walisema hiyo pesa anayo shitakiwa nayo nikubwa sana mil 18 walewalio mkopeshe kila moja alimkopeshea kwa muda wake pesa jumla ni kama milion 6 lakini chakushangaza wameungana wote watatu wakasema wamempa mil 18 Alafu akuna kitu walichowekeana mthamana dada kaachiwa maelezo kashatoa kwa mpelelezi kila siku tunaambiwa turudi polisi kisa kwamba wale wanawake bado hawaja toa maelezo yao ushauri please

Baada ya kuelezea mkasa wote huo Hujasema ni msaada gani unataka !!!!!!!!!
 
kisheria, ushauri wa kisheria ni gharama tafuta 'contact' (mawasiliano) ushauriwe kisheria UCBABAISHE NDG YANGU!
 
Kwanza mdeni afungwi, hapo dawa ni kukubali kulipa deni na utapewa muda! Wala usijali askari wetu ni watu wa kudandia kama case ikifika mahakamani kila mmoja ataambiwa afungue case yake ya madai!

Habari zenu ndugu wasomaji ni matumaini yangu mu wazima wa afya .Kuna dada yangu kapelekwa polisi na wenzake kisa wamemkopeshea pesa. Tulienda polisi kumwekea mthamana lakini askari walisema hiyo pesa anayo shitakiwa nayo nikubwa sana mil 18 walewalio mkopeshe kila moja alimkopeshea kwa muda wake pesa jumla ni kama milion 6 lakini chakushangaza wameungana wote watatu wakasema wamempa mil 18 Alafu akuna kitu walichowekeana mthamana dada kaachiwa maelezo kashatoa kwa mpelelezi kila siku tunaambiwa turudi polisi kisa kwamba wale wanawake bado hawaja toa maelezo yao ushauri please
 
Ndugu yangu wazo langu ni kujiuliza je kutolipa deni ni kosa la jinai linalopaswa kufanyiwa uchunguzi na chombo cha dola!!? Kiukweli haikustahili kumpeleka huyo dada yako polisi maana hayo ni mambo binafsi kati ya wadai na mdaiwa. Na kama ishu ilikuwa ni kudai pesa zao wangeungana katika kesi ya madai na kudai hizo pesa kwa njia ya mahakama na ithibitishwe kwamba alikopa kweli katika makubaliano ya mdomo tu. Sasa mimi nahisi kitendo cha kumpeleka polisi kwa wale wasiojua watakuwa wameshamuita ni 'mwizi' sasa hapo wajiangalie wakishindwa kesi hiyo hizo pesa wanazodai katika shauri atakalofungua huyo dada kana kesi ya madai itaitwa malicious prosecution na atadai fidia inayoweza kuwa zaidi ya pesa alokuwa anadaiwa. Kwahiyo basi ushauri wangu ni kwamba onaneni na wanasheria na mfanye namna ya kumtoa hapo maana hiyo sio sahihi kabisa kumpeleka remand na kama wameshikilia kama mwizi sina wasiwasi kuwa hiyo kesi wanaodai watashindwa tu kwa kukosa ushahidi. Naomba niwakilishe na nasimama kurekebishwa.
 
Back
Top Bottom