Wamizigo
Member
- Sep 8, 2017
- 52
- 54
Habari wana jf?,
Mimi ni mtumishi (mshika chaki) kuna mtumishi mwenzangu tumezinguana nae kutokana na tabia zake za ajabu, hasa za kunisema vibaya mbele za wanafunzi, huku yeye akijikweza.
Kutokana na kuzinguana huko, taarifa zilifika kwa afisa elimu, na afisa akadai kuwa tuandike barua za kuomba kubadilishiwa vituo vya kazi kwa kujihamisha wenyewe ili tuwe shule tofauti. Sasa barua zimejibiwa jana, cha ajabu mimi nmehamishiwa shule ya kijijini kabisa halafu mwenzangu kaachwa pale pale kwenye kituo cha awali (hajahamishwa), nmejaribu kumuuliza afisa elimu sababu za kutomhamisha mwenzangu ambaye ndo chanzo cha ugomvi hata walimu wengine wanamjua wanakaa nae mbali, afisa anajibu kuwa sijamhamisha kwa sababu ni mwalimu wa sayansi wewe ni Arts na shule ina uhaba wa walimu wa sayansi.
Baada ya kunijibu hivyo nimeshindwa nifanyaje na nilikopelekwa ni bush kweli,ukiangalia hata makosa sina kabisa, sasa nifanyaje kabla ya siku 7 nilizopewa za kwenda kuripoti hazijaisha?
Mimi ni mtumishi (mshika chaki) kuna mtumishi mwenzangu tumezinguana nae kutokana na tabia zake za ajabu, hasa za kunisema vibaya mbele za wanafunzi, huku yeye akijikweza.
Kutokana na kuzinguana huko, taarifa zilifika kwa afisa elimu, na afisa akadai kuwa tuandike barua za kuomba kubadilishiwa vituo vya kazi kwa kujihamisha wenyewe ili tuwe shule tofauti. Sasa barua zimejibiwa jana, cha ajabu mimi nmehamishiwa shule ya kijijini kabisa halafu mwenzangu kaachwa pale pale kwenye kituo cha awali (hajahamishwa), nmejaribu kumuuliza afisa elimu sababu za kutomhamisha mwenzangu ambaye ndo chanzo cha ugomvi hata walimu wengine wanamjua wanakaa nae mbali, afisa anajibu kuwa sijamhamisha kwa sababu ni mwalimu wa sayansi wewe ni Arts na shule ina uhaba wa walimu wa sayansi.
Baada ya kunijibu hivyo nimeshindwa nifanyaje na nilikopelekwa ni bush kweli,ukiangalia hata makosa sina kabisa, sasa nifanyaje kabla ya siku 7 nilizopewa za kwenda kuripoti hazijaisha?