silent kills
JF-Expert Member
- Jun 11, 2016
- 566
- 779
Salam,
Naitwa Noel na nimekuwa mdau mkubwa sana kwwnye jukwaa hili la sheria na nimeona ushauri mzuri unaotolewa na wanasheria waliomo kwenye jukwaa.
Niende kwenye mada husika hapo juu nilikodi shamba mwaka jana ili nione najikwamuaje na ukosefu huu wa ajira unaotusumbua vijana wengi.
Nilienda Kilosa mji mdogo wa Kilangali kutafuta aridhi ya kulima na kwa bahati mbaya nikakutana na wenyeji matapeli wakanikodishia shamba lenye mgogoro. Sasa nikiwa shambani mwenye nalo akaja na kunikuta shambani nikamuelezea mimi ni mgeni na shamba nimekodisha tu hivyo sijui lolote.
Nilimtaarifu aliyenikodishia shamba ndo nikakutana nae kwa mtendaji kesi ikawa nzito waliosema nimevamia wakasema hawana shida na aliyenikodishia shamba wana shida na mimi hivyo wakaomba barua toka kwa mtendaji waende Polisi na hivyo nimeitwa polisi.
Aliyesema nimevamia hamtaki aliyenikodishia kwa sababu anasema kuna kesi iko mahakamani na mwenye shamba nae kasema haendi maana kuna kesi kuhusu shamba hili iko mahakani kwahiyo hawezi kwenda. Wakuu kesho ndo naenda Polisi nahitaji msaada wa haraka sana angalau nione napataje kitu kidogo changu nilichopoteza.
Nilitaka kuwatag baadhi ya wanasheria ila ninaowajua wako humu ila sjui kama wao wanahusika na ardhi.
Msaada tafadhali.
Naitwa Noel na nimekuwa mdau mkubwa sana kwwnye jukwaa hili la sheria na nimeona ushauri mzuri unaotolewa na wanasheria waliomo kwenye jukwaa.
Niende kwenye mada husika hapo juu nilikodi shamba mwaka jana ili nione najikwamuaje na ukosefu huu wa ajira unaotusumbua vijana wengi.
Nilienda Kilosa mji mdogo wa Kilangali kutafuta aridhi ya kulima na kwa bahati mbaya nikakutana na wenyeji matapeli wakanikodishia shamba lenye mgogoro. Sasa nikiwa shambani mwenye nalo akaja na kunikuta shambani nikamuelezea mimi ni mgeni na shamba nimekodisha tu hivyo sijui lolote.
Nilimtaarifu aliyenikodishia shamba ndo nikakutana nae kwa mtendaji kesi ikawa nzito waliosema nimevamia wakasema hawana shida na aliyenikodishia shamba wana shida na mimi hivyo wakaomba barua toka kwa mtendaji waende Polisi na hivyo nimeitwa polisi.
Aliyesema nimevamia hamtaki aliyenikodishia kwa sababu anasema kuna kesi iko mahakamani na mwenye shamba nae kasema haendi maana kuna kesi kuhusu shamba hili iko mahakani kwahiyo hawezi kwenda. Wakuu kesho ndo naenda Polisi nahitaji msaada wa haraka sana angalau nione napataje kitu kidogo changu nilichopoteza.
Nilitaka kuwatag baadhi ya wanasheria ila ninaowajua wako humu ila sjui kama wao wanahusika na ardhi.
Msaada tafadhali.