Msaada wa kisheria: Dada yangu katapeliwa nyumba Dodoma

hati miliki ilikuwa na jina la marehemu au jina la huyo jamaa aliewauzia ? swali langu kwako kwa nini dada yako ameshindwa mahakamni? maana hakimi anatoa maelelzo yote anapompa mtu ushindi wa kesi

Eti mvuta bangi

ndugu muuzaji alikuwa na vielelezo vyote ikiwemo hati miliki ya nyumba na ndio maana wakili alihusika na mwenyekiti wa serikali ya mtaa anamjua na alitoa maelezo ya yy ndo msimamizi hao wengine walikuwa hawaishi dodoma pia nyumba yenyewe ilikuwa ni pagala halikufikia hata level ya kupaua ni kama wao walinunua kiwanja wao wamijenga kuwa nyumba kamili

mkuu omba ufafanuzi ili wakat unaandika hayo upate picha kamali
 
ina jina la marehemu haikuwa na jina la muuzaji

hiyo ndio sababu ya kushindwa kesi.. hata uende mahakama ya nchi gani utashindwa tena... sababu msimamizi wa mirathi anakuwa na uthibitisho wa mahakama.. sio maneno tupu
 
unaehisi huyo dada kwa nini ameshindwa kesi mahakamani na kuporwa nyumba?

Wakili wasonga nakuhakikishia bila kuacha chembe ya wasiwasi alipewa hela ajitoe ktk kesi na alifanya hivyo hiyo taarifa tulipewa na msamailia mwema wa ofisini kwake mchezo huo uliendelea hatua zote

mara ya kwanza dada yangu kesi alishinda mara ya pili wakashinda wao baada ya wakili kujitoa
 
hiyo ndio sababu ya kushindwa kesi.. hata uende mahakama ya nchi gani utashindwa tena... sababu msimamizi wa mirathi anakuwa na uthibitisho wa mahakama.. sio maneno tupu


Hapo nimesahau kukwambia mwanzo kesi dada yangu alishinda hatua zote
 
sina uwezo wa kubandika hukumu hapa ya mwanzo ambayo dada yangu alishinda upepo ulibadilika baada ya kukata rufaa na wakili wasonga kujitoa
 
Ninachojua mimi kazi ya mwanasheria unapomuita katika mauziano ya vitu ni
1. Kufanya tafiti na kujua uhalali wa kumiliki na uhalali wa kuuza wa eneo au nyumba husika.
2. Kuandaa nyaraka za mauziano kisheria.

Nionavyo hapo wakili hakufanya kazi yake na ikibidi mfungulie kesi mahakamani ili akufidie yeye au Bima yake.

Kwa hapo alishindwa kutekeleza jukumu lake la kwanza kwa weledi au kwa maslahi binafsi, Aliyekuuzia nyumba (mdogo wa marehemu) sio mtu sahihi ni lazima Angekuwa msimamizi wa miradhi au kungekuwa na mhutasari wa kikao cha familia kuridhia kufanya hiyo biashara.
 
Bila kupoteza muda niende kwenye mada.

Dada yangu na mume wake walinunua nyumba dodoma maeneo ya Nkuhungu ambayo waliuziwa na mdogo wa mwenye nyumba basi katika hayo mauziano alikuwepo wakili wasonga maarufu sana hapo Dodoma na Mwenyekiti wa kijiji kama shahidi na kulisimamia hilo zoezi.

Baada ya kama miaka kama mitano kupita aliibuka dada wa marehemu na kusema kwamba alieuza nyumba mdogo wao wa kiume hana mamlaka hayo na amelaghaiwa ktk kuuza kesi ikaanza ktk mabaraza ya kata ndipo wakina dada wakaomba aletwe ndugu yao aongee au aonekane jambo ambalo walipinga ndugu wa muuzaji kwamba hayupo kapotea.

Baada ya kuhangaishana sana walianza kutembeza rushwa ndipo waliposhinda kesi na dada yangu kushindwa na inasemekana mumewe na huyo dada yupo serikalini alikuwa akitumia hiyo fursa.

Dada alikata rufaa mahakamani bado hukumu zilitoka kama mwanzo maana michezo ilianza toka katika mabaraza ya ardhi ya kata wazee wa mabaraza tayari walikuwa wanajua nini cha kufanya.

Ilifika kipindi wakili wasonga alijitoa ktk kesi kwamba kesi imekuwa ngumu kwao wakati ktk mauziano ya nyumba alishiriki na kukagua hati za mauziano za nyumba na hata kubadili umiliki wa nyumba kwenda kwa dada na mumewe na allikuwa akilipwa kila hatua gharama za huduma yake.

Lengo langu naombeni msaada dada yangu alitolewa ndani ya nyumba na nyumba ikauzwa haraka sana.

Pia naweza nikawa sijatoa maelezao ya kunyooka sana kama kuna atakae hitaji kumsaidia kisheria na ushauri namba zake ni hizi.


0712 505 872
Akate rufaa ngazi inayofata
 
Ume
hiyo ndio sababu ya kushindwa kesi.. hata uende mahakama ya nchi gani utashindwa tena... sababu msimamizi wa mirathi anakuwa na uthibitisho wa mahakama.. sio maneno tupu
Ingekuwa vyema kama ungepata hiyo hukumu ukaisoma na kujua ni hoja gani mahakama ilijikita katika kumpa ushindi huyo jamaa. kuliko kuhitimisha jambo ambalo hauna uhakika nalo.

Nyumba kuwa na jina la marehemu siyo kigezo cha kushindwa kesi mahakamani ila nyumba kuuzwa na mtu ambae siyo msimamizi wa mirathi ingekuwa sababu nzuri.
 
Ninachojua mimi kazi ya mwanasheria unapomuita katika mauziano ya vitu ni
1. Kufanya tafiti na kujua uhalali wa kumiliki na uhalali wa kuuza wa eneo au nyumba husika.
2. Kuandaa nyaraka za mauziano kisheria.

Nionavyo hapo wakili hakufanya kazi yake na ikibidi mfungulie kesi mahakamani ili akufidie yeye au Bima yake.

Kwa hapo alishindwa kutekeleza jukumu lake la kwanza kwa weledi au kwa maslahi binafsi, Aliyekuuzia nyumba (mdogo wa marehemu) sio mtu sahihi ni lazima Angekuwa msimamizi wa miradhi au kungekuwa na mhutasari wa kikao cha familia kuridhia kufanya hiyo biashara.
Mkuu sidhani kama mahakama itakuwa ni sehemu sahihi kumshitaki huyo wakili kulingana na maelezo yako. Bali kwenye Kamitii ya Mawakili.
 
Muuzaji wakati anauza alikuwa na akili timamu na umri wa zaidi ya miaka 18?
 
msomee albadiri kam mbunge wa kinondoni alivyofanywa na wazanzibar. huwa nasema ukikosa haki mahakamani/duniani....nenda rohoni....WATATAFUTANA.
 
Muuzaji wakati anauza alikuwa na akili timamu na umri wa zaidi ya miaka 18?
Sasa hii hoja yako unalenga nini mkuu? Lengo hapa siyo kutaka kubatilisha huo mkataba bali huyu mteja anataka ajue wapi pa kwenda baadabya kushindwa kesi na atatumia hoja gani katika hiyo rufaa.
 
Je, msimamizi wa miradhi alikuwepo na je muuzaji hakuwa na ndugu zake na wakafanya kikao pamoja na mnunuzi kabla hawajaenda hata kwa mwanasheria kuanza michakato?

Utanununuaje nyumba ya familia kwa mtu mmoja bila kushirikisha ndugu zake?
Mkuu watu wengi haya. Mambo unayoyasema hatuyajui ndio maana tunatapeliwa sana mi mwenyewe nmetapeliwa kiwanja dar kifuru kinyerez nataka nikalianzishe mahakani.

*A good wife is from God, but a good husband is from Kigoma*
 
Ndio sababu inatakiwa kuwa na mtaalamu wa Ardhi kabla ya kununua wanasheria wao ni kuandaa documents tu. Huyo wakili hana Kosa wala lawama.
Huku mtaani tunavoowaamini hao unao waita wanasheria ni hatari kumbe hatujui tu hawana lolote ndio wanachangia kupoteza haki zetu kila leo.

*A good wife is from God, but a good husband is from Kigoma*
 
Na muuzaji kapotea . Mh hapo sasa.
Hiyo ni issue ikiyopqngwa na ndugu hata huko kuuza walikaa kikao auze yy pekee yake ili wao waje wadai kuwa hakuwa na mamlaka kisheria ndio maana yule alieuza hakuonekana kwenye kesi.. Hii inakuja kwa kuwa watu wengi hatujui sheria kama kitu kinachoozwa kikiwa cha familia au cha urithi wa watu kuanzia 2 si vizur kukinunua kwa mtu 1 hata kama anaeuza anahati ya hiko kitu au kama mhusika ana mke pia sio vizuri mke nae awe mbali ni bora nae aweke saini yake maana baadae waweza kuuziwa ubao nk.

*A good wife is from God, but a good husband is from Kigoma*
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom