Msaada wa kisheria: Dada yangu katapeliwa nyumba Dodoma

radika

JF-Expert Member
Jul 15, 2014
20,429
32,173
Bila kupoteza muda niende kwenye mada.

Dada yangu na mume wake walinunua nyumba dodoma maeneo ya Nkuhungu ambayo waliuziwa na mdogo wa mwenye nyumba basi katika hayo mauziano alikuwepo wakili wasonga maarufu sana hapo Dodoma na Mwenyekiti wa kijiji kama shahidi na kulisimamia hilo zoezi.

Baada ya kama miaka kama mitano kupita aliibuka dada wa marehemu na kusema kwamba alieuza nyumba mdogo wao wa kiume hana mamlaka hayo na amelaghaiwa ktk kuuza kesi ikaanza ktk mabaraza ya kata ndipo wakina dada wakaomba aletwe ndugu yao aongee au aonekane jambo ambalo walipinga ndugu wa muuzaji kwamba hayupo kapotea.

Baada ya kuhangaishana sana walianza kutembeza rushwa ndipo waliposhinda kesi na dada yangu kushindwa na inasemekana mumewe na huyo dada yupo serikalini alikuwa akitumia hiyo fursa.

Dada alikata rufaa mahakamani bado hukumu zilitoka kama mwanzo maana michezo ilianza toka katika mabaraza ya ardhi ya kata wazee wa mabaraza tayari walikuwa wanajua nini cha kufanya.

Ilifika kipindi wakili wasonga alijitoa ktk kesi kwamba kesi imekuwa ngumu kwao wakati ktk mauziano ya nyumba alishiriki na kukagua hati za mauziano za nyumba na hata kubadili umiliki wa nyumba kwenda kwa dada na mumewe na allikuwa akilipwa kila hatua gharama za huduma yake.

Lengo langu naombeni msaada dada yangu alitolewa ndani ya nyumba na nyumba ikauzwa haraka sana.

Pia naweza nikawa sijatoa maelezao ya kunyooka sana kama kuna atakae hitaji kumsaidia kisheria na ushauri namba zake ni hizi.


0712 505 872
 
Bila kupoteza muda niende kwenye mada.

Dada yangu na mume wake walinunua nyumba dodoma maeneo ya nkuhungu ambayo waliuziwa na mdogo wa mwenye nyumba basi katika hayo mauziano alikuwepo wakili wasonga maarufu sana hapo dodoma na mwenyekiti wa kijiji kama shahidi na kulisimamia hilo zoezi.

Baada ya kama miaka kama mitano kupita aliibuka dada wa marehemu na kusema kwamba alieuza nyumba mdogo wao wa kiume hana mamlaka hayo na amelaghaiwa ktk kuuza kesi ikaanza ktk mabaraza ya kata ndipo wakina dada wakaomba aletwe ndugu yao aongee au aonekane jambo ambalo walipinga ndugu wa muuzaji kwamba hayupo kapotea.

Baada ya kuhangaishana sana walianza kutembeza rushwa ndipo waliposhinda kesi na dada yangu kushindwa na inasemekana mumewe na huyo dada yupo serikalini alikuwa akitumia hiyo fursa.

Dada alikata rufaa mahakamani bado hukumu zilitoka kama mwanzo maana michezo ilianza toka katika mabaraza ya ardhi ya kata wazee wa mabaraza tayari walikuwa wanajua nini cha kufanya.

Ilifika kipindi wakili wasonga alijitoa ktk kesi kwamba kesi imekuwa ngumu kwao wakati ktk mauziano ya nyumba alishiriki na kukagua hati za mauziano za nyumba na hata kubadili umiliki wa nyumba kwenda kwa dada na mumewe na allikuwa akilipwa kila hatua gharama za huduma yake.

lengo langu naombeni msaada dada yangu alitolewa ndani ya nyumba na nyumba ikauzwa haraka sana.

pia naweza nikawa sijatoa maelezao ya kunyooka sana kama kuna atakae hitaji kumsaidia kisheria na ushauri namba zake ni hizi


0712 505 872
mada za utapeli mbona zimekuwa nyingi leo.
 
Mkuu, sasa hapo ametapeliwa au ameshindwa kesi? Unaweza kuthibitisha utolewaji wa rushwa unaoudai? Kwasasa imekuwa desturi, kila anayeshindwa mahakamani hudai kutolewa kwa rushwa. Nashauri uende kwa Mawakili wengine, ukiacha huyo Wasonga uliyemtaja, na kuwaeleza jambo lako kwa msaada wa kisheria na wa uhakika.
 
Mkuu, sasa hapo ametapeliwa au ameshindwa kesi? Unaweza kuthibitisha utolewaji wa rushwa unaoudai? Kwasasa imekuwa desturi, kila anayeshindwa mahakamani hudai kutolewa kwa rushwa. Nashauri uende kwa Mawakili wengine, ukiacha huyo Wasonga uliyemtaja, na kuwaeleza jambo lako kwa msaada wa kisheria na wa uhakika.

Mkuu hayo mazingira ya hiyo kesi kushindwa yanatia mashaka sana ni vingi kafanyiwa ikiwa ni pamoja kutokupewa haki ya kutokusikilizwa ktk mabaraza ya kata ya ardhi
 
kwa nini ununue nyumba ya marehemu kwa ndugu mmoja tu bila familia yake kuhusishwa...

nahisi dada yako alifanya ulaghai ndio maana mahakamani ameshindwa kesi
 
kwa nini ununue nyumba ya marehemu kwa ndugu mmoja tu bila familia yake kuhusishwa...

nahisi dada yako alifanya ulaghai ndio maana mahakamani ameshindwa kesi
Je, msimamizi wa miradhi alikuwepo na je muuzaji hakuwa na ndugu zake na wakafanya kikao pamoja na mnunuzi kabla hawajaenda hata kwa mwanasheria kuanza michakato?

Utanununuaje nyumba ya familia kwa mtu mmoja bila kushirikisha ndugu zake?
 
watu wanakuwa wajanja wajanja ili wapate bei rahisi... wamemuona huyo jamaa ni mvuta bangi hana uelewa wa thamani za nyumba wakamlaghai awauzie nyumba kwa bei rahisi... ndugu zake wenye akili wameshtuka na kudai nyumba yao... mahakamani kweli wameonekana walaghai ... wanasema wamezulumiwa..

unazulumiwaje nyumba ambayo hata cement hujui ilijengwa kwa mfuko wa kiwanda gani?

jenga nyumba yako ndio uishi kwa amani.. au nunua kwa ushahidi ulionyooka

Je, msimamizi wa miradhi alikuwepo na je muuzaji hakuwa na ndugu zake na wakafanya kikao pamoja na mnunuzi kabla hawajaenda hata kwa mwanasheria kuanza michakato?

Utanununuaje nyumba ya familia kwa mtu mmoja bila kushirikisha ndugu zake?
 
Ndio sababu inatakiwa kuwa na mtaalamu wa Ardhi kabla ya kununua wanasheria wao ni kuandaa documents tu. Huyo wakili hana Kosa wala lawama.
 
watu wanakuwa wajanja wajanja ili wapate bei rahisi... wamemuona huyo jamaa ni mvuta bangi hana uelewa wa thamani za nyumba wakamlaghai awauzie nyumba kwa bei rahisi... ndugu zake wenye akili wameshtuka na kudai nyumba yao... mahakamani kweli wameonekana walaghai ... wanasema wamezulumiwa..

unazulumiwaje nyumba ambayo hata cement hujui ilijengwa kwa mfuko wa kiwanda gani?

jenga nyumba yako ndio uishi kwa amani.. au nunua kwa ushahidi ulionyooka
Muuzaji akiwa na power of attorney inayo mruhusu kuuza nyumba haitaji mtu yeyote mwingine
 
kwa nini ununue nyumba ya marehemu kwa ndugu mmoja tu bila familia yake kuhusishwa...

nahisi dada yako alifanya ulaghai ndio maana mahakamani ameshindwa kesi

Hiyo nyumba ilikuwa na hati aliyopewa muuzaji na ndio maana hapakuwa na mashaka
 
watu wanakuwa wajanja wajanja ili wapate bei rahisi... wamemuona huyo jamaa ni mvuta bangi hana uelewa wa thamani za nyumba wakamlaghai awauzie nyumba kwa bei rahisi... ndugu zake wenye akili wameshtuka na kudai nyumba yao... mahakamani kweli wameonekana walaghai ... wanasema wamezulumiwa..

unazulumiwaje nyumba ambayo hata cement hujui ilijengwa kwa mfuko wa kiwanda gani?

jenga nyumba yako ndio uishi kwa amani.. au nunua kwa ushahidi ulionyooka
Na muuzaji kapotea . Mh hapo sasa.
 
watu wanakuwa wajanja wajanja ili wapate bei rahisi... wamemuona huyo jamaa ni mvuta bangi hana uelewa wa thamani za nyumba wakamlaghai awauzie nyumba kwa bei rahisi... ndugu zake wenye akili wameshtuka na kudai nyumba yao... mahakamani kweli wameonekana walaghai ... wanasema wamezulumiwa..

unazulumiwaje nyumba ambayo hata cement hujui ilijengwa kwa mfuko wa kiwanda gani?

jenga nyumba yako ndio uishi kwa amani.. au nunua kwa ushahidi ulionyooka

Eti mvuta bangi

ndugu muuzaji alikuwa na vielelezo vyote ikiwemo hati miliki ya nyumba na ndio maana wakili alihusika na mwenyekiti wa serikali ya mtaa anamjua na alitoa maelezo ya yy ndo msimamizi hao wengine walikuwa hawaishi dodoma pia nyumba yenyewe ilikuwa ni pagala halikufikia hata level ya kupaua ni kama wao walinunua kiwanja wao wamijenga kuwa nyumba kamili

mkuu omba ufafanuzi ili wakat unaandika hayo upate picha kamali
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom