msaada wa kiafya au ukiukwaji wa haki za binaadamu?

ZeMarcopolo

Platinum Member
May 11, 2008
14,013
7,209
Leo nimesoma habari hii zoka Moshi.Mimi imenipa faraja kidogo lakini wasiwasi pia wa ukiukwaji wa haki za binaadamu kwa sababu kukamata mtu bila idhini yake na bila kibali toka kwenye vyombo vya sheria ni ukiukwaji wa haki za binaadamu.

wewe waonaje?



Halmashauri ya manispaa ya Moshi imeanzisha kampeni ya kudumu ya kuwakamata wagonjwa wa akili na kuwapatia matibabu katika hospitali ya Mawenzi mjini Moshi.

Kampeni hiyo imeanzishwa wakati wa wiki ya siku ya wauguzi duniani iliyokwenda sanjari na kupima afya za wanafunzi wa shule za msingi za kata ya Majengo katika manispaa hiyo.

Kaimu muuguzi mkuu wa manispaa ya Moshi Bi Anastazia Lyimo amesema kampeni hiyo ambayo hadi sasa imefanikiwa kwa kuwakamata wagonjwa wa akili watano, itawasaidia wagonjwa hao kuondokana na mateso wanayoyapata mitaani na jamii kuwa salama.

Amesema baada ya matibabu katika hospitali hiyo watapelekwa kituo cha wagonjwa wa akili cha Longuo ambako wanaendelea kupata matibabu na kutunzwa na baada ya wiki mbili au tatu wanakuwa katika hali nzuri.
 
kwa maoni yangu jibu la Kaimu muuguzi mkuu wa manispaa ya Moshi Bi Anastazia Lyimo ndio jibu muafaka.

"itawasaidia wagonjwa hao kuondokana na mateso wanayoyapata mitaani na jamii kuwa salama"
.
 
Tatizo kubwa ni definition ya mgonjwa wa akili ni nini?

Kwa maana mimi sioni tatizo kumkamata chizi anayetembea uchi barabarani au kula kutoka majalalani.Kwa kweli nitakuwa na tatizo kama hatutamkamata na kumpa hifadhi kama siyo tiba au hata kumtafutia ahueni kwa kumweka katika wodi ya vichaa.Kwa hiyo hili halina tatizo.

Tatizo linakuja kama kesho keshokutwa watu wanaweza kukusema wewe una ugonjwa wa akili kwa sababu tu umefanya kitu controversial lakini si uncalled for.Mtu mzima watu wakakusweka

Kwa hiyo kabla ya kusema kwamba huu ni msaada wa kiafya au ukiukwaji wa haki za binadamu inabidi tuelewe anayehusishwa ni nani.

Kwa wale machizi wa kweli kabisa hili halina mjadala kwa sababu ukitaka kupata ruhusa ya chizi ili umuweke katika wodi ya vichaa wewe ndiye utakuwa chizi zaidi.
 
Sijui sheria ya nchi yetu inasemaje ila kuna nchi ambazo ukimkamata mtu bila idhini yake ni lazima utoe taarifa kwa mahakama within 48 hours ambayo itatuma mwanasheria kuja kutathmini hali ya mgonjwa huyo na kutoa ruhusa ya kuendelea kumshikilia mgonjwa au kukataza kushikiliwa kwake.Sababu ni kama alivyosema Pundit,si sahihi kuassume kuwa kila atakayekamatwa atakuwa amefanyiwa hivyo kwa lengo la kumsaidia.

Prevention is better than cure hivyo basi ni vyema vyombo vya haki za binaadamu vikaangalia hili, ingawa kwa jinsi ninavyoona mimi wameanza kwa malengo mazuri.Ila kama unavyojua watu wenye hila wanaweza kulitumia jambo zuri kwa njia mbaya.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom