Msaada wa haraka sana kwa huyu mwanajeshi kama sio wote

Dogo G

JF-Expert Member
Jul 6, 2018
1,052
440
Isee ni hatari sana.Inahuzunisha sio kidogo saaaana,nimeingiwa na huruma ghafla.Katika kupitapita youtube kujua yaliyojiri nimekutana na clip moja iliyorushwa na online tv moja nimeshindwa kuiweka hapa.Katika hiyo clip kuna mwanajeshi wa kenya anaomba msaada toka kwa serikali ya nchi yake kutokana na kuwa mateka kule somalia.

Huyo mwanajeshi ameonekana anazungumza kwa hofu akitetemeka huku akijitambulisha jina lake,nyumbani anakotokea(jina la mtaa na mji),namba ya kikosi anachotoka na taarifa nyingine nyingi kutoka katika jeshi la kenya KDF.Mwanajeshi huyu amedai hayuko peke yake bali ametekwa na wenzie wengine wasiopungua 20 ambapo wanauawa taratibu kutokana na kuchelewa kwa msaada toka kwa serikali.

Ikimbukwe tu hawa wanajeshi wa kenya walitumwa kule somalia kwaajili ya kulinda amani inayochafuliwa na vikundi vya waasi ikiwemo al-shaabab.Kiongozi wa alshaabab aliwahi kuhojiwa akasema madhila wanayoyafanya kenya kila siku hayataisha mpaka pale serikali ya kenya itakapowaondoa wanajeshi wake kule somalia,na wataendelea kuwaangamiza wanajeshi wa KDF siku zote.

Sasa wakuu sijaelewa ni kwanini raisi wa kenya anashindwa kutoa kauli wakati wanajeshi wametekwa wana miezi zaidi ya mitano.Kenya chukueni hatua kwa walinzi wa taifa.Ni lazma muangalie risk itakayozidi kujitokeza iwapo hawo wanajeshi wataendelea kubaki mikononi mwa alshaabab mfano watakuwa wanatoa siri za KDF ili wasiteswe zaidi.

Source:2020 tv/online tv

Sent using Jamii Forums mobile app
 
well... that risk of being POW is part of the job, plus there is no negotiations with terrorists, the best option is to gather enough intelligence and plan a rescue operation.
 
Alipojiunga na jeshi alijua wazi nini maana yake hapo ninlumuombea to there is nothin no body can right now but to watch and celebrate that hero life while it lasts

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ingekua ni hivyo2 hta America angekua ameshaikimbia Iraq kitambo sana, maana ya kujiunga na jeshi ni kua upo tayari kwa lolote, kufa ndio chagua namba1 kwa ajili ya nchi yako

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom