Amri kuu ni Upendo
JF-Expert Member
- Oct 18, 2012
- 789
- 474
Mwaka 2003 gego langu la mwishoni juu kushoto lilianza kutoboka taratibu na kuuma. Mpaka 2008 likawa limetoboka kabisa na kuanza maumivu makali.Watu kadhaa wamenishauri nisiling'oe eti laweza kuniletea matatizo makubwa katika ung'oaji wake. Mganga mmoja aliwahi kunipa dawa ya kienyeji ambayo ilifuta kabisa maumivu ya jino tangu 2008 hadi mwaka jana, lakini mwaka huu tena maumivu yamerudi yakiambatana na kuvimba kwa fizi. Sasa natamani kuling'oa jino hili ila naomba madaktari wataalamu wa meno wanishauri na ikiwezekana ni kwa namna gani ung'oaji wa jino hili unaweza kufanyika kwa usalama na wapi kwa hapa Dsm naweza kumpata daktari bingwa wa meno. ASANTENI