Msaada wa connection ya biashara ya kuku...

jisanja

JF-Expert Member
Nov 17, 2013
1,075
684
Habari za Leo wanajamii forum jukwaa la ujasiliamali.....Naomba tafadhali kwa yeyote anayeweza kunipa market connection ya Wale wanunuzi wa kuku wa kienyeji (kwa jumla) kwa hapa daresalama Naomba anisaidie.....cuz nmejaribu kuzunguka mahotelini wanasema wana watu special hua wanawaletea...mpaka Nmechoka....msaada plz
 
Habari za Leo wanajamii forum jukwaa la ujasiliamali.....Naomba tafadhali kwa yeyote anayeweza kunipa market connection ya Wale wanunuzi wa kuku wa kienyeji (kwa jumla) kwa hapa daresalama Naomba anisaidie.....cuz nmejaribu kuzunguka mahotelini wanasema wana watu special hua wanawaletea...mpaka Nmechoka....msaada plz

Pole sana mkuu,ndio changamoto za ujasiriamali.Pita kwenye magenge kama kinondoni kwa manyanya,Mwenge na mingineyo.Mahoteli yote watu wame cover mkuu,mzee wangu alifanya hiyo yalimkuta hayo,ila usikate tamaa.Njia nyingine unayoweza kufanya ni kupitia kumbi za maharusi waambie wakuunganishe na watu wa catering,unaweza kupata order kila wikend.

All the best
 
Pole sana mkuu,ndio changamoto za ujasiriamali.Pita kwenye magenge kama kinondoni kwa manyanya,Mwenge na mingineyo.Mahoteli yote watu wame cover mkuu,mzee wangu alifanya hiyo yalimkuta hayo,ila usikate tamaa.Njia nyingine unayoweza kufanya ni kupitia kumbi za maharusi waambie wakuunganishe na watu wa catering,unaweza kupata order kila wikend.

All the best

Nashukuru sana kwa ushaur wako....
 
Uwezo wako ni kuku wangapi kwa wiki au kwa siku na kwenda constant muda gani?
Nauliza hivi kwasababu umeenda kwenye mahoteli makubwa, hawa ni biashara za uhakika, wanataka tenda, sasa wewe unafikiri wataisimamisha tenda yao kwa muda wachukue kwako?
Kwavile unaanza bila jina sio rahisi kupata tenda ya mahoteli makubwa ila unaweza kupata ya wale wanaowapelekea ambao ndio kama wauzaji wa Kisutu sokoni nk. Tafuta watu wanaowapelekea taratibu hadi uwajue ndio na wewe uwauzie hao vinginevyo uza hata kidogokidogo grocery, migahawa hii au ile. Bucha na wachoma chips nk utapata bei nzuri kuliko hao walanguzi wanalalia bei ili wapate faida zaidi. Kama unauhakika wa kushika tenda kwa muda mrefu andika barua au omba kuonana na wamiliki wa hizo hotel sidhani kama utakataliwa.
 
Nenda kwenye masoko wanapouza, kama Kisutu, Manzese
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom