Msaada utata nyumba ya kupanga

Tripp

JF-Expert Member
Feb 2, 2018
899
1,543
Kodi yangu imeisha na sina pesa ya kulipa na mwenye nyumba anataka nitoe vitu bila hata subira nimekimbia nimeacha vitu. Nitavifuata nikipata sehemu nyingine.

kisheria imekaaje hii?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hamia Kenya, hakuna kodi huko.
255752530729_status_7e701c40085e4424bcd84cd97471de4e.jpeg
 
Kodi yangu imeisha na sina pesa ya kulipa na mwenye nyumba anataka nitoe vitu bila hata subira nimekimbia nimeacha vitu...nitavifuata nikipata sehemu nyingine,kisheria imekaaje hii

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa sababu vitu/mali zako bado ziko ndani ya nyumba, maana yake bado umepashikilia.

Kwa hiyo, utakaporudi utalipa kodi ya kipindi ambacho wewe hukuwepo lakini vitu vyako vilikuwepo.

Uwepo wa vitj vyako ni uthibitisjo wa uwepo wako, hivyo inamzuia mwenye nyumba kuitumia nyumba kwa matumizi mengine ikiwemo kuipangisha kwa mtu mwingine.

Dawa ya deni ni kulipa, sio kukimbia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu kwanini unaita utata wakati kila kitu kiko wazi kabisa hapo. Nasikitika kusema kuwa hukufanya uungwana mkuu. Siku moja na wewe ukijenga nyumba yako utaona thamani yake especially nyumba ambayo ni kitega uchumi kinachomfanya Mwenyenyumba aishi:

1. Utakimbia hadi lini sasa.

2. Kwanini hukumwambia mwenye nyumba hali halisi miezi 3 kabla, au miezi 2 kabla au hata ule mwezi wa mwisho kuwa unaomba muda kidogo hali yako ya kiuchumi haijakaa vizuri. Kitendo cha kusubiri siku ziishe alafu unakimbia nadhani sio uungwana mkuu
 
Hivi kuna mtu humu amewahi kupewa hiyo notice akakaa bure miezi mitatu akitafuta nyumba nyingine ya kuhamia?

Labda NHC!😁
 
Back
Top Bottom