Msaada unahitajika maana naona kichwa kinaelekea kupasuka

Dinatalelee

Member
Oct 19, 2021
8
42
Msaada unaitajika ndugu zangu maana hata sijielewi kabisa kwa mambo yanayoendelea. Nilikuwa na mke wangu ila tukaamua kuachana baada ya yeye kuchukua vitu na kuondoka. Baada ya muda kaona haitoshi kamtelekeza mtoto wetu mdogo mwenye umri wa mwaka 1 na nusu kwa sister wangu.

Sister yeye ana biashara zake anazozifanya kwa hiyo muda mwingi yupo kwenye biashara zake pia hapo anapokaa sister kuna barabara, sasa mtoto muda mwingi anakuwa peke yake na kwa vile bado haelewi vizuri unakuta anakaa katikati ya barabara. Mara ya kwanza alishagongwa na pikipiki maeneo hayo hayo ila nashukuru Mungu hakuumia sana ila kibaya zaidi kila siku anakoswakoswa na pikipik au gari.

Sister ameniambia nitafute sehemu nimpeleke maana hapo sio salama kwa mtoto mdogo, huwa najitahidi kushinda nae ila siku nyingine inabidi nitafute hela hata ya kula maana maisha haya kukaa hivi hivi ni ngumu kwa mtoto wa kiume.

Msaada wenu unahitajika jamani, nikipata mtu wa kumpa huyu mtoto anisaidie kunilelea au hata kama akihitaji awe wake basi hamna jinsi maana ni bora mtoto aishi maisha yenye usalama kuliko kuishi maisha ya hatari. Shida kazi yangu ni fundi umeme, ningekuwa hata nauza duka ningeweza kupambana nae.
 
Nipo hapa nawaza ni mwanamke wa aina gani anayeweza kuzaa na kutelekeza mtoto tena mwaka na nusu ameanza na kuita MAMA

Anyway, mtoto hana bibi yake? Au hata kwa dada yako unaweza tafuta msaidizi wa kazi akawa anamuangalia hadi anaporejea toka kwenye biashara zake
 
Nipo hapa nawaza ni mwanamke wa aina gani anayeweza kuzaa na kutelekeza mtoto..tena mwaka na nusu ameanza na kuita MAMA

Anyway, mtoto hana bibi yake? Au hata kwa dada yako unaweza tafuta msaidizi wa kazi akawa anamuangalia hadi anaporejea toka kwenye biashara zake
Mi mwenyewe namshangaa huyu mwanamke kwa kweli maana mtoto mwenyewe ni wa kike na mzuri sana tu shida msichana wa kazI inabidi kumpangia chumba manaa kwa sister kumejaa.
 
Mi mwenyewe namshangaa huyu mwanamke kwa kweli maana mtoto mwenyewe ni wa kike na mzuri sana tu.shida msichana wa kaz inabidi kumpangia chumba manaa kwa sister kumejaa.
Msichana wa kazi kaa nae wewe pamoja na mtoto kama na hilo haliwezekani basi.

Nina watoto wawili nipo kwenye harakati za kuchukua upande mzima (wapemba wanaelewa hapa) yaani vyumba viwili au vitatu na sebule kisha nichukue wanangu niajiri na beki tatu nikae nao, maana mama yao kishaolewa huko na hivyo nahitaji kuhudumia wanangu kwa ukaribu zaidi kuliko watoto kulelewa na baba wa kambo.

Sasa wewe mtoto mmoja tena wa kike, mimi nina wa kiume na wa kike hapa naumiza kichwa kutafuta hela.

Pia jiongeze mkuu usitegemee fundi umeme peke yake fungua hata kabiashara ka kuzugia ili isipite siku bila kuingiza hela
Maana unaweza kukaa wiki bila kupata kazi utaishi vipi?

Pambana mkuu baadhi ya vitu inabidi tufosi,

Siku zote mimi nikiwa na matatizo huwa najikubali na kujisemea, “hii ndo raha ya kuwa mwanaume”.
 
Msaada unaitajika ndugu zangu maana hata sijielewi kabisa kwa mambo yanayoendelea. Nilikuwa na mke wangu ila tukaamua kuachana baada ya yeye kuchukua vitu na kuondoka. Baada ya muda kaona haitoshi kamtelekeza mtoto wetu mdogo mwenye umri wa mwaka 1 na nusu kwa sister wangu.
We acha kuzingua jamaa angu.... Mbona una maamuzi mepesi sana juu ya mwanao mzee? Yani mtu amchukue we unaona ni sawa hiyo?

Keshagongwa na toyo bado unaona ni sawa yeye kukaa hapo? Tafuta dada wa kazi akae kwako akulelee mtoto wako..... Mtoto wa kwako nani atamlea, familia ya kwako nani atailea imba fungua njia kitoto kaanza tambaa!!!! Mkuu embu acha uvivu
 
Unataka kugawa mtoto wako akalelewe na kuchukuliwa na mtu mwingine. Huyo mtoto masikini amezaliwa kwenye shida na ni mtoto wa kike, mama kamtelekeza na baba anataka amgawe. Ningekuwa na uwezo ningemchukua nimlee kwa miaka hata mitatu maana naona kwa hapo lazima taifa lipate hasara.
 
Msaada wenu unaitajika jamani, nikipata mtu wa kumpa huyu mtoto anisaidie kunilelea au hata kama akitaji awe wake basi hamna jinsi maana ni bora mtoto aishi maisha yenye usalama kuliko kuishi maisha ya hatari. Shida kazi yangu ni fundi umeme, ningekuwa hata nauza duka ningeweza kupambana nae
Mkuu pole kwanza kwa changamoto hyo, ila usigawe mtoto tafadhali ilhali baba mtu upo.

Kama pesa ya kulipia daycare ni tatizo basi mwambie sister awaombe majirani zake wanaoshinda nyumbani wakae na mtoto, asbh kabla hajaenda kwa shughuli zake ampikie uji amuachie kwa chupa then amkabidhi jirani ashinde naye kuliko kumuacha mtoto mdogo nyumbani mwenyewe ni hatari tena sana.
 
Msaada unaitajika ndugu zangu maana hata sijielewi kabisa kwa mambo yanayoendelea. Nilikuwa na mke wangu ila tukaamua kuachana baada ya yeye kuchukua vitu na kuondoka. Baada ya muda kaona haitoshi kamtelekeza mtoto wetu mdogo mwenye umri wa mwaka 1 na nusu kwa sister wangu.
Kama upo Arusha nitafute tuongee nitakusaidia kwa kipindi ambacho hauna uwezo wa kumlea mpaka utakapokaa sawa
 
Back
Top Bottom