Msaada unahitajika; Je kuna uhatarishi (risk) kiasi gani kwa operesheni ya kichwa

NyaniMzee

JF-Expert Member
Nov 24, 2010
396
727
Wakuu na madaktari mliopo jamvini.
Naomba mnijuze. Nina mjomba wangu ana miaka karibu 90 na amefanyiwa vipimo na kuonekana kuna maji katika kichwa chake yaliyosababishwa na mgando wa damu. Madaktari wamependekeza afanyiwe upasuaji kichwani kesho ili kutoa maji hayo. Binafsi naona hiyo operesheni ni risk kubwa kwa maisha yake. Naomba maoni yenu wakuu.

Natanguliza shukurani.
 
KICHWA NDO UFAHAMU WENYEWE MKUU,WAKIKOSEA KIDOGO UNAKUWA KICHAA,KUPOOZA AU HATA KIFO
 
Wazo langu naliweka kapuni kwanza.

Uhai wa mtu si wa mchezo mchezo kabisa
 
Kichwa ndo engine ya mwili wa binadamu kama mafundi wenyewe ni wa mtaani wa elimu za kuunga unga kama bashite mjomba wako aandae wosia mapema cuz hatutokuwa nae tena
 
Kichwa ndo engine ya mwili wa binadamu kama mafundi wenyewe ni wa mtaani wa elimu za kuunga unga kama bashite mjomba wako aandae wosia mapema cuz hatutokuwa nae tena
Hospital yenyewe ni St Gaspar iko Itigi kwa wale wanaoifahamu.
 
sasa ili apone mnakubali tu mnafanyeje..

mama yangu kafanyiwa operation ya kichwa zaidi ya mara moja. ila matokeo hayakuwa mabaya... tena kwenye ubongo kabisa..

sema alifanyiwa india... sasa kama ndio pendekezo la madaktari afanyiwe tu ili apone
 
sasa ili apone mnakubali tu mnafanyeje..

mama yangu kafanyiwa operation ya kichwa zaidi ya mara moja. ila matokeo hayakuwa mabaya... tena kwenye ubongo kabisa..

sema alifanyiwa india... sasa kama ndio pendekezo la madaktari afanyiwe tu ili apone
Nashukuru kwa encouragement yako
 
Back
Top Bottom